1. Fainali ya UEFA Champions League kati ya Manchester United na Bayern Munich iliyochezwa kwenye Dimba la Camp Nou huko Barcelona, Uhispania, tarehe 26 Mei 1999, Mabao ya dakika za majeruhi kutoka kwa Teddy Sheringham na Ole Gunnar Solskjær yalifutilia mbali bao la mapema la Mario Basler...