Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Zitto: Nina sharti moja tu kurudi CHADEMA

Inanikumbusha stori ya jamaa mmoja ambaye mke wake huwa anafanya analotaka na mumewe mpole, mwisho akaenda mahakamani kuomba talaka, mumewe akasema vema. Alipoona washikaji nao wamemtosa akataka kurudi kwa mumewe naye kasema imetosha kaa hulo huko.
Pole Zito, nadhani there is no way back, you had played your cards very wrongly

Think as if there is no box mkuu,kurudi kwa zitto CDM ni kwa manufaa ya mageuzi ya kisiasa nchini.
 
Naomba kuweka wazi...

Hakuna aliye juu ya chama.Kuna watu wanatafuta kutaka kuwa maarufu kuliko chama.

Zitto akitaka kurudi Chadema anapaswa kuomba radhi ajutie makosa yake na huu ndiyo msimamo rasmi.

Katiba ya chama iko wazi.Kukipeleka chama mahakamani ni kujifukuzisha mwenyewe ndani ya chama.

Hizo sheria ziko FIFA tu.
 
Think as if there is no box mkuu,kurudi kwa zitto CDM ni kwa manufaa ya mageuzi ya kisiasa nchini.

Manufaa ya mageuzi! Ninamashaka ukiangalia kwa upenyo upi. Kulikuwa na fursa kubwa, na nzuri iliyomfanya awe na upeo mkubwa zaidi, lakini alitumia nafasi hiyo na ukuaji wa umaarufu wake kwa njia ambayo haikuwapendeza wengi. Hivi sasa anataka a regain position aliyokuwa nayo zamani, nayo siyo rahisi, hivi sasa nafasi ya uenyekiti wa PAC ndio anayoitumia vizuri, lakini kwa kukiuka matarajio ya walewaliompa nafasi hiyo, lakini haimtii hofu kwa vile 2015 kutakuwa na mabadiliko (siyo lazima ya kichama) ya uongozi
 
Wakati napata akili timamu mitaa ya Kitambwe maeneo ya Mwanga Kaskazini pale mjini kigoma ndipo niliposikia Jina la shujaa Zitto Zuberi Kabwe toka mkoa wa kigoma.

Huyu mtu ndiye shujaa wangu mpaka sasa, Baada ya kuwa na migogoro na chama chake cha chadema, wananchi wa kigoma walikasirishwa sana na kuanza kukichukia chama cha chadema. Hii ilipelekea kuvunjika kwa ngome kubwa ya chadema iliyojulikana kama Urusi.

Wanachama wakagawanyika katika pande kuu mbili, watu waliozoea kuishi kama ndugu wakawa maadui, hii ilileta uhasama ambao mpaka sasa imekuwa vigumu kushiriki katika shughuri za kijamii kwa pamoja. Katika utafiti mdogo nilioufanya inasemekana kuwa Zitto ni mmoja wa waanzilishi wa chama kipya cha ACT, chama ambacho kimekuwa na wafuasi wengi mkoani kigoma na kati ya watu 10 niliokutana nao 9 wanaadimit kwamba wako ACT sababu ya Zitto Kabwe, Chuki kubwa imekuwa kati ya ACT na wanachama wachache waliobaki wakikitetea
CHADEMA kiasi cha watu kuvamiana na kupigana mapanga.

Sina tatizo na Mwami kurudi katika chama kilichomfikisha pale lakini kuna vitu najiuliza kila ninapomfikiria huyu shujaa wa mkoa wangu.

1. Chuki iliyopo mkoani kigoma itaisha lini?

2. Wanachama waliojiunga ACT sababu ya Mwami wataziweka wapi sura zao?

3. Je itakuwa rahisi kwa wanachama wa
CHADEMA kumpokea Zitto?

4. Kada maharufu wa Chadema Mzee Kasisiko na timu yake wataendelea kuitetea ACT na kuwaponda wabaguzi
CHADEMA?

5. Kama kweli Zitto atarudi
CHADEMA, CHADEMA watakuwa wameacha ubaguzi kama alivyodai pale kwenye viwanja vya Mwanga Center community?

6. Watu wa Urusi watarudi pamoja na kunywa kahawa kama kawaida?

7. Je, CHADEMA kitarudi kuwa chama makini kwa watu wa kigoma?

Mtazamo wangu naona kama watu wa kigoma watafikiria mara mbili na si moja kama walivyopokea masikitiko ya Zitto baada ya kudharirishwa na
CHADEMA.

Ushauri wangu kwa Zitto, nawafaham sana watu wa kigoma ni kama Jiko la Jela, Likiwaka halizimiki. Somo dogo tunajifunza toka kwa Dr Amani Warid Kaburu.

Angalizo; Mimi ni mwanachama wa CCM na mzalendo toka mkoa wa Kigoma.
 
Wewe kama kweli ni CCM,inakuuma nini Zito kurudi CHADEMA,wewe utakuwa wa ACT unahaha,by the way lini uliambiwa Zito katoka CHADEMA,my dear this is what the late Njonjo used to say,IN POLITICS THERE IS NO PERMANENT FRIEND NOR PERMANENT ENEMY,politics is a dirty game
 
Wewe kama kweli ni CCM,inakuuma nini Zito kurudi CHADEMA,wewe utakuwa wa ACT unahaha,by the way lini uliambiwa Zito katoka CHADEMA,my dear this is what the late Njonjo used to say,IN POLITICS THERE IS NO PERMANET FRIEND NRO PERMANENT ENEMY,politics is a dirty game

Sawa Ngonani lakini yalikuwa niwazo tu na angalizo kwa Mwami,
 
Ukweli zitto anapendwa na hajawahi kuisema vibaya chadema ila ana washauri wengi wenye malengo hasi.kitu kimoja ajue mpinzni wako kisiasa hasa ccm akikushabikia kuna tatizo.wapo wanaomshawishi atazame chama kikabila, kikanda,kidini,ki-umri,ki-usomi,nk ,kimkoa ,kimaendeleo nk.Sasa hii mitazamo hata akienda act watu hao watamtaka ajenge chama kwa mitizamo hiyo.Huwei kiuhalisia ukawa na chama kwa mfano cha vijana waliosoma sana waislamu,wa kanda ya magharibi,wa kaila flani utakuta chama chako kimebaki na watu wachache sana. Unapaswa kuappreciate diverse nature of the tz society ili ukubalike kwa wote. kWA MFANO KAULI KUWA HAO WACHAGA WANA UMEME HADI MIGOMBANI---------mana yake si wenzetu hao haikuwa sahihi
 
Fmangapii chadema hakikuwa chama imara kigoma...hata katika uwepo wa zito umaarufu wa chama ulikua ukishuka...hata kura alizopata zito 2005 ni nyingi...2010 zimepungua.

Kwa kigoma NCCR ni chama kikubwa kuliko chadema.

Kwa taarifa mkuu
 
Last edited by a moderator:
Ukweli zitto anapendwa na hajawahi kuisema vibaya chadema ila ana washauri wengi wenye malengo hasi.kitu kimoja ajue mpinzni wako kisiasa hasa ccm akikushabikia kuna tatizo.wapo wanaomshawishi atazame chama kikabila, kikanda,kidini,ki-umri,ki-usomi,nk ,kimkoa ,kimaendeleo nk.Sasa hii mitazamo hata akienda act watu hao watamtaka ajenge chama kwa mitizamo hiyo.Huwei kiuhalisia ukawa na chama kwa mfano cha vijana waliosoma sana waislamu,wa kanda ya magharibi,wa kaila flani utakuta chama chako kimebaki na watu wachache sana. Unapaswa kuappreciate diverse nature of the tz society ili ukubalike kwa wote. kWA MFANO KAULI KUWA HAO WACHAGA WANA UMEME HADI MIGOMBANI---------mana yake si wenzetu hao haikuwa sahihi

Dogo/Kubwa una akili sana
 
Kwanza na-declare interest: Mimi ni mmoja wa watu niliokuwa nikimshambulia Zitto. Mimi nilitumia sana habari nilizosoma magazetini ambazo kwa kweli zilinishawishi na kuridhika kwamba Zitto alikuwa akitumika kuihujumu CHADEMA.
Lakini mimi ni mtu mwenye kupenda kusamehe na kusameheana. Zitto aliomba Ushahidi tuliokuwa tukimtuhumu nao, lakini mpaka leo hatujaleta Ushahidi. Damn you, Ushahidi, hata kama upo naomba tutupilie mbali mambo hayo tusameheane na tusonge mbele. Sana sana itaturudisha nyuma kwenye mparurano.
Nakumbuka wakati Zitto anafukuzwa alishambuliwa sana na aliumia sana. Jambo moja nililomsifu ni busara: Kukaa kimya na kusubiri ukweli. Aliweka akiba ya maneno kama alivotushauri Mzee Sheikh Thabit Kombo. Big up sana Zitto.

Jaribu kusahau tulivokushambulia na utusamehe. Wapo waliokushambulia binafsi (kama mimi) na wale waliokushambulia kwa niaba ya chama kama Tundu Lissu. Hayo ni mapito huenda ambayo yalipandikizwa na watu wa CCM kuweka mazingira flani kutushawishi kwamba wewe unatumika, ili tukufukuze, tusambaratike. Tulianza na Mungu, na bado aliendelea kutuunganisha. Mungu huyu huyu, ndo akaleta sakata la escrow ambalo umelishughulikia kiume kweli kweli. Nililia machozi uliposema “I missed the movement...”. Kubwa zaidi niliona hata kina Mbowe na Lissu ambao najua kimsingi huna ubaya nao, walionyesha kukukubali.

Huu uwe ni mwanzo wa kusameheana. Naomba Zitto urudi nyumbani, najua uliumia sana, lakini samehe, achana na mambo ya Ushahidi. Wasamehe waliokushambulia na urudi tupige kazi tuindoe CCM 2015. WELCOME BACK BUDDY.​
 
Kwanza na-declare interest: Mimi ni mmoja wa watu niliokuwa nikimshambulia Zitto. Mimi nilitumia sana habari nilizosoma magazetini ambazo kwa kweli zilinishawishi na kuridhika kwamba Zitto alikuwa akitumika kuihujumu CHADEMA.
Lakini mimi ni mtu mwenye kupenda kusamehe na kusameheana. Zitto aliomba Ushahidi tuliokuwa tukimtuhumu nao, lakini mpaka leo hatujaleta Ushahidi. Damn you, Ushahidi, hata kama upo naomba tutupilie mbali mambo hayo tusameheane na tusonge mbele. Sana sana itaturudisha nyuma kwenye mparurano.
Nakumbuka wakati Zitto anafukuzwa alishambuliwa sana na aliumia sana. Jambo moja nililomsifu ni busara: Kukaa kimya na kusubiri ukweli. Aliweka akiba ya maneno kama alivotushauri Mzee Sheikh Thabit Kombo. Big up sana Zitto.

Jaribu kusahau tulivokushambulia na utusamehe. Wapo waliokushambulia binafsi (kama mimi) na wale waliokushambulia kwa niaba ya chama kama Tundu Lissu. Hayo ni mapito huenda ambayo yalipandikizwa na watu wa CCM kuweka mazingira flani kutushawishi kwamba wewe unatumika, ili tukufukuze, tusambaratike. Tulianza na Mungu, na bado aliendelea kutuunganisha. Mungu huyu huyu, ndo akaleta sakata la escrow ambalo umelishughulikia kiume kweli kweli. Nililia machozi uliposema "I missed the movement...". Kubwa zaidi niliona hata kina Mbowe na Lissu ambao najua kimsingi huna ubaya nao, walionyesha kukukubali.

Huu uwe ni mwanzo wa kusameheana. Naomba Zitto urudi nyumbani, najua uliumia sana, lakini samehe, achana na mambo ya Ushahidi. Wasamehe waliokushambulia na urudi tupige kazi tuindoe CCM 2015. WELCOME BACK BUDDY.​

wewe mpumbavu hatuwezi kumjadili yeye kama anata kwenda aende we are not ready kuwabembelezwa wajinga, mbona hakwenda kuomba ushaidi mahakamani

Bali alienda mahakamni kutetea Ubunge wake
 
wewe mpumbavu hatuwezi kumjadili yeye kama anata kwenda aende we are not ready kuwabembelezwa wajinga, mbona hakwenda kuomba ushaidi mahakamani

Bali alienda mahakamni kutetea Ubunge wake
Ndiyo mimi ni mpumbavu. Nadhani utakuwa umenenepa sasa.
 
Mwanzoni nilikuwa nikimtetea sana Zitto kwa kuwa niliamini ni mtu anaejisimamia ila kwa hili la Escrow nimemshangaa sana, anatangaza kuwa pesa yote ya Escrow ni ya Umma wakati anajua hata Tanesco wenyewe walikuwa wanadai kiasi cha juu walichodai kimeongezwa kinyemela.
Ukitaka kumnunua Zitto kaulize bei yake kwa Mengi na Mkono.ataimba chochote hata ambacho hakipendi au hakiamini.Huyu mnafiki ni kama Jaja wa Yanga na kina Mengi ndo Maximo wake.
 
Mwanzoni nilikuwa nikimtetea sana Zitto kwa kuwa niliamini ni mtu anaejisimamia ila kwa hili la Escrow nimemshangaa sana, anatangaza kuwa pesa yote ya Escrow ni ya Umma wakati anajua hata Tanesco wenyewe walikuwa wanadai kiasi cha juu walichodai kimeongezwa kinyemela.
Ukitaka kumnunua Zitto kaulize bei yake kwa Mengi na Mkono.ataimba chochote hata ambacho hakipendi au hakiamini.Huyu mnafiki ni kama Jaja wa Yanga na kina Mengi ndo Maximo wake.
Ungetuwekea na ka ushahidi mjomba, ingetusaidia. Na ukisema Zitto alinunuliwa, maana yake wajumbe wote 19 wa CCM walinunuliwa, na wale 4-5 wa upinzani. Pia wabunge wote waliosuport PAC walinunuliwa na hao kina Mengi. Zitto alikuwa mwenyekiti tu, msemaji.
 
Atusamee nini wewe??? Yeye ndio aombe msamaha! Chadema kinasonga mbele bila zitto. Alifikiri yeye ni chadema kumbe alishanga kukuta chadema ni taasisi ambayo haimtegemei yeye.
 
Mh. Zitto Zuberi Kabwe malizana nachama chako haraka

Mhe. ZZK ufanye suruhu na chama chako haraka ili ukatetee jimbo lako ninakutabilia mambo mazuri, nina imani mkizungumza vizuri mtayamaliza. UKAWA inajipanga kuwa na wabunge wengi kwani kuwa na wabunge wengi ndiyo serikali yenyewe, akiwa rais huyo Pinda mtambuluza mnavyotaka atabaki analia tu. Chonde chonde ZZK fanya kweli, watakuona mjinga lakini kumbe wajinga wao.
Ninakuaminia.
 
kwani chama cha zitto ni chama gani?
 
Mh. Zitto Zuberi Kabwe malizana nachama chako haraka

Mhe. ZZK ufanye suruhu na chama chako haraka ili ukatetee jimbo lako ninakutabilia mambo mazuri, nina imani mkizungumza vizuri mtayamaliza. UKAWA inajipanga kuwa na wabunge wengi kwani kuwa na wabunge wengi ndiyo serikali yenyewe, akiwa rais huyo Pinda mtambuluza mnavyotaka atabaki analia tu. Chonde chonde ZZK fanya kweli, watakuona mjinga lakini kumbe wajinga wao.
Ninakuaminia.
ACT hawajajiunga na UKAWA, au unamuhesabia kule kwa Wakaanga Sumu?
 
Chadema ndio wanapaswa kumuomba msamaha Zitto maana wame mkosea sana! Hasa Slaa,Lissu,Lema na Mbowe ndio wanatakiwa kumuomba msamaha Zitto.

Ni ukweli ulio wazi Chadema hawana mbunge makini na mweledi kama Zitto Zuberi kabwe!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom