Nikimkumbuka yule jamaa aliyekuwa "apumnzishwe kwa amani" hivi karibuni ila akaokolewa na maafisa usafirishaji (bodaboda), huwa siielewi hiyo severeignity inayotetewa hapa!
NIjuavyo hii gesi ya kwenye mitungi (LPG) inatoka huko ughaibuni, hususan uarabuni. Siyo inayochimbwa hapa.
Ila naungana na wazo kwamba gesi yetu ya Mtwara bado haijatusaidia - kwa vile yenyewe inahitaji mfumo wa mabomba kusambazwa, na mfumo huo hakuna, isipokuwa kwa viwanda na watu wachache...
Ni kweli kwa watu wengi.
Lakini wapo wengi pia ambao kila mwezi au kila kipindi fulani wangewekeza japo kidogo kidogo, mfano kwenye mifuko ya uwekezaji wa pamoja, zikawafaa uzeeni. Unachukulia kama mchango wa harusi, unaweka, unasahau.
Ujengaji wa utamaduni wa kujiwekea akiba ni muhimu. Hata...
Mzabuni angekuwa ameshalipwa kila anachostahili kwa mujibu wa mkataba na bado asiendeleze ujenzi wangeshamchukulia hatua stahiki.
Naamini shida ni kwa mamlaka wenye mradi, yaani serikali.
Watu wa tabaka la kati waichukue hii, na hasa kipande cha kuwekeza sehemu ya mshahara katika maeneo ambayo fedha itakuwa salama (minimal risk) huku ikikufanyi kazi bila wewe kutoa jasho. Sehemu hizo ni kama hatifungani za serikali au za mashirika, unit trusts (hapa kwetu akina utt) nk.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.