Zitto kutimkia ACT-Tanzania?

Zitto kutimkia ACT-Tanzania?

Nenda bwana Zitto Nenda usaliti ujaanza leo:
Ona maneno ya Mwigamba akikulaumu kumuacha JUJU NDANDA na kumpendelea Rafiki yako Kafurila alipofukuzwa uanachama

"Nilitegemea mambo yasiyoendana na sera na kauli mbiu za chama chenu ambazo zinatangazwa hata katika jina la chama (DEMOKRASIA na MAENDELEO) ambayo yalifanyika pale ukumbini uliyaona.Najua jioni wakati wa kutangaza matokeo hukuwepo lakini nategemea ulipata taarifa za kauli za vijana mbalimbali walizotoa pale wakitaja waziwazi majina ya watu walioharibu uchaguzi ule.
Sikutarajia kama Naibu Katibu Mkuu wa chama upinge hatua ile iliyochukuliwa na msimamizi wa uchaguzi pamoja na kikao kingine chochote cha juu ya msimamizi wa uchaguzi eti kwa sababu tu rafiki yako Kafulila alikuwa anaongoza.
Hilo lilinipa taabu kubwa na naomba uniwie radhi rafiki
yangu lakini nasema ukweli wa nafsi yangu kwamba nilifikia kujiuliza mara mbilimbili kama ungechaguliwa wewe kuwa mwenyekiti wa chama hicho taifa, hali ingekuwaje?
Na mwisho nilipingana na wewe pale ulipopinga kwenye vyombo vya habari kuvuliwa wadhifa kwa David Kafulila. Kwanza ulionekana umeweka ubaguzi kwa sababu katika maneno yote uliyonukuliwa ulisisitiza juu ya Kafulila peke yake na hukumgusia kabisa Danda Juju wakati wote walivuliwa kwa sababu
zinazofanana.

Lakini kwa sababu Kafulila ni rafiki yako sana, umemwandaa kuwa mbunge na unamuunga mkono katika harakati zake, na ni mbunge mtarajiwa kwa kuwa anakubalika sana jimboni basi ukamtetea na kumsahau ‘mhanga' mwenzake. Hilo tu linafanya tutofautiane na zaidi sana tunatofautiana kwa kupinga maamuzi ya Katibu Mkuu wako nje ya vikao, maamuzi aliyoyachukua kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo"
Mwisho wa Kunukuu.
 
Wanafiki hutoka kwa unafiki wao na huo ndo uihiari wa kuondokana nao! Umeshiriki kutunga katiba halafu unapeleka suala hilo mahakamani maana yake umeihiari kutoka ndani ya chama! - Hiyali ndo nini tena!

Nashukuru umenielewa japo nimekosea! Asingekwenda mahakamani angeshafukuzwa uanachama siku nyingi alikwenda mahakamani kutafuta haki
 
kwenye escrow ni PAC ndiyo iliyochachamaa...Zitto alionekana zaidi kwa vile alikuwa ni mwenyekiti.

kwa hiyo sidhani kama escrow ndiyo kura yake ya turufu ya kumtoa...
Kumbuka pia kuwa tatizo lake kubwa ni hulka yake ya mimi, mimi, mimi (umimi - egocentrism). Kwa mtu wa hulka hii hawezi kushirikiana vizuri na wenzake katika kikundi cho chote kile (kiwe ni chama cha siasa au cha kuweka na kukopa) kwa sababu anataka yeye ndiye aonekane kinara mara zote, yeye ndiye abebe sifa, yeye ndiye yeye. Ndiyo sababu kubwa ambayo haikuweza kumfanya awe na ushirikiano mzuri na viongozi wenzake wa CDM na hivyo kupelekea mgogoro ambao hatima yake ni hii. Hata akienda ACT mambo yatakuwa yale yale tena mgogoro mkubwa hata kabla ya Oct. Ni hulka na kwa bahati mbaya haina dawa!!!!
 
10300231_10205227885349751_6771353628129122528_n.jpg
 
Wanabodi:

Hoja iliyopo ni kuwa ZZK sasa ni mwanasiasa anayening'inia. Ameshikiliwa na huruma za kibinadamu kwa wale wenye maamuzi ya kumalizia kumdondosha. Kwa kusema hivi sipingani na ukweli ulio wazi kuwa ZZK ni mwanasisasa mwenye haiba kubwa ya siasa, ambaye chama chochote kingependa kutumiaa haiba hiyo kama mtaji wake wa kung'ara kisiasa, Hata CDM wenyewe waliompiga chini.

Ni kutokana na tabia yake ya kutaka kung'ara kuliko chama chake na viongozi wake inafanya akose hadhi a kuendelea kuwa na nafasi ndani ya CDM.

Maamuzi ya ZZK nje ya CDM:
Kila kukicha na kwa taarifa zilizopo ni kuwa destiny ya ZZK ni ACT. Ni sawa; kwa siasa za kwetu na matakwa ya sheria zetu na katiba ni laima uwe mwanachama wa chama fulani. ACT ni chama chenye watu kama kina S. Mwigamba na Kitila Mkumbo. Wote hawa ni wanaharakati katika siasa za Tanzania. ZZK mwenyewe ni mwanaharakati. Chama chenyewe kinaanzishwa na wakongwe waliofukuzwa uanachama kutoka CDM-ambitious.

Maamuzi ya ZZK kubaki ndani ya CDM
Yanaweza kuwa ni maamuzi asiyoyapenda lakini ni uamuzi mzuri ambao yeye binafsi angeuangalia kwa makini na kutizama wapi ana mstakabali mzuri kisiasa. Aombe radhi kwa viongozi wake na chama asonge mbele. Dhambi ya usaliti ikianza haifi kama mla nyama ya mtu.
 
Zitto amesababisha Chadema imekufa

Hv kweli kuna mtu makini anaweza kuwa shabiki au mfuasi wa Zito?Haka kajamaa mimi nakafananisha na Chiluba.Karoho,kabınafsi na kanaelement za udikteta ukıkaangalia kwa umakını.Mtu yeyote asiyetaka ku-comply na matakwa ya group alilomo isipokuwa yeye, wengi huwa madikteta wakpata fursa za kisıasa.Na ZZK akipewa wenyekiti ACT,itathbıtisha hulka yake hii.Angelikuwa n mtu wa itikadi na falsafa,nna imani angepata chama mıongoni mwa vile vilivyokuwepo na kujiunga nacho badala ya CHADEMA.
 
...Kabla ya hao kina Mnyika, sijui mbali na John Mnyika walengwa wengine walikuwa kina nani!

Walikuwa wakina Nimrod Mkono na Pinda , Mkono ashampa zawadi ya Gari mbili, Pinda ndio sijui kama sio uenyekiti wa PAC.
 
Ndo kitu kinachoshangaza. Wamemfukuza wao na bado hawaishi kumuwaza. Tukiwaambia ndo mwanasiasa bora 2005-2015 wanakua wabishi ila vitendo vyao vinadhihilisha kukubaliana nat ukweli huo.

Ubora wa Zito nı katika ıshu ganı kubwa??Chadema ımepafanya vzurı serikali za mitaa ikıwa ZZK alishafukuzwa siku nyngi.Uamzı wa Chadema kumsımamisha Dr uchaguzi uliopita ndo sıri ya mafanıkıo,uchapakazı wa kamanda Mbowe umekuwa wa kupongezwa ndani na nje ya nchi.Hoja za wabunge machachali Lema,Wenje,Mnyika na kamanda Lısu zimekuwa kivutıo kwa wananchi walio wengi.Toka 2010, ZZT hajajenga hoja yoyote ya maana na yenye kuteka hisia za umma.Hakuwa kitisho kwa Spika wala serikali ukılınganisha na jabali Tundu,Lema au Mnyika ambao pindi waliposimama kıtı cha spika kililoa jasho.Hana lolote,amfuate Kaburu amsimulie!!
 
Kuna mambo mawili mnatakiwa kuyajua hapa....CDM wamecheza jambo kwa akili sana......na sio CDM wanaoumia hapa, ila ni Zitto ndio yuko kwenye wakati mgumu.

1.CDM hawawezi kumpa Zitto barua, wao kwa kusema tumemfukuza, imetosha kumuweka Zitto kwatika dilemma, kwa kuwa, mwenyewe Zitto yuko kwenye wakati mgumu kukaa bungeni kwa tiketi ya chama kilichokwisha mfukuza kwa maneno.
2.Inaonyesha kama CDM walishasoma mchezo wa Zitto, kama wasingemuwahi...lipo jambo angewawahi, maana hamna ajuae kuwa lile alilopanga kulifanya mwezi huu lilikuwa nini, so CDM wameamua kumpa mtihani wa kufanya maamuzi ya hatma yake mwenyewe.

Mwisho kabisa ni kwamba kwa CDM kusema tumemfukuza, na hali aliyonayo Zitto, yeye anataka apewe barua ili aende ACT kwa kusema "si nilifukuzwa na CDM" na wakati huo huo CDM hawatatoa barua kwa kuwa bunge lenyewe limeshaisha, ili kama kwa kuambia hivyo Zitto mwenyewe akiondoka kwenda ACT, CDM watasema "mmeona?? yeye ndio alitengeneza ACT akiwa ndani ya CDM, msaliti huyo"" na hii kete ndio ITAMUUA ZITO, kwa kuwa atakuwa ameprove yeye ni msaliti...........tusubili tuone hii sinema
 
Last edited by a moderator:
Wakuu,
Zitto tunamkubali sana, wala hakuna mwenye ugomvi naye. Kwa roho safi, tunamtakia maisha mema kwenye siasa za Tanzania. Binafsi simlaum yeyote kwenye kuyumba kisiasa kwa huyu Bwana. Zitto kajiharibia mwenyewe toka mwanzo kutokana na mwenendo wake wa siri na akina Kitilya et al. Lakini kubwa zaidi kuondolewa CDM ni mkakati ambao hata mafisadi wanahusika sana.
Jana alikataliwa kuliaga bunge, kumkatalia Zitto haikua uwezo wa spika bali ni akina Chenge na mafisadi wenzake. Kuna issue ya kutupilia mbali ombi lake mahakaman! lile sakata la Escrow wapo majaji wa mahakama kuu, sasa ukitazama kwa makini utagundua hali halisi.

Tunamtakia maisha mema kisiasa, akiwa mstaarabu ajipange upya tena kwa busara kuliko kukurupuka. Hii itamjenga zaidi. Ningekuwa yeye ningejipa nafasi ya kutafakari hata miezi mitatu kisha ndo nichukue maamuzi.
 
Will never ever discuss ZZK any more. Let him join his traitors (ACT members). Such a huge stumbling block to quick liberation of our Nation.

Kuna mtu alisema ACT, means, Alliance of Cowards and Traitors. Good bye ZZK, will never write anything concern your any more.
 
Back
Top Bottom