Zitto Kabwe: Tunakwenda Arusha kesho

Magesi

JF-Expert Member
Jul 10, 2012
2,587
577
Waziri kivuli wa fedha Mh.ZITTO KABWE hatasoma bajeti ya kambi ya upinzani kwani wabunge wote wa CHADEMA watakwenda ARUSHA kesho.SOURCE FACEBOOK WALL YA ZITTO MUDA HUU.
 
Waziri kivuli wa fedha Mh.ZITTO KABWE hatasoma bajeti ya kambi ya upinzani kwani wabunge wote wa CHADEMA watakwenda ARUSHA kesho.SOURCE FACEBOOK WALL YA ZITTO MUDA HUU.

Hiyo hotuba ya CHADEMA atuwekee hapa Jamvini tu maana kwa MACCM tukio la Arusha ni shangwe maana kama tungekuwa na Bunge makini kesho ingekuwa siku ya off kama walivyofanya kwenye mambo ya Mtwara, nadhani Mtwara walikatisha shughuli za Bunge kwa vile tukio lile likuwa linahatarisha maslahi ya CCM na mikataba feki na wawekezaji/wauzuajiwa raslimali zetu.

Hamtapoteza kitu waachieni Bunge wapitishe haraka haraka bajeti ya majanga, maana sisi raia hatuoni kitu hapo, Tunawashukuru sana watetezi wetu. Mungu awe nanyi katika safari ya Arusha.
 
Kwa kilichotokea ni vizuri viongozi wote wawe na mshikamano wa pamoja kwani kwa sasa adui Namba moja wa CCM ni CHADEMA wameishasahau adui ambae alikuwa anaimbwa kila siku na Baba wa Taifa(R.I.P) ambae ni Elimu, Maradhi na Umasikini.
 
Mhe. Zito. Habari kama hii uweke na hume JF kwani wewe ni verified member. Huko Face book wengine hatuingii. Kuna utoto zaidi. Hata hivyo huo ni uamuzi bora sana.
 
Hiyo hotuba ya CHADEMA atuwekee hapa Jamvini tu maana kwa MACCM tukio la Arusha ni shangwe maana kama tungekuwa na Bunge makini kesho ingekuwa siku ya off kama walivyofanya kwenye mambo ya Mtwara, nadhani Mtwara walikatisha shughuli za Bunge kwa vile tukio lile likuwa linahatarisha maslahi ya CCM na mikataba feki na wawekezaji/wauzuajiwa raslimali zetu.

Hamtapoteza kitu waachieni Bunge wapitishe haraka haraka bajeti ya majanga, maana sisi raia hatuoni kitu hapo, Tunawashukuru sana watetezi wetu. Mungu awe nanyi katika safari ya Arusha.

kidogo kwa leo hiyo hapo

MAENDELEO YA MICHEZO

Mheshimiwa Spika, maendeleo mazuri ya michezo katika taifa lolote, ni utambulisho mzuri wa taifa hilo katika mataifa mengine kutokana na ushirikiano wa kimichezo na mataifa hayo. Pamoja na mambo mengine, michezo katika nchi yetu inaweza kutumika kutengeneza fursa za kiuchumi kwa kuitangaza nchi yetu duniani katika sekta za utalii na uwekezaji. Ukiacha mbali suala la manufaa ya kiuchumi yanayoweza kupatikana kupitia michezo, michezo pia inawajengea vijana wetu afya na hivyo kuwa na taifa la watu wakakamavu. Kwa upande mwingine, michezo pia ni ajira. Inasikitisha kwamba katika hotuba nzima ya Waziri wa Fedha, hapakuwa na mpango wowote wa kukuza michezo hapa nchini bila hata kujali kwamba timu yetu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ipo katika nafasi nzuri sana hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote katika kuweza kufuzu kucheza fainali za kombe la Dunia mwakani.
Mheshimiwa Spika, Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii katika barua yake ya tarehe 5/4/2013 iliomba Kamati ya Bajeti kuangalia namna ya kusaidia kupata fedha za kujenga michezo na hasa kusaidia Taifa Stars katika juhudi zake za kuelekea kufuzu kwenye michuano ya kombe la Dunia huko Brazil. Hata hivyo Wizara ya Fedha haikutoa hata senti tano kwa ajili hiyo. Kamwe hatuwezi kufanikiwa kwenye michezo bila kuwekeza na kutegemea juhudi za dharura za kamati za kusaidia ushindi. Tukitaka tung’ae kwenye michezo ni lazima tuwekeze sana na kuwekeza ni gharama, gharama ambayo thamani yake ni kubwa sana kwa nchi.
Mheshimiwa Spika, licha ya michezo kuliingizia taifa mapato kupitia asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) inayotokana na viingilio katika michezo mbalimbali, hakuna uwekezaji wowote wa maana uliofanyika kwenye michezo jambo ambalo ni hatari kwa uhai na maendeleo ya michezo hapa nchini. Aidha hakuna mipango madhubuti ya muda mrefu kuhusu maendeleo ya michezo hapa nchini.
Kutowepo kwa mipango madhubuti na ya muda mrefu, kumeshababisha timu zetu kufanya vibaya katika mashindano mengi ya kimataifa na hivyo kulifanya taifa letu lionekane kuwa ni taifa dhaifu au kichwa cha mwendawazimu kama alivyopata kusema Rais Mstaafu was Awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi. Kambi Rasmi ya Upinzani, inatoa angalizo kwa Serikali kwamba, kamwe hatuwezi kufanikiwa katika michezo kwa mipango ya kukurupuka. Aidha ni aibu kwa Serikali kukusanya kodi kutokana na michezo, halafu vijana wetu wanakosa fedha ya nauli kwenda nchi nyingine kwa mashindano ya michezo mpaka wafanye harambee ya kukusanya fedha kwa wahisani. Hivyo, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na CHADEMA inapendekeza mambo yafuatayo yafanyike ili kunusuru tasnia ya michezo hapa nchini;
1. Timu yoyote itakayowakilisha taifa katika mashindano yoyote ya kimichezo igharamiwe na Serikali kwa asilimia 100.
2. Viwanja vyote vya Michezo hapa nchini viundiwe Wakala wa Serikali, Wakala wa maendeleo ya michezo (Sports Development Agency). Wakala huo uwe na majukumu ya kujenga viwanja vipya na kusimamia viwanja hivyo kwa niaba ya Serikali. Viwanja vyote vya michezo vilivyoporwa na CCM kama Lake Tanganyika – Kigoma, Ali Hasan Mwinyi - Tabora, Kirumba – Mwanza, Maji Maji – Songea nk virejeshwe Serikalini mara moja chini ya Wakala wa Viwanja vya Michezo. Wakala pia ujenge academies za michezo maeneo kama vile Mbeya, Tanga, Mtwara, Mwanza, Manyara na Dar es Salaam ili kukuza vipaji vya watoto na vijana.
3. Mashirika yote ya Umma, hasa mashirika makubwa yawe na timu za michezo. Ushauri uliotolewa na IMF na Benki ya Dunia dhidi ya Mashirika ya Umma kuwa na timu ulikuwa ushauri usio wa maana. Wenzetu Uganda kwa mfano, Mamlaka ya Mapato Uganda (URA) wana timu katika ligi Kuu, ambayo ni moja ya timu mahiri katika ukanda huu wa bara la Afrika.
4. Serikali ianzishe Mfuko Maalum wa Michezo (Sports Fund). Pia, Serikali ianzishe Kodi ya Maendeleo ya Michezo (Sports Development Levy). Kodi hii ipatikane kama ifuatavyo: Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ya asilimia 18 iliyokuwa ikikatwa kwenye viingilio katika michezo mbalimbali iondolewe na badala yake kiasi hichohicho kiingizwe kwenye Mfuko wa Michezo (Sports Fund) utakaoanzishwa.
5. Matumizi ya Mfuko wa michezo yawe kama ifuatavyo:
i. Asilimia 50 ya fedha zitakazokusanywa zitumike kujenga miundombinu ya michezo (Sports Infrastructure) kupitia kwa Wakala wa Maendeleo ya Michezo na Academies.
ii. Asilimia 50 inayosalia itumike kuhudumia maandalizi ya timu za Taifa.
 
Ili kuonyesha jambo hili limetuumiza roho zetu, Mh. Zitto na CHDEMA jitahidini sana kulirusha tukio hili kwa kulipia Star TV au ITV maana hawa jamaa wa serikali chovu ya CCM wanaingilia uhuru wa habari na wanatuficha mambo mengi. Tutapiga harambee ya kuchangia gharama za matangazo kwa njia ya Simu.
 
Kutokana na tukio la kinyama
lililotokea Arusha, sitaweza kusoma
hotuba ya Bajeti Kivuli Bungeni.
Wabunge wote wa CHADEMA
tunaenda Arusha kuomboleza,
kutafakari na kuwapa moyo
watanzania wenzetu. Kufuatia
matokeo ya mchezo wa leo dhidi ya
Ivory Coast, nimeona niwamegee
kile ningesema kuhusu Michezo.
Soma natafakari.
MAENDELEO YA MICHEZO
Mheshimiwa Spika, maendeleo
mazuri ya michezo katika taifa
lolote, ni utambulisho mzuri wa
taifa hilo katika mataifa mengine
kutokana na ushirikiano wa
kimichezo na mataifa hayo. Pamoja
na mambo mengine, michezo katika
nchi yetu inaweza kutumika
kutengeneza fursa za kiuchumi kwa
kuitangaza nchi yetu duniani katika
sekta za utalii na uwekezaji. Ukiacha
mbali suala la manufaa ya kiuchumi
yanayoweza kupatikana kupitia
michezo, michezo pia inawajengea
vijana wetu afya na hivyo kuwa na
taifa la watu wakakamavu. Kwa
upande mwingine, michezo pia ni
ajira. Inasikitisha kwamba katika
hotuba nzima ya Waziri wa Fedha,
hapakuwa na mpango wowote wa
kukuza michezo hapa nchini bila
hata kujali kwamba timu yetu ya
Taifa ya Mpira wa Miguu ipo katika
nafasi nzuri sana hivi sasa kuliko
wakati mwingine wowote katika
kuweza kufuzu kucheza fainali za
kombe la Dunia mwakani.
Mheshimiwa Spika, Kamati ya
Bunge ya Maendeleo ya Jamii katika
barua yake ya tarehe 5/4/2013
iliomba Kamati ya Bajeti kuangalia
namna ya kusaidia kupata fedha za
kujenga michezo na hasa kusaidia
Taifa Stars katika juhudi zake za
kuelekea kufuzu kwenye michuano
ya kombe la Dunia huko Brazil.
Hata hivyo Wizara ya Fedha
haikutoa hata senti tano kwa ajili
hiyo. Kamwe hatuwezi kufanikiwa
kwenye michezo bila kuwekeza na
kutegemea juhudi za dharura za
kamati za kusaidia ushindi. Tukitaka
tung’ae kwenye michezo ni lazima
tuwekeze sana na kuwekeza ni
gharama, gharama ambayo
thamani yake ni kubwa sana kwa
nchi.
Mheshimiwa Spika, licha ya
michezo kuliingizia taifa mapato
kupitia asilimia 18 ya Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT)
inayotokana na viingilio katika
michezo mbalimbali, hakuna
uwekezaji wowote wa maana
uliofanyika kwenye michezo jambo
ambalo ni hatari kwa uhai na
maendeleo ya michezo hapa nchini.
Aidha hakuna mipango madhubuti
ya muda mrefu kuhusu maendeleo
ya michezo hapa nchini.
Kutowepo kwa mipango madhubuti
na ya muda mrefu,
kumeshababisha timu zetu kufanya
vibaya katika mashindano mengi ya
kimataifa na hivyo kulifanya taifa
letu lionekane kuwa ni taifa dhaifu
au kichwa cha mwendawazimu
kama alivyopata kusema Rais
Mstaafu was Awamu ya Pili, Alhaji
Ali Hassan Mwinyi. Kambi Rasmi ya
Upinzani, inatoa angalizo kwa
Serikali kwamba, kamwe hatuwezi
kufanikiwa katika michezo kwa
mipango ya kukurupuka. Aidha ni
aibu kwa Serikali kukusanya kodi
kutokana na michezo, halafu vijana
wetu wanakosa fedha ya nauli
kwenda nchi nyingine kwa
mashindano ya michezo mpaka
wafanye harambee ya kukusanya
fedha kwa wahisani. Hivyo, Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni
inayoongozwa na CHADEMA
inapendekeza mambo yafuatayo
yafanyike ili kunusuru tasnia ya
michezo hapa nchini;
1. Timu yoyote itakayowakilisha
taifa katika mashindano yoyote ya
kimichezo igharamiwe na Serikali
kwa asilimia 100.
2. Viwanja vyote vya Michezo hapa
nchini viundiwe Wakala wa Serikali,
Wakala wa maendeleo ya michezo
(Sports Development Agency).
Wakala huo uwe na majukumu ya
kujenga viwanja vipya na
kusimamia viwanja hivyo kwa niaba
ya Serikali. Viwanja vyote vya
michezo vilivyoporwa na CCM kama
Lake Tanganyika – Kigoma, Ali
Hasan Mwinyi - Tabora, Kirumba –
Mwanza, Maji Maji – Songea nk
virejeshwe Serikalini mara moja
chini ya Wakala wa Viwanja vya
Michezo. Wakala pia ujenge
academies za michezo maeneo
kama vile Mbeya, Tanga, Mtwara,
Mwanza, Manyara na Dar es
Salaam ili kukuza vipaji vya watoto
na vijana.
3. Mashirika yote ya Umma, hasa
mashirika makubwa yawe na timu
za michezo. Ushauri uliotolewa na
IMF na Benki ya Dunia dhidi ya
Mashirika ya Umma kuwa na timu
ulikuwa ushauri usio wa maana.
Wenzetu Uganda kwa mfano,
Mamlaka ya Mapato Uganda (URA)
wana timu katika ligi Kuu, ambayo
ni moja ya timu mahiri katika
ukanda huu wa bara la Afrika.
4. Serikali ianzishe Mfuko Maalum
wa Michezo (Sports Fund). Pia,
Serikali ianzishe Kodi ya Maendeleo
ya Michezo (Sports Development
Levy). Kodi hii ipatikane kama
ifuatavyo: Kodi ya Ongezeko la
Thamani (VAT) ya asilimia 18
iliyokuwa ikikatwa kwenye viingilio
katika michezo mbalimbali
iondolewe na badala yake kiasi
hichohicho kiingizwe kwenye Mfuko
wa Michezo (Sports Fund)
utakaoanzishwa.
5. Matumizi ya Mfuko wa michezo
yawe kama ifuatavyo:
i. Asilimia 50 ya fedha
zitakazokusanywa zitumike kujenga
miundombinu ya michezo (Sports
Infrastructure) kupitia kwa Wakala
wa Maendeleo ya Michezo na
Academies.
ii. Asilimia 50 inayosalia itumike
kuhudumia maandalizi ya timu za
Taifa.
 
Uamuzi wa busara sana. Serikali ya ccm inatupeleka ktk machafuko!!! Hlf wanajifanya wapenda amani!
 
Bomu la kanisani Spika alijifanya eti kahudhunika sana na kuteua timu ya kuongozana nayo kwa ndege ya serikali kwenda kutoa pole. Najua hilo haliwezi kufanyika abadani kwa tukio hili. Nyie wabunge wa Chadema chukueni Basi muende wote na njiani muwe mnatoa salamu za yanayojiri ndani ya nchi yetu kwa sasa. Nina hakika mtapokelewa kwa moyo wa upendo na waTz kila mtakapo pita.
 
United we shall strive, Nimeipenda hiuo Kamanda Zitto. Katibuni A Town, huu unyama wa srrikali ya ccm unaelekea mwisho.

Ccm ilizaliwa Arushs, Azimio lilizaliwa Arudha, na byote vimakwrnda kufia A Town
 
Bomu la kanisani Spika alijifanya eti kahudhunika sana na kuteua timu ya kuongozana nayo kwa ndege ya serikali kwenda kutoa pole. Najua hilo haliwezi kufanyika abadani kwa tukio hili. Nyie wabunge wa Chadema chukueni Basi muende wote na njiani muwe mnatoa salamu za yanayojiri ndani ya nchi yetu kwa sasa. Nina hakika mtapokelewa kwa moyo wa upendo na waTz kila mtakapo pita.

Mgamba kwa jinsi wameamua jivua sura na walivyo na haraka ya kuzindua by surprise Nduli wao watakwenda walipua njiani wasem ni ajali au walipita ktk kambi ya CUF na kuanza siasa raia wakawaua.
 
Wabunge wa CHADEMA wamesema hawatahudhuria vikao vya bunge. Tafsiri yangu ni kuwa CHADEMA KWANZA UTAIFA BAADAYE. Arusha ina mbunge wake na viongozi wake.iweje wabungu wote wa kambi rasmi ya upinzania wasiwakilishe wananchi wao? Kwa nini mlipuko umetokea baada ya MBOWE KUONDOKA. Arranged!!.
 
wabunge wa chadema wamesema hawatahudhuria vikao vya bunge. Tafsiri yangu ni kuwa CHADEMA KWANZA UTAIFA BAADAYE. Arusha ina mbunge wake na viongozi wake.iweje wabungu wote wa kambi rasmi ya upinzania wasiwakilishe wananchi wao? Kwa nini mlipuko umetokea baada ya MBOWE KUONDOKA. Arranged!!.

Naamini una shida kubwa kichwani! Hivi unaelewa nini kilijiri kwenye tukio la mlipuko mkutanoni au unajisemea tu, ili mradi uwafurahishe MABWANA zako?

Mbona huulizi Wabunge wa MAGAMBA wanao toroka vikao vya bunge au wanao lala ndani ya Bunge? Si afadhali hao wa KUB walio amua kwenda kwenye mazishi kuliko wa kwenu ambao wamegeuka kuwa watetezi wa serikali badala ya kuwatetea wananchi!!!

Kamuambie aliye kutuma kwamba huko ulipo nituma ni kugumu. Kuna GT na sio vilaza kama nyie!!

SHY AWAY!!!
 
wabunge wa chadema wamesema hawatahudhuria vikao vya bunge. Tafsiri yangu ni kuwa CHADEMA KWANZA UTAIFA BAADAYE. Arusha ina mbunge wake na viongozi wake.iweje wabungu wote wa kambi rasmi ya upinzania wasiwakilishe wananchi wao? Kwa nini mlipuko umetokea baada ya MBOWE KUONDOKA. Arranged!!.
Yess! Arranged by mwigulu nchemba
 
Ili kuonyesha jambo hili limetuumiza roho zetu, Mh. Zitto na CHDEMA jitahidini sana kulirusha tukio hili kwa kulipia Star TV au ITV maana hawa jamaa wa serikali chovu ya CCM wanaingilia uhuru wa habari na wanatuficha mambo mengi. Tutapiga harambee ya kuchangia gharama za matangazo kwa njia ya Simu.

wazo zuri
 
MUNGU awatangulie MAKAMANDA wote katika safari yao ya Arusha.
 
Back
Top Bottom