Mashine za kuondoa sumu mwilini zapigwa marufuku

chakii

JF-Expert Member
Sep 15, 2013
19,700
22,740
BARAZA la Tiba Asili na Tiba Mbadala limepiga marufuku matumizi ya mashine za Quantum na mashine za kuondoa sumu mwilini, kutokana na waganga wanaotumia mashine hizo kutokuwa na uelewa wa kutafsiri majibu.

Imeelezwa kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha wa kutafsiri majibu na kujua matumizi sahihi ya mashine hizo, jambo linalosababisha kutoa majibu yanayowaongezea hofu wagonjwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa baraza hilo, Profesa Rogassian Muhunnah alisema baraza hilo, halitambui mashine hizo na watoa huduma za tiba asili na mbadala wanaozimiliki wanatenda kosa kisheria.

"Kutokana na mashine hizi kutosajiliwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) hivyo ufanisi na usahihi wa mashine hizo hautambuliki na hauna uhakika," alisema Profesa Muhunnah.

Alisema baraza hilo linawaruhusu waratibu wake, ambao wapo katika kila halmashauri kuhakikisha wanashirikiana na mamlaka husika kuzuia matumizi ya mashine hizo na kuzikamata na kuwachukulia hatua kali watakaokutwa na mashine hizo kwa kuwa wanawadanganya wagonjwa.

Aidha, alisema baraza hilo pia linazuia matumizi ya vifaa vinavyotumika katika tiba ya kisasa kwenye utoaji huduma za tiba za asili na mbadala kama sindano, vifaa vya kupimia damu na vinginevyo.

Profesa Muhunnah alitumia fursa hiyo kuzungumzia matangazo ya waganga wa kienyeji, ambapo aliwataka wananchi kupuuzia matangazo hayo kwa kuwa waganga wengi wanaojitangaza ni matapeli, hivyo wawe macho ili wasiibiwe na waganga hao ambao hutangaza dawa za uongo.

Kwa upande wake, Kaimu Msajili wa Baraza hilo, Mboni Baraka alisema matangazo hayo huwatangaza kuwa ni waganga bingwa wanaotibu magonjwa mengi, jambo ambalo halina ukweli, kutokana na kuwa katika waliosajiliwa hakuna hata mmoja ambaye ni bingwa kwani wengi wao wana elimu ya ngazi ya cheti.

"Sasa unadhani mtu wa aina hii atakuwa ni bingwa wa kutibu magonjwa zaidi ya 100? Hawa wanaojitangaza ni waongo wanataka kuwaibia wagonjwa hawana ukweli wowote," alisema.

Chanzo
:habarileo
 
Nikweli waganga wengi wakienyeji niwezi utakuta ukienda kutibiwa unaagizwa kilo 10 zamchele kreti 2 zabia nazi 5 nambuzi kuna yani huwa wanaagiza vitu vitam tu sijawahi ckia wanaagiza bamia au matembele kuna mganga nilitaka kumchalaza makofi eti aliniagiza nimpelekee sisimizi aliekamatwa ugoni!!!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Hizo mashine ni devil machines(za kichawi) zinatengenezwa kiwanda kimoja na mashine za kamali yaani bahati nasibu.
Jiulize mbona hospitlini hazipo? kama ni halali WHO wangeizinisha zikatumika na mahospitalini.
 
Hizo mashine ni utapeli mtupu. Process ya kutoa sumu mwilini sio rahisi hivyo kama unavuta kwa pump. Wanacheza na chemistry tu hapo maji yanageuka rangi.

Umesahau stori za bio disc. Wanaanza kuuza mkistuka inakuja style mpya. Eat health, kunywa maji ya kutosha, fanya mazoezi

. Hakuna muujiza
Walikuwa wapi siku zote. Wanaona wivu hao.
 
Bora. Maana wengi wetu tunaamini mambo kwa urahisi mno - ilikuwa kutapeliwa mtindo moja!
 
Lakini hii nchi tuna tatizo gani, mbona kila wakati tunachukua hatua wakati watu wameshdhurika?

Hilo tatizo hawakuliona wakati hizo mashine zinaanza kutumika?!
 
Kiukweli hilu swala limekuwa kikinitataza sana, watu wanaibiwa mno, hivi inakuwaje unashika kimashine, eti kinapima mfumo wote wa mwili na majibu unapewa muda huo huo, alafu wajanja sana, ukiwa mwanaume lazima wakuambie kuwa nguvu za kiume zimekwisha!! Baada ya hapo sikilizia bei ya dawa, dozi ya chini ni laki 3. Hawa tfda wanabaki kukimbizana na maziwa yaliyoandikwa kwa lugha ya kiingereza tu, eti wa tz hawajui kiingereza.
 
Hizo mashine ni devil machines(za kichawi) zinatengenezwa kiwanda kimoja na mashine za kamali yaani bahati nasibu.
Jiulize mbona hospitlini hazipo? kama ni halali WHO wangeizinisha zikatumika na mahospitalini.

Fanya research wacha uvivu au darasa la 7?
 
Hizo mashine ni devil machines(za kichawi) zinatengenezwa kiwanda kimoja na mashine za kamali yaani bahati nasibu.
Jiulize mbona hospitlini hazipo? kama ni halali WHO wangeizinisha zikatumika na mahospitalini.
Khaa!! Mbona kuna kiwanda kimoja china wanatengeneza bidhaa za mpira na plastic. Moja ya bidhaa zao ni pamoja na kondom na book covers ambazo ndiyo hutumika kwenye misahafu ya dini zetu?? Tumia akili bora waje watuambie madhara yake in details siyo kukumbilia usajili na mambo yanayohusu kodi
 
Back
Top Bottom