ccm

Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho chama tawala nchini Tanzania na chama cha pili kwa muda mrefu zaidi barani Afrika, baada ya Chama cha True Whig cha Liberia. Kilianzishwa mwaka 1977, baada ya kuunganishwa kwa Tanganyika African National Union (TANU) na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar.
  1. CCM msikosee kurudisha hawa wazee wasioridhika, mtalia

    Chama changu CCM, kama hàmjajua, wapinzani wako macho wana hamu kuona mnachagua nani. Naomba niwajuze; msikosee kurudisha wale wazee wasioridhika. Kuna wazee wamekaa jimboni miaka 10-15-25 kama vile bunge ni lao, hakuna mwingine wa kuwapokea. Naomba tusikosee kwa hili. Nawatakia uteuzi mwema...
  2. Dalili zinaonyesha hakuna msaliti wa upinzani atakayepenya kwenye kura za maoni ndani ya CCM

    Kuna kila dalili kuwa hakuna mwanasiasa kutoka upinzani ambaye alihamia CCM ili kuunga mkono juhudi (maarufu kama wasaliti) mwenye nafasi ya kupenya katika kinyang'anyiro kinachoendelea sasa cha kura za maoni ndani ya CCM kwenye ngazi yoyote ile, iwe ubunge, udiwani au viti maalum. Wasaliti wote...
  3. Zitto anajua nini anafanya

    ZITTO ANAJUA NINI ANAFANYA. Mbowe alipompeleka Lowasa CHADEMA (inasadikika kidikteta) alisema wamebadilisha gia angani. Mbowe alikuwa anaamini Lowasa atashinda uchaguzi, alitegemea kuwa ile mitandao ya Lowasa italinda kura na CHADEMA kitashika madaraka. Baada ya matokeo ya uchaguzi (inasadikika...
  4. Kauli ya Mwenyekiti Taifa CCM kwamba kila mgombea ajipiganie inatulaza roho juu tuliounga juhudi, hatuna mizizi CCM, tusaidiwe

    Leo tutapata usingizi wa tabu sana, CCM mnatutupa kweli? Upendo mliotuonyesha umeishia wapi? Jamani jamani Kamati Kuu, hasa Mwenyekiti, hatuna mizizi katika chama na tutabaguliwa, hawa wapiga kura na wanaCCM tuliowakuta ni waarabu wa Pemba,wanajuana kwa vilemba,tunaomba upendeleo maalum
  5. Kila Jimbo la "Muunga mkono juhudi" limebana. Asanteni sana magwiji wa CCM mlioamua kurudi

    Yaani dili limetiki 100 asilimia, kila tunachopanga na kutarajia kina tiki. Hatua ya kwanza kabisa tayari tumefanikiwa kwa asilimia zaidi ya 96. Mambo yanaenda bam bam. Tunasubiri hatua ya pili mchujo wa kura za maoni na hatua ya tatu vikao vya maamuzi ambayo yote hayo yameshaonyesha kufanikiwa...
  6. T

    Mara, Kigoma, Tabora, Kagera wagombe CCM ni PhD, mikoa ya pwani Morogoro, Lindi, Mtwara, Pwani na Tanga ni kujua kusoma, kuandika na pesa

    Halafu mtu analalamika kuwa JPM anapendelea wabunge wa mikoa ya bara katika kuunda Baraza la Mawaziri. Tunapoingia uchumi wa kati ndugu zangu changueni wabunge wasomi. Hawa ndio wenye sifa ya kumsaidia mhe. JPM. Achaneni kumchagua mtu kwa vigezo vya pesa, mnasikia ndugu zangu hasa wa mikoa ya...
  7. GE2020 Vicent Mashinji achukua fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Kawe kwa tiketi ya CCM

    Aliyekuwa Katibu mkuu wa CHADEMA kabla ya kuhamia CCM, Vincent Mashinji amechukua fomu ya kugombea Ubunge katika jimbo la Kawe jijini Dar es Salaam kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi. Jimbo hilo la Kawe lilikuwa chini ya Mbunge aliyemaliza muda wake, Halima Mdee kutoka chama cha CHADEMA. Aidha...
  8. GE2020 Tamaa za Wateule wa Rais kutia nia Ubunge zitawaponza wengi. Ushahidi huu hapa wa Rais Magufuli na Humphrey Polepole

    KUNA FUNZO LOLOTE KWA SASA? Aprili 2019 Rais Magufuli ktk moja ya vikao vya ndani ya chama cha CCM, amemlaumu Naibu Waziri wa zamani wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na aliyewahi kuwa pia RC Tabora ndugu Ludovick Mwananzila kwa kumwita mwenye tamaa nyingi sana. Mwananzila alishika nafasi ya...
  9. GE2020 Sylvester Mujuni 'Mpoki' achukua fomu kuomba ridhaa ya CCM kugombea Ubunge Jimbo la Kigamboni

    Mpoki amejitokeza kuomba ridhaa ya CCM kugombea Ubunge Jimbo la Kigamboni. Mpoki ni msanii wa vichekesho, mshehereshaji, mtangazaji wa kipindi cha Ubaoni redio ya EFM na pia ni mwimbaji wa nyimbo za kugani. Pia soma > Mpoki ndio mchekeshaji bora wa stand up comedy kwa Tanzania > Huyu Mpoki vipi...
  10. K

    Jicho la Tatu ziara ya Mteule Urais CCM Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi

    Naam, ni wakati mwengine tunakupatia taarifa. Jana tarehe 15 Julai, 2020 kulikuwa na mapokezi ya Mteule wa urais wa CCM Zanzibar dkt Hussein Mwinyi. Ziara ilifana na iliandaliwa vya kutosha. Tutatoa tathmini fupi kutokana na taarifa zetu. Shabaha na kupima upepo. Ziara si tu kwamba ilenga...
  11. Ikulu, Dodoma: Rais Magufuli amewaapisha Viongozi Wateule mbalimbali, amewasisitiza kuridhika na nafasi walizoteuliwa

    Viongozi Wateule walioapishwa Leo ni: 1. Bw. Aboubakar Kunenge- Kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam 2. Bw. Joseph Joseph Mkirikiti - Kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara 3. Bw.Paulo Mshimo Makanza - Kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam 4. Bw. Gabriel Pascal Malata- Kuwa Wakili Mkuu wa Serikali...
  12. GE2020 Wingi wa wagombea CCM ni uthibitisho kazi nzuri ya Rais Magufuli kwa taifa letu. Je, Oktoba ni kuchagua au kuthibitisha tu taratibu?

    Wanabodi, Tunapoelekea kwenye hatua ya kwanza ya uchaguzi kwa uchukuaji wa fomu za kugombea kwenye vyama vya siasa, kumejitokeza, uwingi wa mkubwa, wa wagombea kupitia CCM. Huu ni uthibitisho wa kazi kubwa na nzuri iliyofanywa na Rais, Dr. John Pombe Joseph Magufuli na awamu yake ya 5, na...
  13. GE2020 Ni muujiza pekee utakaoifanya CCM wabaki wamoja baada ya uchaguzi utakaofanyika mwishoni mwa mwaka huu

    Kuna mlolongo wa matukio yanayotokea nchini hivi sasa, yanayonifanya niweze kutabiri yatakayotokea nchini baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika nchini kwetu mwishoni mwa mwaka huu Tulimsikia wenyewe Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Magufuli akitamka hadharani bila kificho chochote kuwa kura za...
  14. Ahadi za Rais Magufuli kwenye uchaguzi wa 2015, ambazo ziligeuka uongo

    Wanajamvi, kitu nawachukia wanasiasa ni uongo. Kuna mtu alisema “mwanasiasa akikwambia sasa hivi ni mchana, kama mko ndani, toka nje uhakikishe jua lipo” Chini hapo ni hotuba ya Maghufuli siku anafungua kampeni 2015. Kiaina naona kama kila alichoahidi, kafanya kinyume kabisa! Imekaaje hii...
  15. GE2020 Zitto Kabwe ndiye atakayesababisha CCM waingie Ikulu kiulaini 2020

    Mimi si mwandishi mzuri,ni mvivu kuandika mambo kwa undani. Nitaandika short & clear. Ndani ya miaka 5 ya uongozi wa Mh. Magufuli Watanzania kama wafanyabiashara, watumishi wa umma na watumishi wa sekta binafsi, wakulima wa mazao mbalimbali wamepitia kipindi kigumu. Hata wananchi wa kawaida...
  16. L

    Hizi ndizo sababu kuu za mafuriko ya watia nia CCM

    Mwaka 2019 rafiki yangu wa karibu alinishauri ifikapo 2020 nigombee ubunge. Baada ya kukataa ushauri wake alisema ndani ya CCM hususana serikali ya awamu ya 5 hata ukishindwa ubunge unaweza fikiriwa nafasi nyingine za uteuzi kama ukurugenzi, ukuu wa mkoa, wilaya na makatibu tawala mikoa na...
  17. GE2020 Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqqaro achukua fomu kuomba ridhaa ya kuwania ubunge jimbo la Babati Vijijini kupitia CCM

    Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro amechukua fomu kuomba ridhaa ya kuwania ubunge jimbo la Babati vijijini kupitia Chama Cha Mapinduzi-CCM
  18. GE2020 Aliyekuwa mbunge wa Ndanda (CHADEMA), Cecil Mwambe aibukia CCM kuchukua fomu kutetea jimbo

    Aliyekuwa Mbunge wa Ndanda kupitia CHADEMA, Cecil Mwambe amechukua fomu ya kugombea Ubunge wa Jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020 kupitia Chama cha Mapinduzi.
  19. GE2020 Muhsein Awadhi Said (Dkt. Cheni) achukua fomu ya kuwania Ubunge Ilala kupitia CCM

    Muhsein Awadhi Said (Dkt. Cheni) Muigizaji Mkongwe na Mshereheshaji maarufu amechukua fomu ya kuwania Ubunge katika Jimbo la Ilala kupitia Chama cha Mapinduzi. Baada ya zoezi la kuchukua fomu hiyo Dkt. Cheni aliongea kwa kifupi na Waandshi wa habari kuwa yeye ni mzaliwa wa Ilala kwa sasa...
  20. Tuwe wakweli: Ubunge umekuwa rahisi na usiotisha tena. Kuna wa kulaumiwa au kupongezwa?

    Mimi si mtu mzima sana ingawa nami najongea miaka ya kuweza kugombea Urais wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba yetu ya sasa(miaka 40). Hatahivyo, nimekuwa mfuatiliaji mkubwa wa siasa na mambo ya kinchi tangu nikiwa mdogo. Leo, nitalizungumzia Bunge kama Mhimili mmojawapo wa dola. Mingine, wengi...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…