Hayapo ya kuongea kuhusu CCM ambayo ni yenu? Mnaipenda CHADEMA ama ndio kejeli? Sitofautishi na umbea wa kawaida tu, "Hujatumwa na si mshirika wao" badala ufurahie kushindwa kwao unajifanya unawashauri vizuri eti waje wakushinde, hizi zilikuwa ni zama za zamani saana! Unadhani Mnyika kama...
Mfano wako hausadifu hali halisi ya siasa, unaonekana bado u mjinga wa siasa za vyama vingi ndio maana unadhani wanaumia kwaajili ya posho bila kuyafikiria maslahi mapana ya wananchi ambao wanaimani na wawakilishi wao. Sababu ya wao kutoka ni nani? Hata hilo hujalifahamu! Tafiti kwanza ili...
Kwahiyo wenye ufahamu mkubwa wafikirie kuhusu makusudi yako wakati mwenyewe umeshindwa, utakuwa katika kundi la wasio na ufahamu? Ulipaswa kuandika ulichokikusudia tu, maneno mengi ya nini?
Ninasubiri huko kunyang'anywa kwa EL! Labda kama tungeanza na zilizozuiwa kujadiliwa bungeni walizojigawia, ama sivyo ni uzushi tu. Nadhani nimekosa kipaji cha kunyamaza ningekuwa nacho ningenyamaza tu waseme yote kama alivyonyamaza Mheshimiwa EL, ni jibu zuri na linakidhi kwa kiwango chake.
Unadhani kupigwa tu ndio suluhu ya madai yao? Uhuru gani kama democracy inaminywa? Miongoni mwa elements za democracy ni free and fair election, transparent na nyinginezo nyingi. Je Z'bar kuna free and fair election? Wa Z'bar wasiposikilizwa nani atasikilizwa kwa maslahi na ustawi wa Z'bar?
Tunapohitaji kujadili mambo ya msingi kama ya kujielimisha kuhusu uongozi na tawala katika serikali halafu mwingine anaingiza vitu vya kitoto kama hivi, ni ujinga usioweza kuvumilika! Atamuoa lini? Kwa sheria ipi? Acha ujinga Duppy!!
Unamaana kuwa yeyote anayewatetea wezi naye mwizi? Mbona Magufuli aliwapa siku saba wanaodaiwa/waliokuwa wanakwepa kulipa kodi, naye ni mkwepaji kodi? On the spot mwizi unayemtafuta ukimwona unamkamata na kumpeleka akajibu mashtaka yake!!
Duh!! Hapa nikama una agenda tofauti na mjadala uliotakiwa. Nadhani bunge linaweza kukaa siku za karibuni, wanajua ni nini kinatakiwa sasa. Ningekuwa mimi nimepata fursa ya kushauri ningeshauri liundwe bunge maalumu la katiba ili iletwe rasimu iliyoridhiwa na pande zote!!
Katika usiku wa giza nene mtu/watu hawawezi kuona na kukadiria uzito wa kivuli chako! Samaki ni shujaa, machozi huenda na maji! Kuto kuonekana kivuli haimaanishi kuwa ukiwa nuruni pia huna kivuli!!
Nilisoma mahali fulani kuwa mtu yeyote anathibitika mahakambani kuwa ni mkosaji, unatuthibitishiaje kuwa EL mwizi? Zaidi saana kwa mtazamo wangu ninaona ugunduzi wako umechelewa maana hauna suluhu. Kuhusianisha matokeo ya uchaguzi na tuhuma hizi kunaonesha ni kwa kiasi gani hujatafiti matokeo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.