Hivi huko siyo kuwachanganya vijana wetu kweli. Siku zote walikuwa wapi kutoa mwongozo mpaka wanasubiri mitihani imemalizika ndiyo mwongozo unatolewa?
Duuh, yaani wamekumbuka shuka wakati kumekucha!!! si mchezo kabisa.
Ha ha ha hahaha!!!! kama habari ndiyo hiyo basi elimu kwishey, kila kukicha ni kupanga alama tu badaala ya kuangalia namna ya kuboresha miundombinu shuleni. Mmmmmh, mpaka kawambwa amalize muda wake wa uwaziri 2015 atakuwa ameifanyia KWELI sana elimu yetu kama alivyofanyia KWELI shirika la reli.
Mkuu uliona mbali, hili jambo bado lina sintofahamu nyingi naipongeza Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii kwa kuingilia kati watanzania tuambiwe lengo hasa la kushusha hivyo viwango ni nini?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.