Zitto: Rais ni mbaguzi, simple and clear

Zitto: Rais ni mbaguzi, simple and clear

Wenye upungufu wa uwezo wa kufikiri kutafakari na kuona hawawezi kuelewa maana ya sentensi hizo. Kifupi mkuu wa kaya ana ubaguzi tena bila hata haya. Angalia baraza lake la mawaziri, angalia wakuu wa mikoa angalia wakuu wa wilaya, angalia wakuu wateule wa taasisi mbalimbali za serikali.n.k, utaona jinsi ubaguzi unavyotamalaki. Angalia anavyoshughulikia maafisadi, umewahi kusikia kuna fisadi wa kutoka kanda ile ameshughulikiwa?. Unaona anavyojifanya haoni wala hasikii ufisadi wa Rada Epa Escrow na muhusika mkuu aliyeiingiza serikali mkenge na hadi leo anaendelea kulipwa wala haguswi tena nna cheo kapandishwa. Ukistaajabu ya Musa utaona ya filauni Angalia yule wa sakata la Lugumi kafanywa nini? Kweli hii kanda yetu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! wezi wanatoka kanda zile siyo huku kwetu!?!?!?!?

Kwa hiyo Mramba aliyesema tule nyasi rada inunuliwe ni wa kanda ile? Ama EPA na ESCROW wa kanda ile ni akina nani?
Nyie kwa kuhamamisha magoli hamjambo. JK wa Msonga sasa hivi remote yake imekatika nini ku remote ikulu? Ama System ile ile Magufuli haiwezi mmehamisha magoli kwa ubaguzi. Kweli wana UKAWA ni hatari, ukijiunga ukawa lazima ujue vizuri namna ya kuhamisha magoli.
 
Abubakary alikuwa wa CCM? Japo inatekelezwa ilani ya CCM ndio post zote ziwe za wanaCCM? ina maana hata wanajeshi na mapolisi ni maCCM simply tu kwa kuwa inatekelezwa ilani ya CCM? Kuna kitu hakiko sawa hapa
wanajeshi hawaruhusiwi kuwa na kadi za vyama na wangelazimika basi wote wangekuwa CCM.
Kwi kwi kwi
 
Je na sisi wengine tunaohudumu kwwnye taasisi za umma, inabidi tuondolewe kwa sababu hstuijui ilani ya ccm wala sio makada!
 
Kama Bw Jenerali Ulimwengu alivyobainisha hivi karibuni, jamii ya kiTanzania inarudishwa nyuma miaka hamsini, yaani kana kwamba ndio tumeibuka kutoka enzi za ukoloni! Kwa mtawala kama mtukufu JPM anayejinadi kuwa mzingatifu wa 'hapa kazi tu' angeonesha hiyo dhana kwa vitendo kwa kutoifunganisha kazi ya u-DED na ukada (ukereketwa) wa chama cha siasa.

DED anapaswa kuwa mtaalamu angaa amesomea mambo yanayohusiana na public administration & management na ana uzoefu wa kutosha. Huyu ni meneja.

Iwe ni kazi inayotangazwa na halmashauri husika. Waombaji watume maombi ya kazi, maombi yachekechwe na kamati ya ajira, wanaoonekana kutimiza vigezo wasailiwe, na hatimaye mshindi aajiriwe na Halmashauri kwa mikataba ya kikazi (sio ya kisiasa).

Pindi mhusika atakapokiuka mkataba wa kazi, halmashauri iwe na haki ya kumwajibisha. Hapa hakuna cha u-CCM wala u-ACT-Wazalendo, wala u-CHADEMA. Wa-DED wanapaswa kutofungamana na ukada wa kisiasa.

Wawe neutral na kuwatendea haki wanajamii wote katika himaya zao. Hapa ndio tungeweza kuamini kuwa Mtukufu Rais anamaanisha anachokisema. Vinginevyo 'Hapa ni siasa tu!' tena mbele kwa mbele.
 
"Dkt. Bana anaelezaje suala la Abubakar Assenga ambaye aligombea Ubunge jimbo la Kilombero na kushindwa na sasa ni DAS. Mfano wake ndio mfano Hidaya aliyegombea Malinyi. Rais ni mbaguzi wa vyama, simple and clear."

Zitto Kabwe
Hizi nafasi ni za kuchaguliwa kwa hiyo anayechagua ana haki ya kumchagua anayemtaka sasa kosa lipo wapi? Tubadilishe katiba nafasi zote za kazi wanaopenda waombe na wafanyiwe usaili kama Kenya japo wanafanya kiduchu. Vinginevyo Zitto serikali ya umoja wa kitaifa ipo Zanzibar sio bara.Hata hivyo suala la ubaguzi mbona hata wewe Zitto ni mbaguzi umesahau kule bungeni ulipowaambia wabunge wa upinzani ambao ni wa dini yako kwamba wasitoke nje kwa kuwa.......huo sio ubaguzi na udini ndani yake
 
Ukimsikiliza na kumtazama Mkuu wa Kaya wakati anaongea unaweza hata kumuhurumia kuwa anakwazika mno na kuumia sana na mambo anayoyakemea lakini anachokitekeleza ni tofauti kabisa na message anayoitoa kwa umma kwenye hotuba zake.
Mkuu tayari tusha msoma sana
 
Bahati mbaya amechelewa kujua hayo mambo,awaulize watu wa Buziku na Runazi kule biharamulo wanamjua vizuri jamaa,
Anajua tu sema sasa zzk mambo yamemgeuka kwani inaonekana katoswa
 
"Dkt. Bana anaelezaje suala la Abubakar Assenga ambaye aligombea Ubunge jimbo la Kilombero na kushindwa na sasa ni DAS. Mfano wake ndio mfano Hidaya aliyegombea Malinyi. Rais ni mbaguzi wa vyama, simple and clear."

Zitto Kabwe

Alitaka ateuwe wa UKAWA au ACT kutekeleza ilani ya CCM. !!!! Mbona Vichekesho ....
 
Abubakary alikuwa wa CCM? Japo inatekelezwa ilani ya CCM ndio post zote ziwe za wanaCCM? ina maana hata wanajeshi na mapolisi ni maCCM simply tu kwa kuwa inatekelezwa ilani ya CCM? Kuna kitu hakiko sawa hapa

Wewe unafikiri unashiriki uchaguzi ushike dola ili uwape madaraka vyama vingine? Kitu ambacho hakipo sawa hapa ni tafakuri ya anayeona kuna kitu hakipo sawa. Katika lugha ya isiyoya kidiplomasia lakini ndio ukweli ni kwamba wanajeshi na mapolisi ni watumwa na si viongozi, kazi yao ni kutumwa tu na sio kufanya maamuzi
 
Wakurugenzi ndo wanaokuwa wasimamizi wakuu wa uchaguzi majimboni. Kwa maana hiyo, kama kweli Rais anawinda wana CCM kwa nafasi hizo, uchaguzi ujao wasimamizi wa majimbo watakuwa wana CCM.
 
Back
Top Bottom