Nateseka na wanangu, wasamaria wema nisaidieni nipate pa kuishi na mtaji wa genge

Sawia

Senior Member
Feb 9, 2013
129
40
Habarini wana JF wapendwa, mimi naitwa Telesia Mdumula. Nina mume na watoto 5. Tunaishi Magomeni Dar. Mtoto wa 1 amemaliza la 7 mwaka huu na kupata `B` tunatarajia atachaguliwa kidato cha 1 mwakani. Wawili wanaingia la pili mwakani na wawili waliobaki bado wadogo sana. Mume wangu ni mlemavu wa kusikia na kwa miaka yote huko nyuma alikuwa akifanya kazi kwenye NGO moja kwa mkataba wa muda mfupi mfupi kutegemeana na uwepo wa pesa kwenye miradi aliyokuwemo.

Malipo yake hayakuwa makubwa ila ilisaidia kulipia kodi ya vyumba tulivyopanga kwa wakati, chakula, shule kwa watoto na kidogo nilimsaidia kuzungushia kwenye genge nililouza kuongezea pato.

Mwezi Juni mwaka huu wafadhili wa mradi aliokuwa akifanyakazi mme wangu walisitisha ghafla kutokana na sababu za kiuchumi. Ilibidi wafanyakazi wote waliokuwa kwenye mradi huo waondoke na kutafuta namna nyingine. Mme wangu hadi sasa anahangaikia vibarua ambavyo hata hivyo havipatikani kirahisi na vikipatikana malipo ni kidogo sana.

Baada ya hali kuwa ngumu sana ilibidi tutafute vyumba vya kodi nafuu bondeni tulipata viwili vya elfu 40@,tuliweza kulipa miezi 3 ila mwezi wa 9 kodi ilipoisha tukawa tumekwama kabisa.

Hadi sasa mwenye nyumba anataka tuondoke maana tumeshindwa kulipa kodi yake na nyumba yake ni ya biashara ili apate pesa ya kusomesha wanae shule za kulipia. Hapa tunapoishi bado si salama kwa mafuriko na wakati wowote tunaweza kubomolewa ila hatuna namna nyingine kabisa.

Maisha yamekuwa ya kubahatisha sana tukitegemea genge ambalo nalo halina mtaji na kodi yake ya miezi 6 sh. 180,000 imeisha mwezi uliopita na hatujui tutaipataje.

Tumekuwa tukiishi kwa mlo mmoja tu kwa siku na mara nyingi tumekuwa tukishinda na kulala njaa na watoto. Tumejaribu kutafuta mkopo ila tumekwama kwa kukosa vitu vinavyokubalika kwenye dhamana. Hata vitu vyetu vidogo vya ndani tumejaribu kuuza tupate hela kidogo ya kula na kununua vitu vya kuuza gengeni ila hatupati watu wa kununua. Sasa hivi tumeamua tuuze kitanda cha watoto lakini hatuoni mteja hata mmoja.

Mateso tunayopitia na watoto ni makubwa sana japo hatujakata tamaa. Ninaomba sana wasamalia wema humu JF watusaidie niweze kupata na kulipia kodi ya vyumba 2@40,000 sh. 480,000, kodi ya genge kwa miezi 6@30,000 sh. 180,000 na mtaji wa genge sh. 150,000. Yeyote anayetaka kuona na kuhakikisha mazingira ninayoishi na wanangu anakaribishwa sana.

Namuomba sana Mungu awabariki wote watakaoguswa na tatizo linalonikabili na wanangu pia Mungu awabariki zaidi watakaonisaidia. Shukrani kwenu wote. Namba yangu ya simu ni 0715597591.
 
Itabidi tumshauri@Invisible tuwe na jukwaa la wenye shida na kutaka misaada.
 
Nadhani kama mtu wa kumsaidia una uwezo wa kumsaidia unamsaidia ..ila hawa watu wa magomeni sina imani nao sana..nadhani watu JF wawe na kitengo cha kuapprove kuona kweli hawa watu wanahitaji msaada au ni usanii..
 
Niliona King'asti anasema analo shamba la kulima.

Wasiliana naye upate ajira.
 
Bad timing aisee pamoja na shida yako nijuavyo sisi waTz watadhani ni kama imemuiga yule jamaa wa kuezeka nyumba. Pole sana but timing yako iko pabaya
 
Kama ni kweli I feel very sorry kua upo kwenye hali hiyo, najua kufika kwenye hali kama hiyo mtu unaweza kua very down na ukaona dunia nzima iko upside down. Ila kama mtu unayeomba msaada kwa nini uanze na kuomba msaada wa kusema ulipie vyumba 2 miezi 6.. Mtu aliye katika hali yako angekuja kusema apate angalau msaada wa chumba kimoja kwa hata wiki mbili, yaani ndivyo mtu aliye desperate alivyo, ila kusema unataka msaada wa vyumba 2 miezi 6, sijui nini kingine miezi 6, biashara yako miezi 6. Usimuwekee conditions mtu unayemuomba msaada hata siku moja.
 
watoto watano bila kazi ,pole mama,mimi mwalimu sina mke ila maisha nayaona magumu
 
Ndo haya nimetoka kusema kuwa "shida zina miguu"
Wakuu msibeze shida ya mwenzetu eti kisa mmemetoka kumsaidia MKONGORO
Roho ya upendo na uthamani mliyotumia kumuokoa mwenzetu yapasa vivyo hivyo itumike kumsaidia na huyu naye!
Kama jinsi tuendavyo kuona wagonjwa hospitali na kukuta halaiki ya watu wasio kuwa na siha njema wakipata matibabu, vivyo hivyo na haya matatizo mengine ndo yanavyo tusibu!

Tuwachangie wenzetu walio ktk hali ngumu mbona michango ya sherehe hatuhoji vile inavyo tuandama kila iitwapo leo?
Kutoa ni moyo...
 
Last edited by a moderator:
Ushauri mzuri. Mmejaribu kuangalia swala la kurudi mkoani au kijijini mkajiendeleze na kilimo?? Kilimo kinalipa watoto watasoma shule. Maana kuchangiwa kodi mtachangiwa mpaka lini? Mrudi nyumbani vijijini mjini maisha magumu
 
Hivi fashion ya kuomba mchango wa harusi alianza nani? Maana kama kuigwa ameigwa haswa angekuwa na hatimiliki ya huo ubunifu apew 10% angepiga dili kali kwelikweli.
 
Hii ni kuonyesha kuwa jamii forum inazidi kukuwa na kuaminika kwa jamii, jamani maisha hasa dsm ni zaidi ya vita. Mfano pita kariakoo usiku uone idadi ya watu wanalala kwenye makorido kuna haja ya wenye uwezo kuwasaidia wasio na uwezo. Napendekeza pia jamii forum kuanzisha na kuratibu jukwaa la wenye shida.
 
Ndo haya nimetoka kusema kuwa "shida zina miguu"
Wakuu msibeze shida ya mwenzetu eti kisa mmemetoka kumsaidia MKONGORO
Roho ya upendo na uthamani mliyotumia kumuokoa mwenzetu yapasa vivyo hivyo itumike kumsaidia na huyu naye!
Kama jinsi tuendavyo kuona wagonjwa hospitali na kukuta halaiki ya watu wasio kuwa na siha njema wakipata matibabu, vivyo hivyo na haya matatizo mengine ndo yanavyo tusibu!

Tuwachangie wenzetu walio ktk hali ngumu mbona michango ya sherehe hatuhoji vile inavyo tuandama kila iitwapo leo?
Kutoa ni moyo...

kwa uandishi wako inaonekana ni wewe wewe unatuchora tu hapa
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom