Zitto kung’oka CHADEMA

Zitto kung’oka CHADEMA

Akili ya zitto peke yake ni zaidi ya uongozi wa chadema taifa kwa pamoja yao

Nadhani hiyo itakua ni nafuu kwa CCM kwa sababu mtu mwenye akili nyingi namna hiyo akiondoka kwenye chama kinachowakosesha CCM usingizi si ni afadhari.We huoni kama mchezaji hodari akiwa hayupo ni nafuu kwa timu pinzani.
 
Hamna watu nilipata kuwaamini humu kama wewe, kumbe nawe unahubiri siasa za ukabila, amekosa mtu sio Kigoma, na kama kigoma ndio mwathirika wa siasa za usariti basi mjitazame upya, kwanini kila siku ninyi, nilipata kuongoza seriksli moja ya wanafunzi chuo kikuu, msaidizi wangu alikuwa dada wa kigoma baada ya mgomo akaniruka hatua 100, hili nalo tusiseme, kuna tatizo Kigoma jamani kwenye misimamo. Sorry kama ntamkwaza mtu


Hapana uko sawa kama SIASA unaangalia an individual or a society...

Wewe uko based with an individual kwahiyo chochote kibaya hautataka kumhusisha just because you love his individualism

Mfano; Angalia ni kwanini Kenyatta yuko THE HAGUE ?

Sasa turudi kwa KABWE... Kwanza alitaka kuanzisha Bendi ya wana KIGOMA na yeye awe kama Investor; WanaKigoma ina Maana waliozaliwa huko... Nchi yetu ya TANGANYIKA haijawahi kuwa na Masuala kama hayo; Hadi enzi za TIMU za MIKOA zilikuwa sio za KIKABILA...

Amepata Matatizo na CHAMA CHAKE yeye as an individual ni kwanini MCHADEMA yoyote aliyekwenda KIGOMA alikimbizwa na kupewa Ultimatum - to leave that REGION as if BOKO HARAM take Over?

Siasa sio CHUKI na Kukomoana au kutishia baadhi ya watu wa upande fulani...

Wanao EMBRACE vitu kama hivyo ina Maana wana ufinyu kimadaraka na pia wana chuki... nadhani uliona Mikwaruzano kati ya BILL CLINTON na OBAMA; BILL CLINTON speech ilisababisha OBAMA akashindwa kura katika jimbo la TEXAS...

Lakini baada ya OBAMA kumshinda HILLARY ni huyo huyo BILL CLINTON aliyetoa speeach mura kabisa iliyowaunganisha DEMOCRATS wote wenye itikadi Mbalimbali... na kumuwezesha OBAMA kushinda kwa LANDSLIDE...

Sasa, ni tofauti gani hizo ZITTO anazo zinazomfanya aondoke CHADEMA na ku create a barrier ?? OBAMA na HILLARY ndio walikuwa wanatupiana Maneno ya ajabu lakini ni tu waliheshimu kura za Wananchi wao

Kwani kweli hatuwezi kuijenga DEMOKRASIA ya kweli ? ZITTO ni only 36yrs OLD ana URAIS KIBAO

Angalia VIZURI hiyo HABARI uliyoiandika - Issue sio KIGOMA Issue is DIVISIONs created by POLITICIANS into their REGION


c.c
chikutentema
 
Kama ameshindwa hata kulitolea tamko marehemu mama yake kupigishwa kura kwenye BMK, sidhani kama anaweza kuaminika kwa chochote.
 
Hivi Zito bado yupo chadema!! Hawezi kutoka bora abane hapo hapo,atapotea.
 
Kama ameshindwa hata kulitolea tamko marehemu mama yake kupigishwa kura kwenye BMK, sidhani kama anaweza kuaminika kwa chochote.

hawezi toa tamko habari za uongo na uzushi
 
Hapana uko sawa kama SIASA unaangalia an individual or a society...

Wewe uko based with an individual kwahiyo chochote kibaya hautataka kumhusisha just because you love his individualism

Mfano; Angalia ni kwanini Kenyatta yuko THE HAGUE ?

Sasa turudi kwa KABWE... Kwanza alitaka kuanzisha Bendi ya wana KIGOMA na yeye awe kama Investor; WanaKigoma ina Maana waliozaliwa huko... Nchi yetu ya TANGANYIKA haijawahi kuwa na Masuala kama hayo; Hadi enzi za TIMU za MIKOA zilikuwa sio za KIKABILA...

Amepata Matatizo na CHAMA CHAKE yeye as an individual ni kwanini MCHADEMA yoyote aliyekwenda KIGOMA alikimbizwa na kupewa Ultimatum - to leave that REGION as if BOKO HARAM take Over?

Siasa sio CHUKI na Kukomoana au kutishia baadhi ya watu wa upande fulani...

Wanao EMBRACE vitu kama hivyo ina Maana wana ufinyu kimadaraka na pia wana chuki... nadhani uliona Mikwaruzano kati ya BILL CLINTON na OBAMA; BILL CLINTON speech ilisababisha OBAMA akashindwa kura katika jimbo la TEXAS...

Lakini baada ya OBAMA kumshinda HILLARY ni huyo huyo BILL CLINTON aliyetoa speeach mura kabisa iliyowaunganisha DEMOCRATS wote wenye itikadi Mbalimbali... na kumuwezesha OBAMA kushinda kwa LANDSLIDE...

Sasa, ni tofauti gani hizo ZITTO anazo zinazomfanya aondoke CHADEMA na ku create a barrier ?? OBAMA na HILLARY ndio walikuwa wanatupiana Maneno ya ajabu lakini ni tu waliheshimu kura za Wananchi wao

Kwani kweli hatuwezi kuijenga DEMOKRASIA ya kweli ? ZITTO ni only 36yrs OLD ana URAIS KIBAO

Angalia VIZURI hiyo HABARI uliyoiandika - Issue sio KIGOMA Issue is DIVISIONs created by POLITICIANS into their REGION


c.c
chikutentema

Asante kwa kueleza kuwa issue ni division, lakini kwanini hata wanahabari mmekuwa ni sehemu ya hiyo kampeni ku-justify the lies. Sijakataa kuwa Zitto anaumri huo unaousema lakini si yeye pekee kijana kwenye jamii ya watu mil. zaidi ya 45, wapo wengi wenginge hawajapata tu platforms tena yawezekana wenye karama hasaa na huo unaoitwa uzalendo. Mimi mwenyewe sifurahii kwa haya yaliyomkuta kijana huyu Zitto lakini wawezaje kuzuia kitu kilichoasisiwa na muhusika kwani tunaamini kila unachofanya at a moment kina results kesho. Anyway hoja zijengwe tuhukumiane lakini niweke wazi sipendi mtu anayejaji kitu kwa kutumia, dini, kabila, rangi, ufupi, urefu, uzima ama ulemavu kwani hata Mwal. Nyerere alisema mtu wa aina hiyo hana hoja na wala uhalali wa kupewa anachopigania nngu007
 
Last edited by a moderator:
Zitto akifanya hivyo atakuwa ametenda kwa busara. Lakini pia akifika kule ACT awaelimishe kuwa adui yao si CHADEMA au CUF au NCCR bali malengo yao makuu ni kuleta mabadiliko yatakayoifanya nchi kaendelea kwa kuhakikisha CCM au chama chochote kinachoshikaab serikali hakipati 'absolute majority' na kufanya watakavyo bila woga.

Hata hivyo natabiri ACT kuwa kama TLP na UDP labda itokee miujiza. Mwaka mmoja hautoshi kujenga chama kikapata mafanikio makubwa.

Mkuu Getstart, Hapo kwenye red ndio mtihani mkubwa uliompa ZZK ambao nna uhakika hawezi faulu.Shida inakuja pale ambapo nia yake sio mabadiliko ya watanzania bali maslahi yake na miCCM.

Naamini kama ZZK angekuwa na dhamira safi na CDM haya yote yasingetokea, ila kwa matendo yake na ACT yake nashawishika kusema ametumwa, na huko atakakoenda ataenda kuendeleza kile alichotumwa na kushindwa ndani ya CDM.
 
Zitto unatisha ndo maana Mbowe na magazeti yake wanakufuatilia sana.
 
Zitto anachukiwa na viongozi wa chadema, wakamfitni kisa hatoki kaskazini. Ubaguzi ndani ya chadema ni mkubwa sana


Hii single ilishachuja muda mrefu ,tafuteni nyingine mje nayo.
 
Bado anasubiri nini???? Apotee !!! Au ile kauli yake ya "Nitakuwa mtu wa mwisho kutoka CHADEMA" inamhangaisha????
 
zitto hayupo chadema tulimshamfukuza siku nyingi akakimbilia mahakamani labda na huko ameshashindwa ndo maana aende kwa wanafiki wenzake ccm au act
 
Akili ya zitto peke yake ni zaidi ya uongozi wa chadema taifa kwa pamoja yao
Kumbe wewe ndiye yule mgombanishi aliyetajwa na ZZK. Mwacheni ZZK afanye maamuzi yake mwenyewe. Sasa anattaka kutubu na kurejea CDM yetu hata bila ya uongozi kwani anajua uongozi ni dhamana. Mshindwe wachonganishi wote.
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), inadaiwa yupo katika hatua za mwisho kujiengua ndani ya chama hicho alichojijengea sifa kubwa

Kwa mujibu wa watu walio karibu na Zitto, wamelidokeza Tanzania Daima Jumapili, kuwa mbunge huyo alipanga kujiondoa ndani ya chama hicho mwezi uliopita lakini alishindwa kufanya hivyo kwasababu ambazo hazijawekwa wazi.

Inadaiwa Zitto, alipanga kuondoka CHADEMA sambamba na uzinduzi wa kitaifa wa chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania) uliopangwa ufanyike mwezi uliopita.

Novemba 22, mwaka jana, Kamati Kuu ya CHADEMA iliamua kumvua nyadhifa za uongozi Zitto na wenzake wawili (Dk. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba) kwa madai ya kukisaliti na kukihujumu chama.

Zitto alidaiwa kuwa kinara wa mkakati wa kuleta mabadiliko haramu ndani ya chama hicho, huku waasisi hao wakijipa majina ya MM, M1 na M2 ambao ndani yake anadaiwa kuwamo Dk. Kitila Mkumbo, mjumbe wa CC na NEC.

Hata hivyo Mkumbo na Mwigamba walivuliwa uanachama huku Zitto akikimbilia Mahakama Kuu kutaka CC isijadili unachama wake.

Katika hoja ya msingi iliyowasilishwa na Zitto kupitia wakili wake Albert Msando, aliiomba Mahakama Kuu kuwazuia washitakiwa kwa pamoja ambao ni Kamati Kuu ya CHADEMA au chombo chochote kwa makusudi, kujadili au kuamua suala la uanachama wake.

Maombi mengine ya Zitto ni kutaka apatiwe nakala za uamuzi wa Kamati Kuu iliyoamua kumvua uanachama ili aweze kukata rufaa kwa Baraza la Uongozi la CHADEMA.

Katika ombi la tatu, Zitto anaiomba mahakama iwazuie washitakiwa kuingilia kati wajibu na majukumu yake ikiwemo majukumu yake kama mbunge wa Kigoma Kaskazini.

Mahakama Kuu ilikubali kwa muda kusitisha uamuzi wa CC ya CHADEMA kujadili uanachama wa Zitto mpaka itakapotoa uamuzi wa katika kesi ya msingi iliyofunguliwa na mbunge huyo.

Katika amri hiyo, Jaji John Utamwa alisema kwa kuzingatia masilahi ya pande zote mbili ni vema walalamikiwa wakasitisha uamuzi wowote wa kujadili uanachama wa Zitto mpaka shauri hilo litakapotolewa uamuzi na mahakama.

Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa Zitto, anatarajia kwenda ACT-Tanzania kushikilia wadhifa wa Mwenyekiti wa chama hicho ambacho makada wenzake Mkumbo na Mwigamba wamekimbilia.

Harakati hizo za Zitto, zinadaiwa kushamiri zaidi hivi sasa baada ya CHADEMA kumaliza uchaguzi wake wa kitaifa na nafasi aliyokuwa akiishikilia imejazwa na John Mnyika

Kumalizika kwa uchaguzi wa CHADEMA, uliofanyika kwa utulivu hivi karibuni kunatajwa sababu ya Zitto kukata tamaa ya kurejea madarakani hivyo anaona njia pekee ya kujinusuru kisiasa ni kuhama CHADEMA.

Mbunge huyo kabla ya kukimbilia mahakamani alitaka kiitishwe kikao cha Baraza la Uongozi ili apewe fursa ya kujitetea ambako aliamini atapata uungwaji mkono

Hata hivyo tangu Zitto atoe ombi hilo Baraza hilo limeketi mara mbili bila kuwepo ajenda inayomuhusu kujadiliwa jambo lililoashiria hakukuwa na uungwaji mkono

Zitto afunguka

Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili, juu ya taarifa za kujitoa CHADEMA, Zitto alisema kwa muda mrefu kumekuwa na taarifa potofu dhidi yake.

Alisema baadhi ya taarifa zina lengo la kumchonganisha na kumharibia sifa yake mbele ya jamii na makada wenzake.

Zitto alisema jambo lolote linalomhusu hatosita kulizungumzia mwenyewe kama alivyowahi kufanya katika masuala mbalimbali.

Alisema kwa muda mrefu kumekuwa na mambo yanayovumishwa dhidi yake ambayo hayana ukweli

Zitto, alibainisha kuwa ikiwa ataondoka au ataendelea kubaki CHADEMA jambo hilo analijua mwenyewe.

“Watu wasema mambo kwa kuhisia hisia, mimi ndiye ninajua ninachokifanya……Hizo nyingine ni hisia za watu siwezi kuzizuia” alisema

“Nawaomba watu wajiepushe na maneno maneno ya mitaani, nina uwezo mkubwa wa kuzungumzia masuala yanayonihusu” alisema.

Dk. Slaa anena

Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willibrod Slaa, amesema ni haki ya kikatiba na ruhusa kwa mwanachadema yoyote kuhamia chama chochote cha siasa anachoona kinamfaa.

Dk. Slaa, alisema fununu za aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zitto Kabwe, kutaka kujiunga na chama kipya cha ACT Tanzania, anazisikia na hawezi kumzuia kuhamia huko.

Alisema haoni kama anayo sababu yoyote ya kumjadili Zitto katika uamuzi wake wa kutoka CHADEMA na kuhamia chama kingine.

“S mimi Dk. Slaa wala CHADEMA, wanayo sababu yoyote ya kumjadili mtu na uamuzi wake mwenyewe …anayo haki ya kuhamia chama chochote ambacho ataona ana manufaa nacho, hana haja ya kupata kibali cha mtu”

“Zitto hatokuwa mwana- CHADEMA wa kwanza kuhama cha hiki na wala hatakuwa wa mwisho ….wengi watahama na wengi watahamia hivyo sioni kama kuna dhambi yoyote hapo” alisema

Katibu Mkuu huyo alisema kwa sasa hayuko tayari kuzungumzia mwanachama anayehama na kuhamia, bali yuko tayari kujadili maslahi ya Watanzania na nchi hasa suala la katiba iliyopendekezwa.

“Kichwa changu sasa kinafikiria ni namna gani kitawasaidia Watanzania waikatae katiba inayopendekezwa ambayo imechakachukuliwa kwa ajili ya manufaa ya watu wachache” alisema.


Chanzo: Tanzania Daima

Kwani sasa hivi yuko cdm? Mbona alifukuzwa siku nyingi?
 
Zitto anachukiwa na viongozi wa chadema, wakamfitni kisa hatoki kaskazini. Ubaguzi ndani ya chadema ni mkubwa sana

Ubaguzi ndani ya cdm ni mkubwa kama ilivyo wizi wa rasilimaki za taifa ndani ya viongozi wa ccm.
 
Back
Top Bottom