Zomea zomea yamwangukia Mwakyembe

Zomea zomea yamwangukia Mwakyembe

Kijallo

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2011
Posts
409
Reaction score
61
Wakuu siku ya jana, mh Mwakyembe, amezuiliwa na wakazi wa Kyela kuingia stendi ya Kyela na kuzomewa na wakazi wa hapa wakidai aliwaahidi lami na hajatekeleza, toka juzi hakuna gari linaloingia stendi, natamani sana kuwatumia picha lakini nipo via mobile
 
acha maneno ya uzushi, tuma picha
 
Hakyanan huyu shetwain sasa, Hata Mwakyembe!!!!??
 
Kutokana na organization mbovu ya CCM kupata nafasi ya uongozi inayohitaji kupigiwa kura ni lazima ulaghai na mbinu tofauti tofauti zitumike(bila kujali madhara ya baadae) na ndiyo tunayoona sasa....

Mwakyembe aliahidi lami ila hiyo hela haipo mfukoni kwake, wana Kyela walistahili kujua hiyo ilikua danganya toto kumvusha! ...lakini wawe na subira, mchakato unaendelea
 
acha maneno ya uzushi, tuma picha
Natumia simu mkuu wangu,

Natamani nikuonyeshe magogo yaliyowekwa, wananchi wanasema walilala, sasa wameamka, kama una ndugu hapa Kyela mpigie hata simu akwambie
 
Wangemchapa na bakora kabisa maana kapoteza pesa zetu nyingi kuzunguka Marekani akidai anaichunguza Richmond matokeo yake kaishia kumfichia Bwana Mkubwa madudu yake na akakubali kurubuniwa Pipi ya Unaibu Waziri na kutulia tuli kama keshafika Kileleni.

MWAKYEMBE nae KWISHNEAA...
 
Kama bosi wake alizomewa na Pinda tena kwake anategemea nini? Tuna muiga Waziri Mkuu
 
Mwakyembe ni FISADI kuliko hao anaowataja, sema yeye ni mwanasheria, hatumii jina lake, lakini fisadi mkubwa asitudanganye chochote
 
Wakuu siku ya jana, mh Mwakyembe, amezuiliwa na wakazi wa Kyela kuingia stendi ya Kyela na kuzomewa na wakazi wa hapa wakidai aliwaahidi lami na hajatekeleza, toka juzi hakuna gari linaloingia stendi, natamani sana kuwatumia picha lakini nipo via mobile

Kama Mwakyembe naye anazomewa sasa nani atabaki. Mbona maahadi yaliyomwagwa ni mengi mno, basi watazomewa wengi kwa kuwa sioni hizo ahadi zitatekelezwa japo nusu yake.

Kama kweli Mwakyembe amezomewa basi tatizo la CCM si ufisadi wa kuiba pesa za nchi tu bali na uongo pia. Ahadi za uongo ndizo zitakazoimaliza CCM 2015 si kingine.
 
Asante CDM kuamsha watanzania; this time kila anayetaka kuwa kiongozi lazima apime kama anaubavu wa kutatua matatizo ya wana nchi. Hivi jamani naomba kuuliza ukihamasisha watu kuwa kataa wabunge wote waliochakachua kwa mtindo kama ule wa Muleba ni uhaini? Naona hii strategy itasaidia kupunguza hizi siasa sanii za chama cha magamba. Maana tume ya uchaguzi wameichakachua, katiba sijui kama watatupa mpya so kama hawataki sheria ichukue mkondo kwa upande wao na sisi tukiamua kuipindisha kwa namna hii si itakuwa ngoma droo? Mpaka kila mtu akubali kuongozwa na sheria. Nifahamisheni fasta ili nianze mpango mzima wa uharakati wa kuongoza operation 'popoa mawe na kisha zomea' wabunge wote ambao hawawakilishi mawazo ya wana nchi!
 
Mbaya zaidi Cdm wanafanya mkutano wao kesho katika uwanja wa siasa,
 
Wasiomfahamu Mwakyembe na usanii wake wanaweza kushangaa. Huyu ni mtu wa ahadi kama JK, sasa na huu uwazri waliompa ndiyo utakaomzika. 2015 tunakomboa jimbo toka mikononi mwa wasanii
 
mwakyembe ni Fisadi kuliko wengine, na ni muongo sana lakini si Mwanasheria? ndio mabingwa wa kusema uongo na kukufanya uamini kuwa ni kweli, halafu jeuri mno, hatuwataki wanasheria na maprofesa, ndio waangamizaji kimya kimya
 
Kama Mwakyembe naye anazomewa sasa nani atabaki. Mbona maahadi yaliyomwagwa ni mengi mno, basi watazomewa wengi kwa kuwa sioni hizo ahadi zitatekelezwa japo nusu yake.

Kama kweli Mwakyembe amezomewa basi tatizo la CCM si ufisadi wa kuiba pesa za nchi tu bali na uongo pia. Ahadi za uongo ndizo zitakazoimaliza CCM 2015 si kingine.
Kwa hali ilivyo sasa hivi ndani ya CCM na ufahamu wa watu yakua wa CCM ni nani na nini?Hali hii itawakumba viongozi wengi wa CCM.CCM imevua ngozi ya kondoo sasa mambo yako wazi,na huu usanii wa kujivua magamba badala ya kuleta tija kwa CCM ndiyo unaitosa zaidi kwani watu wanashindwa kuelewa magamba ni yapi na kwa vile idadi kubwa ya viongozi wa CCM ni magamba kwa mtizamo halisi.Wananchi wanasubiri magamba ni yapi kwa mtazamo wa CCM,wakati CCM inaendelea kukaa kimya wananchi wana haki ya kumshuku kila kiongozi wa serikali ya CCM kwa sababu hawajui magamba ni yapi.Pili hata hao viongozi makini waliomo katika CCM ni vigumu kuwaamini kwa kukaakwao kimya miongoni mwa magamba na kujaribu kuturubuni kua wanachapa kazi.Jitihada zao nazifananisha na mtu anaejaribu kusukuma gari liende mbele akiwa amekaa ndani ya gari hilo wakati dereva wa gari hilo JK,amevuta breki ya mkono na kukanyaga breki ya mguu na utingo CCM kaweka kigingi.MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Ni kweli kabisa kuwa Dr Mwakyembe anakupambana na zomea zomea kila akikatisha baadhi ya mitaa Kyela mjini;na hali ilikuwa tete zaidi juzi stand ya mabasi wakati wakazi wa Kyela walipofunga stand hiyo kwa sababu ya kukithiri kwa uchafu na kuwepo kwa madimbwi yanayotiririsha maji machafu kwenye maeneo yao ya biashara!

Juzi ilikuwa ni mkutano kati ya wananchi,DC,DED na Mbunge lkn wote hao viongozi hawakutokea na kuzidisha hasira za wananchi;walihaidi kuwa sasa mkutano huo utafanyika jana(sina taarifa kama nao ulifanyika au la)!

Wananchi sasa bila kuogopa wanamuhoji Mwakyembe ahadi za serikali hasa kuhusu barabara ya Kyela-Matema beach ambapo Rais JK mwaka 2005 aliwahaidi wana Kyela na kuirudia tena ahadi hiyo mwaka 2010 bila matekelezo yeyote yale;pia wanamkumbusha kuhusu ahadi ya meli mpya waliyowahaidi wana Kyela lkn majibu yake ni negative!

CHADEMA ikiongeza juhudi kidogo tu hasa za kuanza kumtafuta potential candidate wao Kyela basi pasipo shaka yeyote ile wanachukua jimbo hili kiurahisi kabisa;uzuri zaidi ni kuwa Dr Mwakyembe kaisha tangaza kuwa HATAGOMBEA mwaka 2015 hivyo kulifanya jimbo la Kyela"kutokuwa na mwenyewe"!
 
Yeye mwenyewe alizichota mwaka 2004 ili atengeneze umeme wa Upepo Singida, badala yake pesa katumia kwa kampeni apate ubunge na kujijenga, alikuwa lawyer mbuzi tu
 
Back
Top Bottom