Salamu waungwana,
Ninawashukuru sana waliojitokeza kufuatilia matatizo yanayonikabili na familia yangu kupitia bandiko nililoliweka humu kuomba msaada. Msamaria mmoja aliamua kunipatia makazi ya nyumba huku Madale mwingine akanisaidia usafiri wa kuhamisha vitu na familia toka Magomeni hadi...
Nipo Dar, nina hamu sana ya kujifunza na kuendesha kilimo hicho kuanzia mwezi ujao. Kama unaweza kunifundisha kwa vitendo hadi kufuzu na kuwa na uhakika wa kilimo hicho na soko lake tuwasiliane zaidi.
Hii ID ni ya mume wangu huwa naingia na kutumia kama suala ni la kifamilia na mara nyingi huwa tunashauriana na kukubaliana hivyo kutokana na hali yake kama nilivyoeleza kwenye mada husika. Sijaona ulazima wa kuwa na ID yangu humu kwa vile hata nikitaka kuingia humu natumia hii hii na ili...
Bado sijapata mteja. Ndicho kitanda pekee cha watoto nilichoongelea hapa kuwa imebidi niuze lakini hadi sasa sijapata wa kukinunua kama umenisoma vizuri mkuu.
Habarini wana JF wapendwa, mimi naitwa Telesia Mdumula. Nina mume na watoto 5. Tunaishi Magomeni Dar. Mtoto wa 1 amemaliza la 7 mwaka huu na kupata `B` tunatarajia atachaguliwa kidato cha 1 mwakani. Wawili wanaingia la pili mwakani na wawili waliobaki bado wadogo sana. Mume wangu ni mlemavu wa...
Waungwana nauza kitanda double decker cha chuma chini ni futi 5x6 na juu futi tatu na nusu kwa sita. Ni kizuri na imara nauza pamoja na godoro lake la juu. Bei sh. 350,000/= pungufu tunaweza kuongea. Nipo Magomeni Dar. Nimeshindwa kuattach picha. Yeyote anayehitaji tuwasiliane kwa PM au anipigie...
Mkuu hizo lita 100 au 200 unapata kwa mtu mmoja au unakusanya kwa kuzunguka kwa mfugaji mmoja mmoja hapo Mkuranga? Hao wafanyakazi 2 au 4 wanasambaza maziwa wapi? Soko la uhakika la kuuza lita 100 au 200 lipo wapi au ni kwa kutembeza mwenyewe kwa kutumia hao wafanyakazi?
Wakiwezeshwa wanaweza, tatizo la hapa Tanzania na nchi nyingi za Afrika watu wenye ulemavu hawapewi fursa kulingana na mazingira ya ulemavu wao. Hata Serikali ni kama vile haijui hili. Walemavu wamebaki kupambanishwa tu na wasio na ulemavu wowote bila kuzingatia mahitaji maalum ya ulemavu wao.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.