Jeri utalipwa hapa hapa duniani haya uliyosema kama sio kweli yatakurudia jaribu kuweka akiba ya maneno maana wewe ni mwandishi wa habari na ni kijana bado una safari ndefu mbele mwombe Mungu akusaidie akuongoze ktk maisha yako bila mungu na kutenda yaliyomema huwezi kutoka
Naona wapinzani bungeni wanateswa sana kama kweli spika anataka kukaa nao basi wasipende kuwaonea au kuwatesa hakuna kisichokuwa na mwisho hapa duniani jamani kumbukeni pia maneno ya Mungu wakati mwingine
Analima baada ya kustaafu kazi,unataka mtu amalize kusoma akalime inamaana alisomea kilimo au,jaribu kidogo kujiongeza maana unafikiri hata kilimo kinafanyika bila pesa waulize wanaolima wakwambie
Kuna siku watu wataelewa ukweli kuhusu haya muda utasema,na hakuna chenye mwanzo kisicho na mwisho kila kitu Mungu anaona na tukimwomba kwa bidii tutaona yote kabla ya kuondoka hapa duniani.Mungu yupo na atuongoze atulinde sana tumalize salama
Hii inasikitisha sana hivi vitu Mungu hapendi na kweli Mungu wa mbinguni anaona hii dhambi itazidi kuwagarimu watu jamani badilikeni maana na dunia nayo sasa imebadilika sana.hapa sasa nitaombea nini?
Leo amesema uraisi wake ni sisi tunao na huku majuzi kule dar alisema hakuna aliyemsaidia kupata uraisi alipiga kampeni peke yake.Ukitenda mema bila kupendelea upande wowote kazi yako inakuwa rahisi sana,bashite hakubaliki tenda haki na watu wasitishwe na uruhusu bunge ili wananchi wajue...
Kama kazi imekuwa ngumu kuliko ulivyotegemea si uombe kustaafu?Uraisi sio kazi ya kukimbilia ni kazi ya kumtanguliza Mungu mbele na kuomba hekima kuliko tunavyofikiri.Utazeeka mapema sasa
Ndege huliwa kwa majina na kuna wa kifuani na mgongoni.kama hiki sio kipindi chako hutapata ila kama ni wakati wako utapata hewa sana.mambo ni magumu ila kipindi hiki unaambiwa kuna watu wanapiga dili kwelikweli kama huamini muulize jirani yako
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.