Zungu atoa ufafanuzi kuhusu kodi ya mtandao

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,007
9,873
1618991962609.png



Mbunge wa Ilala, Azzan Zungu, alipendekeza kuwepo kwa kodi ya Uzalendo itakayokatwa kila siku kupitia Mitandao ya Simu kwa kila Mtanzania ili kuwa chanzo kipya cha mapato kwa Serikali.

Zungu amejibu kwa ku-comment kwenye ukurasa wa Instagram wa JamiiForums akieleza kuwa Tsh. Bilioni 540 alizotaja sio kwa siku bali zitakusanywa kwa mwaka.

Pia amewataka wananchi kufikiria mahitaji ya elimu, huduma za afya na barabara ambazo zinapaswa kugharamiwa.

Zungu amesema mitandao ya simu imefanya watu waishie kupigiana simu na kuokoa kiasi cha nauli ambacho wangetumia kuwatembelea ndugu zao. Hivyo sio mbaya kulipa kodi.

ZAIDI SOMA
-
Azzan Zungu ataka uwepo wa kodi ya uzalendo itakayokatwa kwenye Mitandao ya simu kwa kila Mtanzania
 
Kwanza anaongelea vipi suala la viongozi wachache wa serikali kutafuna mabilioni ya wananchi bila kuchukuliwa hatua kabla hatujaenda kwenye kuzidi kuwabana wananchi kwa mikodi kuna mkakati gani wa kulinda hizo kodi.

Tukianza na ripoti ya mkaguzi watuhumiwa wamechukuliwa hatua gani. Tunaposema Tanzania ni tajiri inawezekana hata kwa mapato hayahaya Tanzania ingekuwa mbali sana lakini wanufaika wachache na wasio na uchungu.

Na wanachofanya ni kutumia tu gharama yoyote kuhakikisha wanabaki kwenye nafasi zao ili waendelee kula lakini sio kuboresha hii ni akili mbovu sana.
 
Huyo mzee asitake kutufungulisha saumu zetu akae kwa kutulia kama ana minyoo ameze dawa,

Ningemuona wa maana kama angewaambia wachumia tumbo wenzake hapo mjengoni waache kupokea posho na mishahara ikatwe huo ndio uzalendo sasa.
 
Hana akili uyo zungu.

Hivi akili yake ktk kutanua wigo wa Kodi ndo imeishia hapo?

Kama anaujua uzalendo kwanini asipendekeze wabunge zaidi ya 300 wapunguziwe posho ya kikao laki laki kuchangia huo uzalendo.

Anaweza akatupa mchanganuo wa matumizi ya laki 3 na 80 kwa kujikimu tu kwa sikU pale bungeni?
 
Kwahiyo ndo atuandikie kama alitoroka chekechea? Inawezekanaje mtu kama huyu alishawahi kuwa Waziri ilihali hawezi kuandika kwa vituo?
 
Hivi MAKONDA wakati anakamata aliowaita "Wazungu wa Unga" huyu alimwachaje wakati anajiita Zungu?
 
Ana hoja nzuri, ila tungeanza kukata kodi kwanza kwenye posho ZOTE za wabunge zisizo za mshahara. Hapo tutaenda sawa.
 
Yaani hata kuandika neno Gharama hawezi....huyu mbunge inaonekana hayuko sawa.

Angeanza na hao wabunge wasio na chama na bado wanapokea mshahara na marupurupu kinyume na utaratibu na hizi ni kodi za watu masikini na wafanyakazi.
 
Hizi ni dalili za kujichokea kuwa mbunge maana anajua 2025 hawezi tena kugombea baada kupita kimagumashi 2020 kwa kuhonga wajumbe mlungula
 
Kwanza anaongelea vipi suala la viongozi wachache wa serikali kutafuna mabilioni ya wananchi bila kuchukuliwa hatua kabla hatujaenda kwenye kuzidi kuwabana wananchi kwa mikodi kuna mkakati gani wa kulinda hizo kodi.

Tukianza na ripoti ya mkaguzi watuhumiwa wamechukuliwa hatua gani. Tunaposema Tanzania ni tajiri inawezekana hata kwa mapato hayahaya Tanzania ingekuwa mbali sana lakini wanufaika wachache na wasio na uchungu.

Na wanachofanya ni kutumia tu gharama yoyote kuhakikisha wanabaki kwenye nafasi zao ili waendelee kula lakini sio kuboresha hii ni akili mbovu sana.
Ahsante mkuu umeniwahi kwanza warudishe mabilioni ya kwenye Ripoti za CAG ili tuamini km wazalendo sio kuendelea kutukamua halafu pesa mnahamishia China na Uswiz..
 
Back
Top Bottom