Kaka yangu Watanzania tumekubali kufanywa mazezeta kwa kukubalia haya:
Nikikuchukia basi nataka watanzania wote wakuchukie mfano halisi ni JK chuki ya JK kwa Lowassa imetufanya watanzania wengi tumchukie Lowassa badala ya kuchukia Matendo ya Lowassa na yanayoshabiahiana na hayo mfano ufisadi na rushwa na si kumchukia mtu.Kama tungekuwa na akili kuanzia ndani ya CCM wasingelikubali hilo leo tusingekuwa hapa tulipo.
Pili tunapumbazwa na lugha za vitisho na chuki ili tugawanyike na wachache waendelee kula raslimali zetu bila kutumia nguvu nyingi.Leo tumewekewa chuki na visasi kwa wenye nacho bila kujiuliza utajiri wao umepatikanaje??Hivi ni kweli matajiri waote ni lazima wawe wameiba??Je wanaCCM walioiba raslimali zetu na leo wako madarakani wamefanywa nini??Je hawa matajiri ni hawa wawili tu Manji na Mbowe ndiyo waliyotuletea umasikini Tanzania??Je wale wa Escrow,UDA,Stanbic,Richmond,Kivuko kibovu,nyumba za serikali,Green blblah,makaa ya mawe,madini yetu,hawa viongozi walioletea Taifa hasara wamefanywa nini??Hivi ni halali tuawasulubu hawa wawili tu??
Hivi tumeshindwa kabisa kujiuliza tatizo ni nini??Kwanini tujengewe chuki na viongozi wa dini wakubaliane nayo wanalipwa nini??Ni aibu kwa Taifa lenye viongozi wa dini na wastaafu kuliangalia hili kisa ni uoga,basi bora usizaliwe kama upo kwenye nafasi badala ya kutetea haki uko busy kuongeza chuki,basi hustahili kuishi.
Kuna baadhi yetu ukiona hoja zetu 100% ni Ubaguzi,Chuki na Visasi sababu tu viongozi/watawala hawawapendi wapinzani,kaka tunatakiwa kubadilika.
Mkuu nakuvulia kofia kama hata robo ya watu humu ndani wangekuwa na mawazo kama yako, tungekuwa tunajadili mambo ya muhimu na wanasiasa labda wangebadilika maana wangejua tunakijua nini wanachokifanya. Mitandao imesaidia nchi nyingi duniani kuleta mabadiliko ya kiuchumi na siasa. Lakini mitandao ya Tanzania inawasaidia walio madarakani na wanaotaka kuingia madarakani kufuja kila kitu sababu kitu kikubwa kwako ni support kubwa wanayoipata kutoka kwa makundi yaliyogawanyika.
Makonda kataja majina ya wanaoshukiwa kuwa wauzaji na watumiaji unga. Kashambiliwa na wabunge wa pande zote mbili CCM na UKAWA. Sina hakika kama waliungana kwa kuilinda katiba, niasema hivi sababu kabla ya kutajwa Mbowe na Manji na Zungu hakuna aliyesema hili ni kosa. Hapa ni unafiki mkubwa kwa makundi yite mawili.
CHADEMA walitumia haki gani kumtangaza Lowasa na wana CCM wengine kama ni wezi na mafisadi????
Nape na CCM yake walitumia kifungu gani kumtangaza nchi nzima Lowasa kama ni fisadi wakati mimi na wewe tunajua kuwa Mahakama peke yake ndiyo yenye uwezo kikatiba kumhukumu mtu kama mwizi ama fisadi, naomba wewe unisaidie wapi Nape na Slaa ama Lissu waliitwa na kikao chochote cha Bunge kuulizwa kama Makonda alivyoitwa???? Hakuna jibu la maana utalipata lakini kama ulivyosema hivi sasa mpaka humu JF watu wanajitoa akili kwatetea wabunge kwa kumwita Makonda. mimi binafsi sioni kosa alilolifanya Makonda kwa nchi kama ya kwetu ambayo sijui kama ina Katiba kweli ama ni kama Somalia.
Kuhusu mabadiliko, Ndugu yangu si rahisi kuyapata mabadiliko ya kweli. Mimi ni mmoja wa vijana wa wakati huo mageuzi yalivyoanza na tulihamsika zaidi ya watu uliowaona mwaka jana maana sisi tulitumia akili zetu hatukuwa nyumbu. Tatizo lilonikwaza niachane na siasa za upinzani na kuwa mtazamaji ni pale Kina marando, Lamwai, Mtei, Seif na wengine wengi walipodharau maoni ya wana mageuzi wa kweli kina Mzee Chief Abdalah Fundikira, James Mapalala, kasanga Tumbo na wengine ambao kweli walikuwa wanamageuzi ambao walimsumbua Nyerere miaka ya sitini wakidai vyama walipotaka serikali ya mpito wakati tunaisubiri katiba mpya ambayo ingetutoa na unyonge wa kuwa na katiba ya chama kimoja. NCCR lengo kubwa lilikuwa kuomba katiba mpya lakini njaa ama tama ya madaraka iliwafanya viongozi wetu watufikishe hapa tulipo. Na siku zote hua nasema hii dhambi itawatafuna sana UKAWA sababu walitusaliti watu wengi tuliowaamini.
Wakiwa wanapigwa virungu hua siawaonei huruma. Mtikila watu walimuona kama kichaa lakini kwangu mimi Mtikila alikuwa na maana zaidi kuliko hawa wachumia tumbo wa CCM na UKAWA
Mtikila alifungua kesi kama tatu za kikatiba ambazo
Kesi za kikatiba ambazo aliwahi kuzifungua ni pamoja na kesi ya kutaka wagombea binafsi kuruhusiwa katika uchaguzi Tanzania, wananchi wa Tanzania Bara kuruhusiwa kwenda Zanzibar bila passport na vyama vya siasa kuruhusiwa kufanya mikutano bila kuomba kibali toka kwa Wakuu wa Wilaya ama Polisi. Lakini wakati mchungaji Mtikila anapata misukosuko hakuna hata mwanaisasa mmoja wa upinzani alimuunga mkono. mtikila aliishia kupelekwa gerezani kwa kupigania haki za watanzania za kikatiba lakini sasa tuna watu wanaitwa makamanda wanawekwa ndani kwa kutukana lakini tunawaita ndiyo wapigania haki. Haki gani unaipigania kwa kutukana watu??????
CCM na wabunge wake nao wana share ya kuturudisha nyuma kiamendeleo kwa ku ng'ang'ania katiba ya chama kimoja. Historia inatuambia wanyonge hawawezi kubaki kuwa wanyonge siku zote pale Mtikila mwingine akitokea na kutuhamasisha kama Mtikila alivyofanya miaka ile ya tisini pale viwanja vya jangwani najua fika kutakuwa na Burkina Faso ya Tanzania.
Lakini mpaka hapo atakapotokea Mtikila wa 90s' sioni kama kuna mtu yeyote mwenye mapenzi ya hii Nchi zaidi ya matumbo yao awe CCM ama CCM B ambayo ni UKAWA. Na watu wa kuweza kumpa nguvu Mtikila mwingine wa miaka ya 90 ni sisi lakini sioni kama wapo hapa JF zaidi ya makundi ya ku support chuki binafsi.