Zitto, Makamba wautaka urais?


Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 29th February 2012 @ 08:10

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, amesema maoni yake ya kutaka umri wa wagombea urais upunguzwe hayalengi yeye kugombea nafasi hiyo.

"Siwezi kutaka Katiba iandikwe kwa ajili yangu … isionekane kwamba matakwa ya muda mrefu ya vijana ya kutaka umri wa kugombea urais kupunguzwa, yanalenga kunipa fursa mimi.

"Mimi ni binadamu, naweza nisiwe na sifa za kuwa Rais, lakini kukawa na vijana wengine wengi wenye umri chini ya miaka 40 wenye uwezo na uzalendo wa kutosha kushika usukani wa nchi yetu," amesema Zitto katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.

Zitto amesema, anaona, kwamba ni vema yakapatikana mabadiliko ya vizazi katika uongozi wa nchi ili kukabili changamoto za sasa zinazokabili Taifa.

"Tunapojiandaa kutoa maoni kuhusu Katiba Mpya, ni vizuri vyombo vya habari vikajikita kutoa taarifa bila tafsiri au kuwatafsiria maoni ambayo wananchi na viongozi watakuwa wanatoa kuhusu maudhui ya Katiba Mpya," amesema.

Mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, amevishutumu vyombo vya habari vilivyohusisha kauli yake ya kutaka kupunguza umri wa kugombea urais na yeye kuutaka.

"Mimi nikiwa mwanachama na kiongozi wa chama changu, Chadema, naelewa na kuheshimu taratibu na kanuni tulizojiwekea za kuomba nafasi za uongozi, ikiwamo ya urais," amesema.

Ameongeza kuwa, nafasi ya uongozi ndani ya Chadema haiombwi kwenye warsha na kwamba iwapo wakati mwafaka utafika na kutokana na matakwa ya jamii, kikiona apewe jukumu lolote hatasita kutekeleza wajibu huo akiwa au bila kuwa mgombea.

Amesisitiza, kwamba alichozungumza juzi yalikuwa ni maoni yake na kwamba muda umefika kwa Taifa kupunguza umri wa kugombea urais, akisema maoni hayo yanazingatia ukweli, kwamba hakuna sababu zozote za kisayansi zinazomfanya mtu wa chini ya miaka 40 akose sifa za kuwa Rais.

"Msimamo huu nimekuwa nao tangu zamani nikisoma shule na haujawahi kubadilika. Hakuna mahala popote katika maoni yangu, niliyotoa jana (juzi) niliposema nataka umri wa urais upunguzwe ili nipate fursa ya kugombea urais," alisema Zitto.

Msimamo wa Zitto unafanana na wa Mbunge wa Bumbuli, January Makamba (CCM), na waliutoa pamoja juzi katika kongamano la kuelimisha vijana kuhusu Katiba lililomalizika jana Dar es Salaam.

 
Wote wanatamaa za uongozi, Zito tunamjua sana kwa mamboyake anayofanya awezi kuongoza nchi, kama anashindwa ku be organized kwenye chama chake ndiyo ataweza Nchi? jibu ni No is not smart enough to rule Tanzania for this time, Tukirudi kwa January tunaona wazi vitayake na Ngeleja ilivyo kuwa kubwa iyo yote anataka akabithiwe ile wizara ili nae apate ulaji kambla ya 2015, kwani anajua ikifika 2015 yeye anachake network yake itakua imepigwa chini labda atabakia na Ubunge tuu, soo wameamua kutafuta attention kutoka wa watu ili nao wasikike but sijaona kati ya ao wanaojiita Vijana anayeweza Kuongoza Nchi yetu.
 
Mimi sijawahi kukaa Chini na Zitto AMA na January lakini katika kusimamia maslahi ya nchi hujikuta tuna mambo tunakubaliana, naturally tu. Kila siku rafiki zangu huilaumu party caucus ya CCM wakidai inawafanya wabunge wanaotokana na CCM wasisimamie hoja za kitaifa na badala yake wasimamie mambo ya Chama chao. Leo hii inashangaza kuona wenzetu aw CHADEMA wanataka Zitto asifanane mitazamo na watu aw CCM!
 
Kigwa,kama CDM inasimamia mambo ya chama kuliko maslahi ya taifa nang'atuka!
 

Hv mi najiuliza sipati jibu kwani whts so special ktk CDM&CCM,kila jambo ni hawa tu, halafu kwani ukiwa ktk vyama unauzika uhuru wako binafsi kama wa kufanya vile unavyopenda, kushirikiana na watu ,hata wale walio ktk vyama tofauti..,kwa mtazamo wangu hawa jamaa kwanza nawapongeza japo wanakosa sapoti lakini lengo lao ni kuleta mapinduzi ya kifikra na mtazamo ktk siasa za TZ, waendelee 2po pamoja tutashinda
 
Mkuu kwenye itikadi hapo; Zitto na January wana itikadi moja in common: Wote wanapinga posho za vikao ila hao makamanda wengine unaosema hawana nia thabiti ya kuzipinga posho.
Kimbunga hivi hiyo ndiyo maana ya itikadi labda mimi ndiye sielewi maana yake.
 
Ukiacha John Mnyika hao vilaza wengine akina Lema,Msigwa,Sugu et al Zitto ataongea nao nini? Apoteze muda kufuatana na mbumbu ili iweje sasa? Nafurahia sana Urafiki wa Zitto na January wote wako Smart Kichwani!

that's duh!!!!
mwezi wa kwanza=nyepesi=smart ????????
nwayz that's ur thinking.
 
Wameunganishwa na common interests.Binafsi,sina imani na Zitto.
 
Slaa kaoa lini? Dr. Slaa ana mchumba. Na ni mgombea urais, pekee aliyezunguka nchi nzima na mchumba!
so what? Inakusaidia nini wewe kama mtanzania? au inakupunguzia nini wewe kama Mtanzania? Jiheshimu/Heshimu wenzio ili nawe uheshimiwe!
 

kwa nini age limit iwe miaka 35?kwa nini isiwe 39 au 18?
 
so what? Inakusaidia nini wewe kama mtanzania? au inakupunguzia nini wewe kama Mtanzania? Jiheshimu/Heshimu wenzio ili nawe uheshimiwe!

lipumba alikuwa mgombea urais pekee aliyezunguka nchi nzima(na sasa marekani nzima)bila ya kuwa na mchumba,mke wala demu..na jk alikuwa mgombea wa urais pekee aliyezunguka nchi nzima na mke mmoja na mwingine kabakia nyumbani na msururu wa vimada vinamuangalia kupitia runinga!!!!
 
this defence is too low and you can't fool me!!!hata kilaza lusinde hawezi kusema nataka umri upunguzwe ili nigombee urais!watu wana mashaka labda kutokana na mwenendo wako lately!!
 

To me also its my perception, hawa jamaa wakuwaangalia sana.
 
this defence is too low and you can't fool me!!!hata kilaza lusinde hawezi kusema nataka umri upunguzwe ili nigombee urais!watu wana mashaka labda kutokana na mwenendo wako lately!!
 
Ni Tanzania pekee mtu ambaye alikuwa mwandishi wa hotuba za rais anachaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge inayoshughulikia masuala ya energy; zaidi ya yote, nchi yetu ina gesi nyingi ya asilia na inategemea kuwa na mafuta siku za usoni. Vijana hawa wawili madaraka yamewaingia kichwani sana, na sifa wanazopewa kila siku, zimewaondolea unyenyekevu (humbleness) uliowafikisha hapo juu.

Ni muhimu kwa Zitto kufahamu ya kuwa sio kila kitu kwenye maisha unaweza kukipima (quantify) kwa njia ya kisayansi. Na vile vile, sayansi nayo haina majibu ya kila jambo. Kuna vitu kwenye maisha watu wanajifunza kutokana na experience zao katika maisha! Kwa hiyo kusema hakuna ushahidi wa kisayansi unaonyesha ni lazima mtu kuwa na miaka (at least)arobaini ili kuwa rais wa Jamhuri ni kupoteza umma.

Kwa kutumia Rationale ya Zitto, mtu anaweza kusema umri wa miaka kumi na nane kwa ajili kupiga kura ushushwe kwani hakuna ushahidi wa kisayansi, unaonyesha ya kuwa mtu akifikisha huo umri ndio anakuwa tayari kufanya maamuzi chanya. Mtu mwingine anaweza kusema, umri wa kupata leseni ya kuendesha gari nao...

Kingine kinachonikwaza hapa ni timing ya hili jambo. Inafahamika ya kuwa Zitto kufika mwaka 2015 hatakuwa hajatimiza umri wa kugombea urais. Kwa mtu yeyote anayejua kuconnect dots ataona ni kwa nini huyu bwana ameileta hii hoja kwa sasa...
 
Uxkonde......! Kila ki2 kpo poa but makamba ni mpiganaji zasy hata Mbowe alimkaribisha ajiunge na CDM pale bungeni so ni lazima ashikamane na mpiganaji mwenzake zitto.

Upiganaji wa makamba una contradiction kubwa kwa sababu ya mapatron wake kina EL na RA...haaminiki huyu hata kidogo
 


Mkuu acha kupotosha jamii,Prof Lipumba ana mke,hilo linathibitishwa kwenye CV yake. Tusipende majungu ya kike bila mpango wadau suala ambalo ni personal hata kama wewe ni National figure bora liendelee kuwa binafsi la kwako,haya mambo ya fulani sijui ana mchumba,mara sijui huyu ana wake kila kona tuwaachie wanawake wa uswahilini sisi tuangalie sera na ubora wa mtu kumchunguza maisha binafsi ni dalili ya kuwa mvivu wa fikra!!!
 

Mwakajilae,

Na wazee wanafiki tulio nao kwenye political landscape wanataka vijana wote Tanzania tuwe mazuzu namna hiyo ili waendelee kututumia.Tusikubali.....
 

Mkuu,

Hao ni blindfollowers kwenye siasa,sio wanachadema wote wanaoamini hivyo.Ni baadhi tu ya watu wachache wenye fikra mgando wanaojisingizia kuwa wanachadema.Hakuna mwanachadema mwenye akili timamu anayeweza kufikiria kama ulivyosema hapo juu..............
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…