Kweli yanayojiri hivi sasa yanafurahisha. Hivi kweli majeshi yetu (JW, Polisi, Zimamoto na Uokoaji, MAGEREZA, Uhamiaji) yanapopita mabarabarani yakiwa kwenye dharura inabidi hivi sasa sisi wananchi tuwasimamishe na tusiwapishe hadi tutakapowahoji watufahamishe ni dharura gani wanayoenda...
Hamza kuua Polisi siyo hoja ya msingi kwenye hii mada. Mtu yeyote anaweza kuua kwani haya tumeyashuhudia sehemu mbalimbali hata huko Marekani. Hao Polisi wetu unaodai kuwa hawana mafunzo ya kutosha nao wanaweza kuua hata mara kumi ya hao.
Tunachozungumzia hapa ni Weledi na Uadilifu wa Polisi...
Njia za kuwasiliana kwa Polisi zipo lukuki. Pamoja na Radio Calls pia mawasiliano hufanyika kwa njia ya simu. Haiwezekani kila askari Polisi kuwa na Radio Call kwa mawasiliano.
Tanzania tuna Polisi wapatao takribani 50,000. Kosa lolote linapofanywa na askari Polisi mmoja (kama kweli ni kosa) si busara kutoa blanket conclusions, yaani za kiujumla jumla. Polisi ni binadamu na wanatoka katika Jamii zetu. Ni watoto wetu, ni ni kaka na dada zetu na wengine ni baba na mama...
UHALIFU ni tabia ambayo inajengeka kutokana na mazingira, malezi, makuzi, maadili nk. Huwezi kuhalalisha uhalifu sababu ya wewe kuwa na njaa kali au ugumu wa maisha. Muhimu hapa ni kupewa elimu na kama itashindikana ni sheria kuchukua mkondo wake bila huruma.
Ugumu wa maisha ni kipimo cha akili...
Mkuu, umeanza vizuri hapo mwanzo lakini umeharibu katika mwendelezo. Suala la kitaaluma linahitaji fikra pevu na ukomavu wa mawazo, hoja na rai. Hekima kubwa, busara pamoja na maarifa hujenga hoja mujarabu.
Jitahidi kujiweka mbali na mawazo mgando, mahaba na hisia binafsi za kisiasa (prejudiced...
Ili kuweza fanikisha mapambano dhidi ya hawa Panya Road lazima turudi katika taratibu za malezi ya miaka ya nyuma. Tunapaswa kuwajibika katika malezi ya watoto wetu kuanzia ngazi ya familia. Wazazi, walezi na ndugu tunapaswa kuwa karibu sana katika kuwalea vema kwa kuwafundisha tabia njema na...
"PANYA ROAD" ni watoto wetu wenyewe. Tunaishi nao tunakula nao na tunalala nao pamoja kwenye nyumba zetu. Na hata wanapoleta mavuno yao ya uhalifu tunashiriki nao katika kufaidi matunda ya uhalifu wao. Hivyo tusijitoe ufahamu kwa kuwa tunawajua vizuri.
Dawa si kwaua kama baadhi wanavyodai. Hapo...
Kiswahili ni lugha ya taifa na inaeleweka kiurahisi na wengi. Kwa nini ujichoshe kiasi hicho kutumia lugha ambayo hauna umahiri nayo. Umeshindwa kufikisha ujumbe sahihi uliokusudia sana sana tu umechosha na andiko lako.
Safari nyingine Tumia Kiswahili au pata msaada wa wanaojua Kiingereza...
Mamlaka husika huko Zanzibar imeishalitolea taarifa suala hili hivyo tuache mihemko tusubiri taarifa ya uchunguzi ambayo inadaiwa tayari umeishaanza.
Angalizo ni kwamba tuwe makini sana na uchunguzi wetu, tukitilia maanani timing ya haya malalamiko ambayo yanadaiwa kutokea Mwaka mzima uliopita...
Hao siyo wanafunzi tena, wengi wao ni wahitimu na ni viongozi sehemu waliko. Kuhusu ubaguzi nadhani ungefanya utafiti kidogo tu kujua kuwa wengi wao ndoa zao ni za mchanganyiko wa rangi
Mbona yule mwenye dawa alfulela ulela za kutibu kila ugonjwa duniani na kuwa na maduka ya dawa zake nchi nzima na matangazo lukuki; lakini mwenyewe alishindwa kujisaidia na akaanguka hadharani siku ya harusi yake hayumo? Hii siyo "double standard"?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.