Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,198
- 7,539
kuna uhusiano wa karibu sana.kitu chochote kile huanza na imani na kisha utendaji.ndo maana hata nyrere alisema ujamaa ni imani.kwa hiyo mtu ukishajenga imani kuwa wewqe ni bora zaidi ya wenzako ni tatizomimi binafsi sioni uhusiano wa karibu kati ya watu kuitwa waheshimiwa na suala la ufisadi.[this means coefficient of correlation is equal to zero].
Haya ndio maoni yangu pia, ila tunamkumbusha tu Zitto alisema atawataja wenye fedha Uswisi ila nashangaa tena leo akiimiza Serikali itafute majina. huu ni usanii.Hivi tukiwafahamu hao walioficha fedha Uswisi, tukajua na kiasi walichoficha, halafu itakuwaje? Chenge tulimfanya nini tuliposaidiwa kufahamu kuwa ana dola milioni moja kule Jersey? Tuliisha ichakachua sana ile sheria iliyoanzisha TAKUKURU. Sheria ile ya enzi za Mwalimu mtu kama Chenge angesimama yeye mahakamani kutueleza amezipataje zile pesa. Sheria ya sasa inaitaka TAKUKURU ndio ichunguze, itafute ushahidi mzito sio wa kimazingira. Itaupata wapi?
Mwacheni Zitto aendelee kujikusanyia umaarufu wa bure tu.
Na mimi na muunga mkono Kinana uheshimiwa ni njia moja wapo ya kutengeneza matabaka ndani ya jamii.
Kabisa ndugu yangu. Tumelisema sana hili. Mwaka 2006 niliwahi kuhojiwa na kutamka sitaki kuitwa mheshimiwa. Ukisoma maandishi yangu au hotuba zangu bungeni ninaita watu ndugu. Hata interview ya juzi JF nimeita watu ndugu. Dkt. Slaa alilisema pia hili.
Tulipinge kwa kuwa Kinana kasema? Kinana ndio kasema baada ya sisi kusema, hivyo yeye katuiga sisi.
"Watanzania wamekosa matumaini, ni lazima tuanze upya kujenga matumaini kwa wananchi wetu"
"Bunge limeingia kwenye mtego wa kuanza kupoteza matumaini kwa wananchi"
"Vyombo vya habari zina nafasi kubwa sana ya kujenga imani kwa wananchi"
"Jamiiforums nimefanya mahojiano nao kwa masaa 8 wananchi wameuliza mengi, vyombo vya habari vina nafasi kubwa kwenye kurejesha imani kwa wananchi"
"Ripoti ya ngwilizi inatakiwa iwekwe wazi ili wabunge waijadili"
Kutoka kipindi cha mahojiano asubuhi hii ITV Zitto Kabwe ametangaza kumuunga mkono Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Kinana kwa uamuzi wake wa kukataa na kukataza wanaccm kuitana waheshimiwa. Anasema tulipoacha kuitana Ndugu ndipo matabaka na kasi ya kujilimbikizia Mali na madaraja katika utoaji huduma ilipoanza. Je, Ndugu ni physchological factor katika kujenga nchi moja. Tuendelee na mjadala.
Ametamka mwenyewe leo asubuhi kupitia ITV-Kumekucha kuwa hivi karibuni atakuwa Uswiss kuendelea na uchunguzi wa 'mihela' yetu iliyofichwa na mafisadi wa chama changu cha CCM na Serikali yake. Akadai kuwa atakutana na Wapelelezi wanaomsaidia kwenye suala hilo.
Sasa Zitto anatumwa na nani huko? Atafanikiwa? Hebu tujadiliane kwa kujenga
"Watanzania wamekosa matumaini, ni lazima tuanze upya kujenga matumaini kwa wananchi wetu"
"Bunge limeingia kwenye mtego wa kuanza kupoteza matumaini kwa wananchi"
"Vyombo vya habari zina nafasi kubwa sana ya kujenga imani kwa wananchi"
"Jamiiforums nimefanya mahojiano nao kwa masaa 8 wananchi wameuliza mengi, vyombo vya habari vina nafasi kubwa kwenye kurejesha imani kwa wananchi"
"Ripoti ya ngwilizi inatakiwa iwekwe wazi ili wabunge waijadili"
Kweli kazi ipo na Zitto anajitaidi kupanga mikakati yake lakini sioni kama "ndugu" na "mheshimiwa" kuwa ni chanzo cha kulimbikiza mali, ishu hapa ni ubinafsi wetu na kupenda kutumia ujinga wa walio wengi kwa manufaa ya wachache, watu hatujui haki na taratibu, hebu fikiria kama polisi wa barabarani unapogongana na mwenzako anakuja na kuwaambia malizaneni wenyewe au niwapeleke polisi wakati wote mmekata bima za magari yenu, ni tatizo zaidi ya hayo majina hapo Zitto
Zitto anatumika na JK ndiyo maaana kila siku anamsifu JK huku watanzania wengi wakimuona JK kilaza.tOO MUCH agenda zisizo na majibu.Mara kashirikiana na MEMBE kumhujumu Lowassa yaani full usanii.YANA MWISHO hata Lamwai alikuwahivyo leo kapotea .just wait and see