Hili suala la mwekezaji wa Mlimani city ni baadhi tu ya machache yanayotia dosari chuo chetu hiki kikongwe nchini, ni vizuri pia ukafanyika uchunguzi kuhusu matumizi na mapato ya hiki chuo. Wafanyakazi wengi wa hichi chuo hawana motisha kabisa ya kufanya kazi hapo, ubora wa chuo unapungua kila...
Inashangaza sana, yani pamoja na Magu kukisifiasifia sana hali ndio hiyo!. Kuna watu wangu wananiambia utakuta Professor ana wanafunzi 25 darasani lakini Assitant Lectuter ana wanafunzi 300 darasani halafu hapati allowance yoyote zaidi ya mshahara anaopata. Hapa lazima kuwe na vinyongo sana.
Hii barabara sasahivi hali ni mbaya kupita kiasi hasa ukizingatia magari mengi yanatumia hiyo njia. Zaidi ya mwezi sasa viliwekwa vifusi ambavyo mpaka leo havisambazwa mpaka vifusi vingine vimesombwa na mvua, hii nayo imeongeza kero kwenye hiyo barabara. Nashindwa kuelewa kwanini tunapata hii...
Hawa jamaa sasa hivi mbona ni kama wanatukomoa wananchi?, maana akikusimamisha anakuomba leseni hapohapo anaanza kupunch machine yake, hakuna muda wa kukuambia kosa lako na wewe kujitetea, hivi wanafikiri hizi elfu 30 tunaziokota au?. Awali nilifikiri labda sisi wananchi ndio tuna shida lakini...
Hii habari ya hapa kazi tu kuna wengine imewashinda. Tuishio Kimara ni zaidi ya wiki sasa hatuna maji bila taarifa yoyote. Umeme nao ni kero, ukiripoti tatizo siku itaisha bila tanesco kulifanyia kazi. Sasa nauliza hii HAPA KAZI TU kwa hawa jamaa nayo ipo likizo ya christmas na mwaka mpya au...
Mbona kila fundi ni muongomuongo tu, tapelitapeli tu.
Uwe fundi nguo, fundi ujenzi, ukishaitwa fundi tu ni kama vile laana, why?
Kwanini mpo hivyo?
Kwanini mnaharibu sifa zenu?
Tatizo ni nini?
Ingekuwa mimi ni waziri wa Elimu ningerudisha Ardhi University UDSM, maana yanayoendelea sasahivi kwenye hivi vyuo hata sielewi zaidi ya kusema ni ulafi wa madaraka hasa ukizingatia ukaribu wa hivi vyuo viwili.
Ardhi ilijitenga na UDSM lakini ikaja kuanzisha kozi ambazo zipo UDSM mfano Civil...
Habarini wakuu,
Nafikiri na hawa nao wa Insurance za magari walitakiwa walipe VAT kwenye malipo yaleyale ya awali.
Kinachofanyika sasa ni kumlipisha mlipaji.
Nakupongeza sana kurudisha heshima ya Elimu na Wasomi. Hujakosea kumchagua Ndalichako kwenye wizara hiyo muhimu. Usikatishwe tamaa na maneno ya vilaza. Simama Imara. Safisha kila mahali. Elimu kwa kipindi kirefu imekuwa ni kama mchezo, watu hawapo serious, wanafanya mambo vile wanataka, ukiwa na...
Maeneo ya Kimara tumekuwa na matatizo ya kukatikakatika umeme mara kwa mara bila ya taarifa yoyote zaidi ya mwezi sasa, na uweza kurudi hata baada ya masaa 24.
Tatizo ni pale ukipiga namba yao ya simu (0788 379 696) mara nyingi huwa ipo bize au itaita tu bila kupokelewa (Jaribu hata sasahivi)...
Lugha ya kufundishia iwe kiswahili kuanzia shule za awali mpaka vyuoni. Shida zote tunazozipata kwenye elimu zitapungua sana, tutapata vijana wengi ambao sio mzigo kwa Taifa.
Nasikitika kusema wakazi wa Kimara hatujapata maji kwa muda mrefu. Leo yametoka kwa nusu saa tu.
Tatizo langu ni kwanini hakuna taarifa zozote kuhusiana na hili.
Hiyo nusu saa ni majaribio au!.
Naona kwenye magazeti zoezi linaisha leo. Najiuliza limeanza lini!. Ni kweli limekuwa likifanyika!. Nikaona labda shida ni mimi, nikajaribu kuuliza watu kama kumi hivi kuona kama wanafahamu, hakuna hata mmoja aliyekuwa anajua chochote kuhusiana na hilo. Nafikiri kuna tatizo mahali. Inawezekana...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.