Kama chama kikuu cha upinzani nchini, wapenda demokrasia tunawatetea na kuwategemea. Kama chama kikuu cha upinzani nchini,tunatarajia mjipange na kuwinda ushindi mwaka 2020. Lakini,mnazingua.
Kwasasa hamuainishi hoja mnazozisimamia kama ilivyokuwa wakati ule wa kupinga ufisadi. Kwasasa mmekuwa mkiibuka na hoja zinazotokana na yanayosemwa. Yaani,hoja za kudandia. Mnazingua.
Lengeni kuongeza Wabunge na Madiwani mwaka 2020 badala ya kukesha na vijembe twitter,youtube na facebook. Acheni kuyumbayumba na kudaka hoja zisizo na msingi. Mnazingua.
Jipambanueni kwa hoja. Jengeni chama chenu na kuwatumikia wananchi waliowaamini majimboni,katani,vijijini na vitongojini. Hakuna faida ya kubishana kila kukicha na vyombo vya dola na Serikali. Pigeni kimyakimya. Acheni kuzingua!