Anajivunia kuwa mtanzania Dr.Slaa sio mroho wa madaraka kama ccm na makapi wake,hana haja na uongozi,zaidi alikuwa anasaidia jamii ijitambue lkn makapi ya ccm na pesa zao wamenunua haki za watu
Ni bora chadema ingepoteza ikiwa na dk.Slaa kuliko ikipoteza ikiwa na lowasa,maana vijana na jamii iliyo waamini chadema watagawanyika na kukoswa wapi wakimbilie maana tayali wanaotuhumia ufisadi wanasafishwa na chama chao! Nasema hii ni hatari na tujiandae kisaikolojia kuendelea kuona ufisadi...
Nakuunga mkono 100%. Slaa amepigania chama kitambo na anauwezo zaidi ya lowasa ambae anamakovu kibao,ktk hali ya kawaida chadema wamepunguza mvuto kwa wanainchi na wasahau kushinda zaidi ni machafuko tu!
Ushindi wa chadema na uhai wake uko kwa Slaa na kama mnabisha ajitowe muone ambavyo chadema itapoteza umaharufu na umashuhuli wake! Kitendo cha chadema kumpokea lowasa na kumuona kama Mungu wao na bila masharti hii ni hatari sana na lazima chadema tukubali kupoteza kwa wananchi.
Kama cdm wataamua kumsimamisha EL kupeperusha bendera ya ukawa basi nitaamini wapinzani tutasubili sana kuchukuwa nchi! Lakini pia nadhani itabidi zzk arudishwe kundini maana makosa yake ni mepesi kulinganisha na huyo fisadi mkuu na mnafiki kwa wananchi wa Tz,maana yeye alijua ukweli kuwa...
Mkuu umezungumza kweli tupu na mimi naongeza kuwa kwa mwendo huu hakunachama cha kizalendo wote wapigaji tu! Dr.slaa na lisu wanachakutuambia wanachadema !
Naomba kama haya yasemwayo ni tetesi basi yabaki hivyo lkn dr.slaa ama mwingine yoyote lkn co huyo lowasa tutapoteza tena
Unajua ccm tumewachoka maanayake ni watu wake na sio rangi za nguo zao! Lowasa ni ccm walewale najua anaweza kuwa msafi lkn lisemwalo lipo! Apokelewe kama mbunge tu na sio kugombea urais kitakachofanyika tutakuwa tunapambanisha ccm @ kwa ccm jambo ambalo hatutaki wananchi wa kawaida!
Ninaimani na slaa na wengine wote na sio lowasa hatakama ni msafi lakini wakati huu hatufai kuwa rais, alipaswa kuwa mwazi wakati wa richmond na mauchafu mengine yaliyofanyika wakati wake.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.