kuna ujumbe unasambazwa kwenye makundi ya whatsapp ukidai kuwa kuna namba ikikupigia ama kutuma ujumbe na ukijibu unapoteza maisha kwani mtumiji wa namba hiyo anatafuta damu za watu ni kweli?
Nimeona taarifa ikionesha kuwa unywaji wa maziwa mabichi husababisha ugojwa wa brucellosis na mimi kwa upande wangu nimekuwa nikinywa maziwa mabichi kwa muda kidogo japo sijawahi kuona changamoto yoyote.
Jambo hili lina madhara?
Naomba msaada kujua uhalisia wa swala hili upoje juu ya makubaliano yaliyosainiwa kati ya serikali ya Kenya na Ujerumani kubadilishana wafanyakazi 250,000 kutoka Kenya.
Baadhi ya jamii huamini kuwa ulaji wa limao na ndimu husababisha upungufu wa damu mwilini.
Uvumi huu uliosambaa kwenye maeneo mengi hutoa maonyo makali hasa kwa watoto na wanawake wenye ujauzito wanaojaribu kutumia matunda haya.
Je, ni kweli kuwa matunda haya hukausha damu mwilini?
Kuna magonjwa mengi yanayosababisha upungufu wa Kinga mwilini ikiwemo maambukizi ya VVU.
Kumekuwa na mijadala mingi pamoja na tetesi zinazohitaji majibu ya kina kuhusu uwezekano wa kupata VVU/UKIMWI kutoka kwa mtu aliye athirika hasa ikihusisha ushiriki wa tendo la ndoa pasipo kutumia kinga hata kama ni mara moja tu.
Ukweli upoje na majibu ya kisayansi yanatoa picha gani? Baadhi hudai hauwezi kupata VVU/UKIMWI kwa kufanya tendo moja tu la ngono na muathirika pasipo kutumia kinga kwa kuwa maambukizi hayaji kirahisi hivyo kama tunavyodhani.
Nimeona poster ya The Chanzo yenye picha ya Freeman Mbowe ikiwa na maelezo ya kwamba Mwenyekiti huyo wa CHADEMA amemshukuru Rais Samia kwa kuungana na CHADEMA Kuomboleza msiba wa mzee Kibao, je taarifa hii ni ya kweli na chanzo chake ni The Chanzo.
Nimeona video ikisambaa toka jana ikimuonesha Tundu Lissu akiwa anazomewa na watu waliokuwepo kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jana tarehe 11/09/2024 wakimzomea na kumuita YUDA je ni cha kweli?
Habari wapendwa, kuna taarifa inatembea mitandaoni kuwa Dkt. Slaa amepata taarifa ya Deusdedit Soka ya kwamba atauawa leo na kutupwa msituni, je, Taarifa hiyo ni kweli imetoka kwa slaa? Na ina ukweli?
Salaam Wadau wa Michezo,
Kuna taarifa nimeiona inadai kuwa Willy Esomba Onana aliyekuwa mchezaji wa Simba SC msimu uliopita ameibuka shujaa kwa kufunga mabao matatu katika mchezo wake wa kwanza wa kirafiki. Taarifa hiyo nimeiona kwenye akaunti ya Instagram ya Aggy Simba na kwa SeekerTZ.
Habari wakuu, nimeshangaa sana kuona WASAFI TV ikitumia lugha ya kihuni tena yenye maudhi katika uwasilishaji wa taarifa.
Chombo mahili hakiwezi kutumia neno 'usela mavi' katika kufikisha ujumbe wake kwa hadhira,binafsi siyo mtaalamu wa teknolojia labda nyie wajuvi wa mambo hayo tazameni hii video chini kisha mniambie kama ni editing au laa.
Kama ni Wasafi kweli lazima tujiulize maswali yafuatayo:
Je hii jeuri wanaipata wapi ya kutudhihaki sisi juu ya msiba mkubwa kama huo?
Je wao wanatumika katika kuchochea maovu ya utekaji au wao wanajikuta akina nani labda na chombo chao?
Je wamezingatia nini katika uwasilishaji wao wa hiyo habari na je wameelewa kweli nini maana ya kupinga na kupaza sauti kwa vitendo juu ya mauaji?
Pia soma...
Salaam ndugu zangu,
Nimekutana na picha ya JamiiForums ikienea ikionesha ujumbe wa Prof. Mkenda unaodai kuwa kwa sasa vigezo vya kupata kazi kwa Wanafuzni ni kuwa na GPA 3.8. Jambo hili limenistua.
Je kuna ukweli hapa? Picha yenyewe hii hapa chini:
Fatuma Karume asema CHADEMA wanahusika na mauaji yanayoendelea, hatuwezi kulilaumu Jeshi la Polisi kila siku wakati viongozi wa CHADEMA wenyewe wakishutumiw na wapo kimya!
Kumekuwa na post ya Jenerali Ulimwengu aliyoichapisha kwenye mtandao wa X kwamba Mwalimu Julius Nyerere alikuwa Mwenyekiti wa chama chake kuanzia mwaka 1954 mpaka 1977, ukweli wa kauli hii upoje?
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu, amesema Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe amemzuia kwenda katika ofisi kutokana na yeye kueleza ubadhirifu unaofanywa ndani ya chama.
Pia Lissu amesema sababu nyingine ya kuzuiwa kwenda katika ofisi hizo ni kutokana na kutoa siri za vikao ndani ya chama, na kumueleza ukweli kuhusu kitendo cha kuanzisha taasisi nyingine ndani ya CHADEMA.
Aidha Mwanahalisi ina nakala rasmi ya barua ya siri ambayo Mbowe amemwandikia Lissu kwa kumpiga zuio la kwenda ofisini.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.