Independent-Mind
JF-Expert Member
- Mar 10, 2015
- 712
- 207
ZZK katika ubora wake,eti bado kuna jamaa anaandika "Mnafiki@work",we unaipenda Tanzania au Chadema?
Umenifurahisha sana hapa, watu wanaumia moyoni tu
BAdo wapo kwenye hizi stage, wakivuka hizo utawaona tu hapa.
First they ignore you, then they ridicule you, then they fight you, and then you win.
Mahatma Gandhi
Wamevuka stage ya kwanza ya kum-ignore, ndio maana wanamfuatilia kila anapopita.
Saizi wapo kwenye stage ya pili,kumkashifu na kumzomea,
Kisha Zitto atafight back kwa kuendelea kusimama na hoja zenye nguvu,kushinda ubunge, kuendelea kuwa kinara wa hoja zenye maslahi ya taifa, kupambana sana na serikali bungeni.
Baada ya hapo hawa hawa, watasalimu amri na kukukubali kuwa alionewa, watampa ushindi.
Mi nasubiri tamko la Tundu Lisu huyu Zitto ni serekali hiyohiyo
Ni kichekesho na Serikali kuahidi kwa wazanzibari kuwa mafuta na gesi sio suala la Muungano halafu inatunga sheria za mafuta na gesi za kutumika Zanzibar. Miswada hii haikufikiriwa vizuri na hivyo iondolewe.
Muswada wa mafuta na gesi Asilia hauzingatii haki za wananchi. Imerundika mamlaka kwa Waziri wa Nishati na Madini na haki ya wananchi kushiriki na kutoa ruhusa utafutaji na uchimbaji haikuainishwa kwenye sheria. Chama cha ACT Wazalendo kinataka haki hii iwepo kwenye sheria.
Haki ya ' free prior informed consent ' ni suluhisho la migogoro kati ya wananchi na wawekezaji.
Muswada wa mapato ya mafuta na gesi imeandikwa haraka haraka na umeacha kabisa kushughulikia suala la mgawo wa mapato ya mrahaba kwa maeneo yenye utajiri huo.
Kwa miaka mingi tumekuwa tukipendekeza kuwa sehemu ya mapato, hasa mapato kutoka kwenye mirahaba ibaki kwenye wilaya zenye rasilimali.
Muswada huu umekwepa eneo hilo na litaleta mgogoro mkubwa kwenye nchi yetu. Hivi sasa wananchi wanaotoka kwenye maeneo yenye Dhahabu wanapata mgawo kutoka tozo za halmashauri.
Muswada huu upo kimya eneo hilo na hivyo kukosesha mikoa kama Mtwara chanzo muhimu cha mapato.
Muswada huu ukienda bungeni bila kupata maoni ya watu wa Kusini itakuwa sio haki. Ni vema kuondoa muswada huu bungeni ili kupata muda wa kutosha wa kupata maoni ya wananchi.
Wananchi wa Mtwara, chama cha ACT Wazalendo ndio chama pekee cha siasa hapa nchini ambacho kimeweka wazi sera zake kuhusu utajiri wa Maliasili ya nchi.
Sera hizo zimetamkwa ndani ya Azimio la Tabora lililozinduliwa tarehe 13 Juni 2015 mjini Tabora.
Azimio lina lengo la kuhuisha Azimio la Arusha ili kujenga Tanzania ya watu walio sawa na wananchi kumiliki uchumi wao wenyewe.
Tumewaletea chama chenu, mkipokee na kukilea. Chama cha Wanyonge chenye misingi imara na shabaha ya kuwakomboa watanzania kiuchumi.
Asante sana
Zitto Kabwe
Kiongozi wa ACT Wazalendo
Huyo Tundu Lisu unayemkashifu ndio tishio la vibaraka kama nyie na hiyo serikali ya kijambazi na kifisadi mnayoikumbatia. Kosa lake kubwa ni kwamba ahongeki kama huyo Zitto anayefikiri anafahamu kila kitu.Tundu lisu hana uwezo wa kuongelea mambo ya kitaalam kama hayo! Tundu Lisu ni mropokwaji tu. Kwa hiyo utasubiri sana.
Tatizo mnapenda kuangalia na kutaja wanayofanana tu bila kutaja wanayotofautiana,Tofauti yao ni kuwa ZZK is by far very capable,na hiyo ndio silaha yake,so unachokitegemea kimtokee utasubiri sana.Mimi nadhani ni vema Zito akaelewa kuwa uwezekano wa kurudia enzi zake za umaarufu wa kisiasa kamwe haziwezikurudi.asifikiri Mrema alipenda kuisha hivi ni kwamba jamii huangalia kwa makini mwenendo wa mwanasiasa tapeli.Nasikitika kukuambia nawe uko njia hiyo hiyo ya Mrema
ha ha ha umenifurahisha sana bora mfia nchi kuliko chamaHaka kajamaa tumekafujuza kameanzisha chama chake bado kanatusumbua tu. Dawa ni kumzomea kwenye mikutano yake ili asisikilizwe maana ukikasikiliza tu, ubavicha unakutoka.
Sijawahi kumuamini zitto asilani sitomuamini kiyama
Mimi nadhani ni vema Zito akaelewa kuwa uwezekano wa kurudia enzi zake za umaarufu wa kisiasa kamwe haziwezikurudi.asifikiri Mrema alipenda kuisha hivi ni kwamba jamii huangalia kwa makini mwenendo wa mwanasiasa tapeli.Nasikitika kukuambia nawe uko njia hiyo hiyo ya Mrema
Acheni unafiki nynyi chadema leo kafulila mbona hammwiti msaliti na mlifukuza ktk chama chenu but zitto ndo mnafik.zitto ni mjenga hoja pekee ambae hana mpinzani.
Mi nasubiri tamko la Tundu Lisu huyu Zitto ni serekali hiyohiyo
Tundu lisu hana uwezo wa kuongelea mambo ya kitaalam kama hayo! Tundu Lisu ni mropokwaji tu. Kwa hiyo utasubiri sana.
Zzk sikuwahi hata siku moja kukusifu humu jf lkn kwa hili tupo pamoja japo kuwa mimi ni kiongozi mkubwa tu ndani ya chadema!Penye ukweli wacha uongo ujitenge!