JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Nyota wa zamani wa Real Madrid, Roberto Carlos anadaiwa kuingia kwenye mgogoro na mkewe hali iliyopelea atumia majengo ya uwanja wa mazoezi wa Real Madrid kama makazi wakati akishughulikia suala lake la talaka na mkewe waliodumu kwa miaka 15 Wenzi hao, waliofunga ndoa mwaka 2009, sasa wanakabiliwa na vita vya kisheria kuhusu utajiri mkubwa wa Carlos, unaoripotiwa kuwa na thamani ya pauni milioni 133 (Tsh410,091,550,000)
Binamu wa rais wa zamani wa Syria, Bashar al-Assad aliukiwa kwa kunyongwa na baada ya kupandishwa juu na crane. "Baada yakuwasili kwa vikosi vya waasi wa Syria katika mji wa Latakia, ilitangazwa kuwa Suleiman al-Assad, ambaye alikuwa kiongozi wa Vikosi vya Ulinzi wa Kitaifa, aliuawa. Kwa mujibu wa gazeti hilo, Suleiman al-Assad alinyongwa kwa kutumia kreni katika uwanja mmoja huko Latakia. Sababu ya kuuawa kwake ilikuwa uhusiano wake wa damu na rais wa zamani, pamoja na "uhalifu dhidi ya wale waliopinga utawala huo."
Inadaiwa huyu jamaa bhana enzi za utumwa, alitumika na masta wake kama mbegu ya kuzalisha watumwa wenye nguvu. Inadaiwa kutokana na kuwa na nguvu, umbo maridadi na urefu wa futi 7 hivyo masta wake alimpa upendeleo wa kipekee wa kumpunguzia majukumu mengi huku kazi yake kubwa ilikiwa ni kulala na kuwapa mimba wanawake mbalimbali ili waweze kumzalia masta wao watoto wenye nguvu ambao wangetumika katika shughuli za kitumwa. Roque Jose Florêncio aliacha idadi kubwa sana ya watoto.
Je, ni kweli kuna Samaki mtu? Maana huku mtaani kuna watu huwa wanatuhadithia namna walikutana na Samaki watu au kuhadithiwa na wengine stori kama waliona mwanamke Mrembo mweupe kama Mwarabu ila amekaa juu ya jiwe au ufukweni au anaogelea kwenye bahara au ziwa. Mwanamke huyo wanaeleza anakuwa na nywele ndefu na chini umbile la samaki wa kawaida ila kuanzia kiunoni ndio binadamu, na wasimuliaji husimulia kuwa ukitaka kumkamata unaona analia na anaomba usimkamate wengine wakidai wana watoto wadogo wananyonyesha, au wana familia hivyo kuomba waachwe huru waondoke. Stori ni nyingi sana huku wakidai samaki watu hao hukamatwa na kuliwa kama samaki wengine huku viwiliwili vyao vikizikwa au kutupwa tena majini. Je, ukweli ni upi JamiiCheck...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…