Kero yangu ni kucheleweshwa kwa mradi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Alinato mpaka Posta inayojengwa na kampuni ya CRJE.
Imefika miezi mitatu sasa haijafanyiwa marekebisho tangu walivyoichimbua...
Hawa jamaa ni very conservative, slow, backward and premitive institution.
Upande wa customer care ni wabovu na wameoza. Unaweza kuweka hela zako vizuri kabisa ila kuzitoa sasa utazungushwa kama...
Mimi ni Mwananchi wa Wilaya ya Mbeya Vijijini nina kero ambayo inatutesa sana wakazi wa huku.
Kero kubwa iliyopo ni ubovu wa barabara ya kutokea Mbalizi, hadi Iwiji ambapo inapita Isangati...
Kuna daraja lipo Kibaha Mji, Kata ya Pangani, Mtaa wa Lumumba (liko karibu na Daraja la Jeshi) liliharibika wakati wa mvua ya Mwaka juzi (2024) ile kubwa lakini mpaka leo halijatengenezwa tunapata...
Huku kwetu kuna Shule ya Serikali inayoitwa Shule ya Msingi Tambani, ipo Mbande Mwisho, Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani ina changamoto ya uhaba wa madarasa na madawati na pia miundombinu yake...
Ujenzi wa barabara ya Ali H. Mwinyi eneo hili la Mbuyuni, Ada Estate, Kinondoni umeathiri miundombinu ya maji taka. Bomba la maji taka linamwaga maji hapa jirani na Gudal Petro Station zaidi ya...
📍 – Bunju “B”
Kwa wanaopita barabara ya Bagamoyo jioni, hasa eneo la Bunju ‘B’, hali ya foleni imekuwa ya kawaida kila siku.
Tatizo kubwa ni:
Daladala kuegesha kiholela barabarani badala ya...
Kero ya matakataka Mitaa ya Mbagala Kuu ni zaidi ya miezi mitatu sasa hakuna gari la taka lilopita mtaani kwetu. Matakataka yamezagaa na ukizingatia sehemu za wazi ambazo Watoto wanacheza...
Stendi ya Mawasiliano ni eneo lenye muingiliano mkubwa wa watu kutokana na uwepo wa soko pamoja na mabanda mengi ya biashara. Licha ya umuhimu mkubwa wa eneo hilo, upatikanaji wa huduma ya choo...
Tunawaandikia kama mawakala wenu tukitoa malalamiko yetu rasmi kuhusu huduma za umeme (LUKU) na controller number, ambapo kwa muda mrefu hakuna kamisheni inayolipwa kabisa huku makato ya miamala...
Ni wazi kuwa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshindwa kutekeleza wajibu wake wa msingi wa kulinda mazingira na ustawi wa wananchi. Moja ya mifano ya wazi ni...
Kwako Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Dr .Aaron Kagurumjuli , MADEREVA wa mkataba tumekuwa tunacheleweshewa mishahara kila mwezi hivo kupelekea kufanya kazi kwa mawazo,
Kazi yetu inahitaji kuwa...
Tunatambua tangu matukio yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi 2025 yamesababisha usimamizi wa usafi na mazingira kuzorota, hofu ikiwa kwa Wanasiasa kuogopa lawama za Wananchi.
Hii imesababisha...
Kero yangu ni kukatika-katika kwa umeme mara kwa mara katika eneo la MATIKA, Kata ya Lugarawa, Wilaya ya LUDEWA, Mkoa wa Njombe huku wahusika wakikaa kimya bila kufanyia ufumbuzi suala hili...
Dar es Salaam ni jiji lililo na mito inayotiririsha maji kuelekea baharini, lakini kwa muda mrefu kumekuwa na uhaba wa maji. Kwa muda mrefu jiji hilo limekuwa likitegemea maji ya mto Ruvu unaopita...
Sisi watumishi wa Idara ya Afya tulioajiriwa tarehe 23 Juni 2025 katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji, tunatoa malalamiko yetu rasmi kuhusiana na kutolipwa kwa pesa zetu za kujikimu ambazo kisheria na...
Sisi Watumishi wa Umma ambao ni waajiriwa wapya Serikalini katika Kada ya Afya, Halmashauri ya Kilosa Mkoani Morogoro tuna changamoto ya kutolipwa stahiki zetu za fedha za kujikimu na majibu...
Ndugu zangu, hali ya upatikanaji wa maji katika Kijiji cha Mayonje, Kata ya Milepa katika Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini, imekuwa ya kusikitisha sana, tangu mwezi wa 11, 2025 mwanzoni baada ya...
Wananchi wa Kijiji cha Mayenje, kilichopo Kata ya Milepa katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga (DC), hatuna huduma ya maji safi kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu.
Chanzo cha tatizo hili...
Niwe mkweli sijawahi ona halmashauri wazembe, wala rushwa, wavivu kama halimashauri ya Msalala-Kahama.
Halmashauri hii imegeuka kuwa kilio kwa watumishi wa umma, ukiwa na shida husikilizwi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.