sentino2015
Senior Member
- Apr 9, 2015
- 176
- 30
Hahahahaha shibuda anajiita droga!!!kiboko cha Chadema
Mkuu politics has myriad of assumption given the circumstances ambazo zina shape the national or local politics. Siasa tu za regional integration kama EU zina impact kubwa sana jinsi mataifa yanavyotunga social policy zao kikubwa ni uwezo wa budget and monitoring mechanism of the policy ambazo nchi inawezaa jiamulia itatekeleza vipi.Erick Please wala usiende huko sio muundo wa Constitution unaounda mfumo bora wa ugawaji keki ya taifa. Kuwa Federal au Unitary haina maana yoyote ikiwa nchi zote duniani hazina mfumo mmoja na zimeweza kujenga mfumo bora wa ugawaji keki ya Taifa. Ni nchi za Kiafrika tu ndiko tunaendeshwa na ulafi kama mifisi bado tunagombania hadi mifupa.
Unaweka vitu viwili tofauti kwa pamoja kipimo cha mshahara wa mtu sehemu nyingi inategemea how easily the candidate can be replaced, time to gain necessary skills and value of the position to the organization mwishowe uwezo kima wanachoweza lipa bila kupata hasara na kile unachozalisha.Labda nikuulize hivi kwa nini wewe una mshahara mzuri kuliko wafanyakazi wengine? na kwa nini watu wote tusiwe na mshahara mmoja,sawa ili kutokuwa na ubaguz unaozungumzia. Ipo mikoa leo watumishi wa umma kama walimu/madaktari hawajalipwa mishahara wakati mikoa mingine wamelipwa!. Kuna usawa gani hapa unaozungumzia au dicrimination unayozungumzia inatokana na Mikoa tu au?
Malipo yako determined na income generated as well supply of labour, ndio maana huko juu nikasema kuna social value pia zinachangia how society view rights and people needs all together na hata hilo lazima lizangitie income.Hivi mtu nikisema kuwdo a na kijakazi anayefanya kazi nzito za nyumbani kwa malipo hafifu ni UTUMWA! Inakuwa namtetea Kijakazi au nataka wenye vijakazi wapungukiwe pato lao? Sasa huyu Kijakazi achangamkie fursa zipi ikiwa humuwezeshi? Kesho akianza kukuibia unasema mwizi wakati kwake yeye hizi ndizo fursa zilizokuwepo!. Hivi nikisema Madaktari wetu wanastahili mshahara zaidi ina maana nafanya Ubaguzi ama tunatakiwa kutazama demand/supply na kazi yao kuwa kipimo cha kustahili..
Mkuu hili swala ni pana na refu kwa sie tusiopenda kuandika sana kwakukwepa kutoa maelezo marefu ndio maana pia atuji pia kwenye lile jukwaa lenu. Hila siasa za magharibi iwe mfumo wowote ni value principles na moral za jamii hiyo zilipofikia ndio msukumo at any point wa sera(ukitaka kujua ni zipi angalia what sectoral pressure groups are advocating na kuchanganua economically given the national resources and spending priorities of policy area), muundo wake taifa lenyewe na sera ni kati ya income distribution and creating opportunities ambazo nyingi sasa zipo central right or central kutokana na uelewa wa jamii kwenye maamuzi ya siasa ambazo zime evolve over time (somo refu subiri kitabu changu inshallah kwa maelezo zaidi).Kifupi mkuu wangu nchi za magharibi walichotushinda sisi ni kuweza kuweka mfumo bora wa ugawaji keki ya Taifa na kila mahala panapokuwa na mfumo bora basi wananchi wake huwa na maisha bora zaidi na tumeona kote nhci za magharibi bila kujali wana muundo gani wa seirkali wamefanikiwa kugawama keki hii kwa kuweka fursa zaidi za uzalishaji sehemu zilizokuwa na maliasili.
Ndio maana nikakwambia kuwe na supporting industry sasa asilimia kubwa ya watalii wanaenda kilimanjaro na arusha ukajenge uwanja mtwara hao watalii utawaingiza vipi huko kunako husika. Isitoshe ata huo uwanja wa ndege ulijengwa strategically ku-serve both regions kutokana na uwezo wa serikari na vipaumbele vya muda huo maamuzi ya ku-invest ayafanyiki kwa mapenzi but returns and importance of particular investment.Ngoja nikuguse nyumbani...Jiulize hivi unafikiri kuwepo Uwanja wa Ndege Kilimanjaro haikusaidia zaidi uwekezaji katika Utalii na makuzi ya mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro!. was it a good Idea or bad? ikiwa mikoa mingine ilikuw ahaina hata kiwanja cha ndege ndogo..Kwa nini ilihitajika ku invest katika kiwanja kile. Je kama serikali isingejenga Uwanja ule unadhani hali ingekuwaje..
Business decisions have to consider a varietyof reason mimi sikukubaliana hata wale wasauzi walioamua kufunga virago kisa kulazimishwa kutumia bidhaa zinazolimwa hapa it does not make business na uwezi kuangalia strategy za watu people bear cost and profit margins si kingine kwa mbinu zao.Sasa iweje Mtwara wawe na gas lakini bandari ya kusafirisha gas hiyo ijengwe Dar! makao makuu ya shirika la gas hiyo liwe Dar, Account zake ziwe Dar, mzunguko wa fedha zote za mauzo ya Gas ya Mtwara yanafanyika Dar badala ya Mtwara. Na kosa kubwa mnalofanya vyama vya siasa Ni kuzungumzia jarida (heading) pasipo kutazama ndani kuna nini. Kuna jamaa mmoja jana kanambia hili ya kwamba sisi hamwe hatuzungumzii Content wala Context siku zote tunabishania Process na huishia. Hii ni kweli kabisa na naanza kuelewa ama kuwasoma vizuri zaidi Wadanganyika.
kwasababu kwa sasa Mtwara hakuna benki za mikopo au vipi mbona sielewi hoja yako, unataka serikari iwekeze vipi Mtwara kwa sasa unajuaje as things develop in the future kutokana na uwezo wa serikari aitawekeza Mtwara zaidi; leo serikari aina uwezo wa kufanya offshore exploration wewe unataka wawekeze Mtwara aisee.Hizo banki account ndio zingewawezesha wananchi wa Mtwara kuchukua mikopo wakafungua biashara, au hata wewe kuhamia Mtwara. Government expenditure, upatikanaji wa mitaji, matumizi na gharama za uzalishaji na huduma zinavyoongezeka ndivyo maendeleo ya wananchi yanavyozidi kupanda.
Mkuu sasa unavyosema social democratic values na mgao wa keki ya taifa unadhani ni nini? Sera bora ya afya inachukua hela chungumzima matter of fact kwa nchi kama uingereza 30% of annual budget inaishia huko na chanzo kikubwa cha government income ni taxes, ukienda kushoto zaidi kama Scandinavia kwenye better health policies much is allocated in the sector (at least wao wana utajiri wa mafuta na gesi). Kwa hivyo kugawana keki sio lazima uone barabara tu. All social policies cost money sasa inategemea vipaembele vya serikari ni sehemu gani na huko pia ndio namna ku share keki ya taifa na ndio mantiki ya social democratic universal income distribution policies.Tunachozungumzia hapa ni swala la mafuta na Policies za chama cha CCM kuhusiana mgao wa keki, hizi habari nyingine tuachane nazo kwanza.Maswala ya EU yanapanua tu wigo la utekelezaji ikiwa wataamua AFYA ni haki. Hii haiondoi ukweli kwamba sheria ni moja. Kama Uingereza imeamua pekee watatunga policies zao wao na ikikubaliwa EU kinachobadilika hapo ni upana wa mipaka tu (wigo) kwa sheira hiyo kutumika. Kama vile tukikubali ndoa ya Mashoga (Lol) katika Bunge la JMT basi inalazimika sheria hiyo itumike na Zanzibar. na zipo sheria zinazoweza tumika Bara zisitumike Zanzibar au kinyume, vivyo hivyo EU na nchi zenye muungano.
Uwe na kumbukumbu na unacho andika sio mimi niliesema upendeleo wa malipo za sehemu ni wewe ndio uliolileta, Isitoshe ebu nitajie nchi yoyote ya magharibi ambapo mineral resources policy inayonufaisha jimbo na ipo kwenye unitary constitution au sehemu yeyote ya federal constitution ambapo resources zimeelezwa ni mali ya federal state halafu kukawa na special regional favours kwa sababu tu ya kuwa na resources? Hapa si itaji kujua ukweli wa hoja yako kujua ni impossible especially on unitary states.Swala la Ubaguzi ujmelileta wewe, na sidhani kama hii ni Policy mahala popote kwa saabu nchi za magharibi wanatumia mtindo wa kunufaisha majimbo yenye maliasili hivyo kwa maneno yako ya mwanzo unadai hiyo ni dicrimination kwa sababu sisi ni Unitary Country. ndio maana nikakukatalia hoja yako kuwa Unitary haifanyi Policies ziwe mgawane sawa kwa sawa. Na ndio maana nikaweka mfano wa mishahara mbona haiko sawa!
Navyojua Mtwara kuna feasibility study ya bandari kuhusu kuunganisha nchi za kusini sasa ata kama unataka kufanya kitu na auna hela unategemea abracadabra ndio maana nilikuuliza unajuwa mipango yote ya maendeleo ya Mtwara ya muda mrefu.Sikusema Mtwara wajengewe Uwanja wa ndege ila nachosema ili Mtwara wafaidike na kuwepo mafuta, serikali inaweza jenga bandari kama ilivyojengwa uwanja wa ndege Kili italeta ajira. Serikali yao ya halmashauri pia waweze kukidhi mahitaji yao katika kuboresha wazingira yao kiuchumi. Kwa nini swala la maendeleo ya Mtwara wapangwe IKULU? Hizi Halmashauri zina kazi gani? kukusanya ushuru na kufagia mabarabara ya vumbi! na kwa nini Halmashauri zisiwe na mfuko wake katika kujiendeleza haswa wakiwa na vitu kama mafuta wasubiri mgao usiokuwa wa haki kutoka serikali kuu. Haya ndio ya Shinyanga wana Dhahabu lakini badrabara zote mbovu, mkoa hauna maji, umeme wa kukamatia halafu unategema kutakuwepo na uzalishaji wa ajira!..
Soma kwanza sheria ya gas na mafuta iliyopitishwa kama anaweza fanya chochote cha siri na anaweza kwepa thoughted contract models au kuna mtu anaweza fanya favour tena za kuipa serikari hasara za kishamba, again tuache kufikiri vitu ambavyo havipo kiuhalisia bali tu deal na facts zilizopo ndio siasa zenyewe hizo na jinsi maamuzi yanavyofikiriwa.Sisi wengine chale hutucheza tunapoona mizengwe ya serikali hii. Wee fikiria Mtwara yenye Gas na Mafuta, leo wamekuja mpa Contract tajiri mkubwa Afrika ambaye Utajiri wake umetokana na vitalu vya mafuta na gas.. Halafu tajiri huyu anapewa contract ya kujenga bandari yake binafsi. Mkuu 2+2 kamwe haiwezi kuwa 22, mwerevu atang'amua. Madudu kama haya ndio yanatakiwa kufanyiwa kazi kwa makini zaidi na kuhakikisha wananchi wanafaidika na maliasili hizi.
Pato la gesi lina baki hapahapa depending on the size of the well lakini serikari ni mnufaika wa kuanzia 50%-80% in additional to profit made taxes, terms and condition are to be reviewed once the investor has recouped his investment costs.Kama huelewi kwa nini mzungunguko wa fedha ama pato unaweza kujenga uwekezaji basi itakuwa kazi mpya kuzungumzia hili kwa sababu mkuu wangu hiyo fedha uloiweka benki kama akiba haikai katika sanduku bali hukopeshwa watu wengine wakaifanya mtaji wao. mzunguko huo ndio unaoendeleza watu na mikoa. Kama pato la Gas linakwenda banki za nje utanategemea wana Mtwara wataweza vipi kupata mikopo.
Nadhani somewhere kwenye thread I mentioned value ambazo taifa inasimamia na vitu gani inavipa kipaumbele hata UK could have opted for people to pay for hospital insurance ili wapate matibabu; lakini kuna swala la ambao hawana kazi wakiumwa je awana haki ya kupewa huduma za afya zenye kiwango? kwa hivyo inatafutwa mbinu nyingine ya ku-fund those services ili huduma hiyo itolewe kwa wote bila ya kubagua.Mahala popote penye better Health care kunatokana na matumizi bora za fedha za Umma, na lazima igharimu zaidi, kinachopishana ni aidha gharama hizo zichukuliwe na serikali ama na wananchi wenyewe na siri kubwa iliyopo ni uwezo wa kugharamia aidha wananchi maskini huwezi kutegemea wataweza kukabiri gharama kwa sababu Utajiri wa nchi sio lazima uwafikie wananchi walio wengi. Nigeria ni tajiri pengine nchi tajiri kuliko zote Afrika lakini standard ya maisha ya watu wake inaweza kuwa chini ya nchi kama Mauritius ambao hawana mafuta. Kwa hiyo siuo tu swala la health kuwa right au privilege inategemea na uwezo wa watu na mazingira yake kiuchumi.
Thanks for clarifications isipokuwa hoja ilikuwa hizo sheria zinasema sehemu husika zipendelewe kwenye makusanyo ama vipi? kama Zitto anavyo pendekeza.Ukienda Libya, Norway, Amerika au Canada swala la Mafuta na Gas hutungiwa sheria na Federal Government haijalishi kuwa serikali hiyo ni Unitary au Federal kwa sababu tofauti baina yao ni mgawanyo wa majukumu (power) katika majimbo na utekelezaji wa shughuli wa serikali hizo. Kwa hiyo sheria ya mapato ya gas na mafuta inaweza kuwa sawa katika aina serikali yoyote. Kwa hiyo Federal Government inapotunga sheria ya mapato inahusu nchi nzima, Leo Alberta wana mafuta, kesho yakivumbuliwa Quebec au Nova Scotia sheria itakayo tumika ni ile ile inayotumika Alberta.
Nimekusoma vizuri na ulichoashiria ni kwamba Zitto analeta siasa za Ubaguzi na ukaandika haya:- U
Wasn't it obvious jinsi gani anavyo himiza Mtwara wawachiwe sehemu ya mapato kwa sababu ya gesi kutoka huko; you know what na watu wa Dar waseme asilimia kadhaa ya kodi ibakie kwanza Dar wajiamulie kama wajengewe barabara na vitu vingine maana mapato ya kodi pia ni income ya serikari kwa mtaji huo si Dar saa hivi ingekuwa kama Jo'berg tu.nitary states do not discriminate all they do is foster regional advantages gesi inakuja wananchi wa sehemu hizo automatic wana fursa za kuchangamkia fursa za kiuchumi zinazo compliment uzalishaji wa gesi na huduma zake.
Ukishakuwa na akili za kibaguzi inakuwa ngumu kuona unachokisema ni kiasi gani cha asilimia ya sh100 ya kodi ya watu dar kwenye ongezeko la mafuta itachangia kwenye miradi ya umeme vijijini? Sasa unataka kusema wakazi wapo happy wao kupewa umeme wa kusuasua, hospitali zisizoridhisha, maji si ya uhakika, shule si bora, ajira bado tatizo, makazi ya kuishi na huduma zingine bado ni tatizo; loe kwanini wachangie sh 100 huko sijui vijijini Mtwara kupewa huo umeme wao unawuhusu nini.Ulichoshindwa kuelewa ni kwamba kuwezeshwa wananchi wa Mtwara haina maana pato lote la Gas na mafuta litapewa Mtwara isipokuwa Mtwara kama mkoa unapewa (ruzuku) juu ya pato la kodi katika matumizi ya serikali na halmashauri zake wakati huo huo Kitaifa mikoa yote ikifaidika Corporate tax za shirika hilo, kodi na ushuru wa jumla katika matumizi ya shrika hilo, mishahara nakadhalika.