Kwanini wanawake wanakuwa desperate na ndoa?

supercharger GT

JF-Expert Member
Sep 25, 2016
1,007
1,944
Kuna kipindi nilikuwa na girlfriend wangu, akanicheat na jamaa flani. Tukagombana ila nikagundua sababu ni alikuwa ana hamu sana ya kuolewa na mimi nilikuwa bado sijasettle na jamaa alimpanga atamuoa, basi nikabariki kumuachia kiroho safi ingawa niliumia! Kweli akaolewa maisha yakaendelea ila hakuacha kunitafuta e.t.c.

Sasa likizo hii nimekuja kusalimia akasikia nipo, kaanza kunisumbua anasema anataka nimpatie japo mara moja maana tangu aolewe hana raha yoyote zaidi ya ile heshima tu kuwa kaolewa, ila nikicheki mshkaji alivyo sioni kama anayosema huyu mwanamke ni kweli.

Sasa anasumbua hadi imekuwa kero na ubaya mji huu mdogo sana na anajuana na friends wangu wa zamani so hata nikimkwepa bado kuna mtu atamuambia tu nipo mahali gani nakunywa bia e.t.c nashangaa mtu katimba.

Wanawake huwa wanasukumwa na nini kuolewa haraka halafu wanajuta?
 
Kumbuka ile laana ya Mungu pale eden bado inawatafuna na haitawaachia mpk masihi atakaporudi mara ya pili... Walilaaniwa kuwa tamaa zenu (wanawake) zitakuwa juu ya mwanaume siku zote, nae atakutawala.... Mpaka leo mwanaume ndie kiongozi ndani ya ndoa. Watadai uhuru na hawajui wakumdai uhuru bcoz aliewalaani sio mwanaume bali ni muumbaji wao. Haki sawa watapewa na huyo huyo.
 
Kwasababu jamii ndiyo imeshatujenga hivyo, mwanamke ukifikisha miaka 30+ hujaolewa, wazazi wanakuwa na wasiwasi, marafiki wote uliosoma nao wameolewa na wana watoto unajiona tofauti sana. Wakati Oprah ameolewa mwaka huu akiwa na 60+.
Nadhani zilikuwa ni habari za uzushi tu hakuolewa.
Yule yuko kwenye u boyfriend na girlfriend mwaka wa 30 huu.
 
Nadhani zilikuwa ni habari za uzushi tu hakuolewa.
Yule yuko kwenye u boyfriend na girlfriend mwaka wa 30 huu.
Nilisomaga Ebony zamani sana in 90's ni kuwa walishapanga harusi kitabu cha Oprah kikatoka ndani yake alimzungumzia Graham, Graham alikasirika sana wakaamua kuairisha harusi, Oprah alikuwa very disappointed akamwambia kama unaahirisha leo hatutaona tena.
 
Back
Top Bottom