Hao wawili umesema ni waume za watu , kwa misingi hiyo unaendeleza mahusiano ambayo ni lazima yana madhara kwa familia zao, nadhani ni suala la muda tuu kila kitu kitakuwa wazi . Kwa upande mwingine umesema huyo aliye single umemsaidia kwa mambo mengi sana japo yeye ni mtu mgumu sana na...
Mkuu unamlaumu na kumuita mshamba kwa sababu amerudisha pesa ya mlevi, kwa hiyo wewe unajiona una haki kumuibia mlevi kwamba kwako wewe wizi siyo tatizo bali ulevi ndiyo tatizo. Badilika mkuu , wizi kwa tafsiri fupi ni kutwaa kitu/mali ya mtu mwingine bila ridhaa yake . Alichofanya ndiyo njia...
Iwapo hapakuwa na kikwazo kingine chochote unaweza mrudia ili mfunge ndoa iwapo wewe upo tayari kufunga ndoa
kama bado unajiona mdogo na muda wa kufunga ndoa haujawadia , basi mjulishe ili aendelee na Maisha yake.
Kwa kadri ya andiko lako unaonekana bado unampenda,mapungufu mengine ni ya kawaida...
Tanzania kwa sasa hatuna dairy farms, hivyo uzalishaji unategemea watu binafsi ambao wanazalisha Kiwango ambacho si kikubwa ku sustain kiwanda kwa mwaka mzima, Kwa miezi ya March hadi june maziwa ni mengi sana na yanaharibika kwa sababu hatuna storage facilities na reliable transport kuyatoa...
Halafu pia tambua kuwa, iwapo unalala saa 4 usiku na kuamka saa 12 asubuhi ujue hayo ni masaa 8 kwa hiyo katika siku yenye masaa 24 masaa 8 unakuwa umelala , hiyo ni theluthi moja (1/3) hivyo iwapo utaishi kwa miaka 60 inakubidi utambue kuwa 1/3 ya muda huo utakuwa umelala na hivyo hauzalishi...
Mkuu umeleta hii taarifa kwa wadau baada ya kuona siyo jambo la kawaida na bila ya kuuma uma maneno una mchango mkubwa sana kwenye kumuharibu huyo mtoto, tofauti kati yako na huyo mama yake ni jinsia zenu tuu, lakini kosa ama dhambi mnayofanya inafanana kabisa na ndiyo sababu umeendelea naye...
Iwapo wewe binafsi unaona mumeo mtarajiwa anania njema nawe kwa siku za mbeleni , na wakati huohuo wewe unataka ukamilishe ndoto yako ya masomo, na wazazi wako wameishajitoa kuhusu malipo yako ya ada, nakushauri UAHIRISHE masomo yako , ufunge ndoa, baada ya hapo iwapo bado utaona kuna unahitaji...
upo sahihi kabisa, apate mtaalamu wa lishe ambaye atamuanzishiya program ya diet ili kuongeza stamina , anapaswa kujua kuwa kuna mabondia wajanja watakuwa wanamkumbatia kila mara ili kuvuta muda na akifika kwenye raundi ya saba ama nane atakuwa kachoka na hapo ndiyo wataanza kumshambulia . Ni...
Kwa kawaida mtoto hawezi kuwa Analia tuu bila sababu, tafuta daktari mzuri bingwa wa watoto ama nursing officer wa muda mrefu wasilisha tatizo lako watakusaidia. Acha kabisa wazo la kuwapa kilevi. Utakapowazoesha kilevi utakuja jutia maisha yako yote yaliyobaki. Unapoona watu wazima wanatembea...
Mkuu, uafrica ni janga duniani, hii rangi nyeusi inahusishwa na mambo yote mabaya duniani . Utasikia nguvu za giza, umekuwa blacklisted, hata anapotafutwa kiongozi wa juu wa kanisa katoliki ni hadi utoke moshi mweupe na siyo mweusi.
Katika misingi hii nani atakubali umzalie mtu mweusi ?
Wapo wanaoifanya mkuu, Sinza alikuwepo mmoja, mwanzoni alikuwa ameajiriwa kwenye bucha Fulani lakini baadaye akafungua yake mwenyewe , tena hii ni tangia mwaka 2010
Hili siyo tatizo la Kigoma peke yake, mikoa yote ya mipakani tatizo hilo la mwingiliano lipo, Wamasai wa Kenya vs Wamasai wa Tanzania, Wakurya wa Kenya vs wakurya wa Tanzania, Wangoni, Makonde, wanyasa, wagunya, nk
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.