Zitto Kabwe ndani ya Karatu

Zitto Kabwe ndani ya Karatu

acheni chuki binafsi wana JF, kubalini kuwa Zitto ana mchango mkubwa ndani ya CDM na nadhani ni yeye na Dr. Slaa ndio wanaoongoza kuifanya CDM leo iwe tishio. Nani atabisha.? Zitto ameleta hamasa kubwa kwa vijana kupenda CDM kuliko mwingine yeyote. Kama yeye ni pandikizi la CCM, kulikuwa na haja gani aijenge chadema wakati ilikuwa haijulikani.? Mapandikizi ni wale wanaodandia chama kikiwa kimeshakomaa. Zitto kajiunga na chama wakati ana miaka 16 na chama kilikuwa hakijulikani, na amekua nacho na ameshiriki kukijenga. Ni mpumbavu gani duniani apoteze muda wake kujenga nyumba halafu aanze kuibomoa? Mkubali msikubali, zitto ni jembe la chadema na hakuna wa kumtoa sababu hana hatia yeyote na ndio atakibeba chama 2015. Acheni kuwa na wivu na ubaguzi usio na msingi.
 
Hahahaa!molemo kuna siku hamjamfatilia?
Eti intelijensia?mna inteligensia ?
Hahahaa!wadanganyeni hao hao!
Mshumbusi au?
Nenda hata wewe mbona wewe ni mnafiki sana na kuwadi wa uzandiki si uwahi uende.
Sasa bado subili picha jioni utakimbia wewe.
Uamusho muna mambo yenu, CHADEMA hakuna ugomvi kama unavyodhani
hata ZZK alisema chama kikiona hawezi kwa sasa atakubaliana na uamuzi wa chama hapa fahamu kuwa ZZK atakuwa na miaka 39 mwaka 2015 umri ambao katiba haimruhusu kugombea urais labda katiba ibadilishwe
 
Zitto amewashika pabaya 2015,kama ni maumivu ya tumbo basi ni la kuhara lazima mkajisaidie ndio mpate nafuu mkibana yamejaa kwenye gwanda.

Kwi kwi kwi!
Zitto kweli jemedali.
Waangalie tu wasijisahau wakaingia choo cha kike.
 
Zitto haitaji Choppa wala kukodi mafuso kujaza watu katika mikutano kijana anakubalika.2015 lazima lengo litimie ingawa ni ngumu kumeza kwa wapika chuki.
 
acheni chuki binafsi wana JF, kubalini kuwa Zitto ana mchango mkubwa ndani ya CDM na nadhani ni yeye na Dr. Slaa ndio wanaoongoza kuifanya CDM leo iwe tishio. Nani atabisha.? Zitto ameleta hamasa kubwa kwa vijana kupenda CDM kuliko mwingine yeyote. Kama yeye ni pandikizi la CCM, kulikuwa na haja gani aijenge chadema wakati ilikuwa haijulikani.? Mapandikizi ni wale wanaodandia chama kikiwa kimeshakomaa. Zitto kajiunga na chama wakati ana miaka 16 na chama kilikuwa hakijulikani, na amekua nacho na ameshiriki kukijenga. Ni mpumbavu gani duniani apoteze muda wake kujenga nyumba halafu aanze kuibomoa? Mkubali msikubali, zitto ni jembe la chadema na hakuna wa kumtoa sababu hana hatia yeyote na ndio atakibeba chama 2015. Acheni kuwa na wivu na ubaguzi usio na msingi.
nakuunga mkono mkuu kwa kauli yako hii
zaidi tuanapaswa kusimamia kile ambacho mtu anakisema na siyo kutendea kazi hisia zetu ambazo % kumbwa huwa si za kweli
 
Zitto kazi anafanya wasiwasi wa watu unatokana na jinsi anavyotoa kauli zake mbalimbali bila kujua kuwa zitatafsiriwa kumchafua lakini pia kumgobanisha na viongozi wake wakuu. Ashukuru kuwa wana busara na wanajua jinsi ya kumchukulia, vinginevyo angeonekana mhaini na angenyang'anywa uanachama. Cha msingi Mh. Zitto apime kauli zake kabla ya kuzitoa kwa umma kwani siku uongozi wa Chama ukibadilika ataumia.
 
nakuunga mkono mkuu kwa kauli yako hii
zaidi tuanapaswa kusimamia kile ambacho mtu anakisema na siyo kutendea kazi hisia zetu ambazo % kumbwa huwa si za kweli

msijali katiba mpya itakuja na nafasi kibao za uraisi ,makamu wa kwanza wa rais ambayo itakuwa ni ya rais wa zanzibar,makamu wa pili wa rais itachukuliwa na rais wa tanganyika ,na nafasi ya rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania ,waziri mkuu na mawaziri watakuwa hawatokani na wabunge ,sasa kwa nafasi zote hizo .mnamshambulia Zito kwanini ,ni vema sasa basi tuwache kuamua mambo kwa hisia,
 
Zitto amewashika pabaya 2015,kama ni maumivu ya tumbo basi ni la kuhara lazima mkajisaidie ndio mpate nafuu mkibana yamejaa kwenye gwanda.

Interesting, kwamba Siasa zimefikia hatua hii. Ati kauli hizi ndizo zitampeleka Rais madarakani.Huu urais sasa umekuwa urahisi. Bahati nzuri mnaishi kwa predictions wakati muda wenyewe upo na utaongea
 
msijali katiba mpya itakuja na nafasi kibao za uraisi ,makamu wa kwanza wa rais ambayo itakuwa ni ya rais wa zanzibar,makamu wa pili wa rais itachukuliwa na rais wa tanganyika ,na nafasi ya rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania ,waziri mkuu na mawaziri watakuwa hawatokani na wabunge ,sasa kwa nafasi zote hizo .mnamshambulia Zito kwanini ,ni vema sasa basi tuwache kuamua mambo kwa hisia,
Sijui wanao mshambulia wana maana gani

kumbuka kuwa lazima katika mpya ieleze uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa/mseto
 
Safi sana kamanda hakuna kulala mpaka kieleweke

MH:NAIBU KATIBU MKUU NA MBUNGE WA KIGOMA KASKAZINI NDUGU ZITTO ZUBERI KABWE AMEMALIZA MKUTANO WAKE ALIOUFANYA HUKO KARATU KATA YA ENDAMARARIEK AMBAYO INAPATIKANA MAENEO YA VIJINI.
MKUTANO WAKE ULIKUWA MKUBWA SANA,UMATI WA WATU ULIKUWA NI WAHALI YA JUU SANA TOFAUTI NA MTU YEYOTE AMBAYE ANGEFIKIRIA UPATIKANAJI WATU.

ZILIKUWA NI SHANGWE NA KELELE ZA PEOPLES POWER HUKU WANANCHI WALIOWENGI WAKITAMANI KUMSHIKA AU KUMGUSA MBUNGE WAO(CHADEMA) MH:ZITTO KABWE.

KATIKA MKUTANO ULE MH:KABWE AKUTANA NA CHANGAMOTO KUBWA SANA YA TATIZO LA MAJI KWA WANACHI WA KATA ILE NA MAENEO YA JIRANI,PIA HUDUMA ZA AFYA NI TATIZO KUBWA.
AKIHUTUBIA MAELFU YA WANANCHI WALIOJITOKEZA KWENYE MKUTANO HUO,MH ZITTO AMEELEZA MAMBO MBALIMBALI YANAYOLIHUSU TAIFA LETU,AMEZUNGUMZIA SWALA LA UFISADI,AMEZUNGUMZIA NAFASI YA HALMASHAURI NA MAENDELEO YA WILAYA YA KARATU,AMEZUNGUMZIA NAFASI YA KILA MWANAKARATU KUIUNGA MKONO CHADEMA ILI KUPATA UKOMBOZI WA KWELI KATIKA NCHI HII

SEHEMU KUBWA YA WANANCHI WA KARATU WALIKUWA NA OMBI KWA MH:ZITTO LA KWENDA KUWAFIKISHIA MATATIZO YAO SEHEMU HUSIKA HASA JUU YA UPATIKANAJI WA MAJI.

KESHO TAR:30/09/2012 MH;ZITTO ATAFANYA MKUTANO MKUBWA WA HADHARA KARATU MJINI IKIWA NI MWENDELEZO WA MIKUTANO YAKE YA KUJENGA NA KUIMARISHA CHAMA NDANI YA NCHI.
HIVYO WANACHADEMA,WANANCHI,WANAKARATU WOTE MNAOMBWA KUHUDHURIA KWA WINGI SANA KWENYE MKUTANO HUO,KWANI MBUNGE WENU WA CHADEMA TAKUWA NA NAFASI KUBWA YA KUONGEA NA WANANCHI WAKE JUU YA MUSTAKABARI WA TAIFA LETU.
NAWASILISHA
(karatu)
 
Kwahiyo alikwenda kusikiliza kero za wananchi? si wana mbunge wao ambaye ni moja ya jukumu lake kusikiliza kero na kuwakilisha?
Tunaomba alichozungumza na nukuu kabisa ili tuone mantiki ya safari yake.

Kila utakacholetewa hapa jamvini kuhusu hotuba ya Zitto Karatu hakitakidhi kiu yako maana hamu yako wewe ni kuona Zitto amezungumzia urais au kurusha madongo dhidi ya CDM. Utasubili hadi uwe mbili. Hiyo ndiyo CDM hautaona siasa za namna hiyo.
 
wewe shamba boi na tarishi wa Dr. Slaa tuliza akili hiyo ndio demokrasia; hata wewe kama unajiweza tangaza nia yako ya kugombea uraisi; kumbe na Chadema mna intelijensia asante sana kutujuza; niliwahi kuambiwa intelijensia yenu inafanyakazi kama mganga wa kienyeji; kuwekeni makini msije makijita vidole vya macho.

Chama
Gongo la mboto DSM

Matusi ni hatua ya mwisho kabisa kwenye ujenzi na utetezi wa hoja unayoisimamia.Mara nyingi hutumiwa na mtu aliyefirisika na kuparaganyika kimawazo. Kwa maneno mengine hatuwezi kutarajia hoja ya maana tena kutoka kwako.
 
Zitto haitaji Choppa wala kukodi mafuso kujaza watu katika mikutano kijana anakubalika.2015 lazima lengo litimie ingawa ni ngumu kumeza kwa wapika chuki.

Zitto ni jeshi la mtu mmoja!
 
Hahahaa!molemo kuna siku hamjamfatilia?
Eti intelijensia?mna inteligensia ?
Hahahaa!wadanganyeni hao hao!
Mshumbusi au?
Nenda hata wewe mbona wewe ni mnafiki sana na kuwadi wa uzandiki si uwahi uende.
Sasa bado subili picha jioni utakimbia wewe.

Jinsi ulivyoandika nalazimika kuamini wewe ni Uzao wa Ismaili uliotokana na Uzao wa Kijakazi. Huna lolote zaidi ya mlengo wa Kidini Kidini tu. ZZK hataweza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Isitoshe huu sio Wakati wa kuongelea nafasi ya Uraisi badala yake tuwekeze fikra zetu kwenye kukijenga Chama. Sehemu nyingi sana CHADEMA hakijafika. Huu ni wakati wa kutoa elimu ya Uraia kwa Watanzania wote ili wazijue haki zao ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha vijana kujua umuhimu wa kupiga kura na kuwa tayari kuzilinda kwa gharama YEYOTE. Bila kutoa elimu ya kutosha kwa wapiga kura hasa vijana ambao ndo hazina ya mwaka 2015; hatuwezi kuishinda CCM.

Kinachomsukuma ZZK kuongerea nafasi ya Uraisi Wakati huu ni kuwafurahisha MABWANA waliomtuma kukivurunga CHADEMA. Njaa kitu kibaya sana, ZZK anaendekeza njaa sana na ndo maana anayasema haya anayoyasema. Aende kujenga Chama vijijini Tanzania bado Kubwa sana. Makete hajawahi fika na sidhani Kama anao huo mpango wa kwenda huko. Naamini kabisa kilichompeleka karatu si kukijengnga Chama. Kapeleka umbea na kupima upepo wa Kauli yake ya Kigoma.

Ukweli usiopingika, ZZK ni pandikizi la watu wenye nia mbaya ya mapinduzi ya kweli hapa NCHINI kwetu Tanzania. Ni mmoja wa magugu shambani inafaa tulipalilie shamba letu na kuyaondoa magugu yote tubakie na mimea mizuri tu. Mungu ibariki Tanzania ili Tanzania mpya na yenye matumaini mapya ipatikane.
 
Karatu tena?anyway fine ningefurahi zaidi kama angelikuwa Unguja na Pemba,na kwa bara nigeffurahi zaidi kama angelikwenda Bagamoyo hapo nadhani kweli angelikuwa amekwenda kujenga chama,huko labda kukiimarisha,si aendekwanNdugai pale Kongwa?au aende kwa Lowasa .Fine tunamkia ujenzi mwema.
 
Mimi nampenda zitto sana hasa kwenye siasa zake,Lakini kwa matusi haya ndhani umeharibu kila kitu.Zitto kweli ni Kiongozi Bora ndani ya chadema.

samahani kama nimekukwaza kwa maneno niliyoyasema,(wajinga,mabwege)sikua na nia ya kumkwaza yeyote yule,ila hao wanao muita ZITTO mamluki nafikiri wametumia hasira na jazba kwani katika maoni yake ZITTO hakua na lolote baya kwani ametumia haki yake kidemokrasia kabisa,sasa watu waeleweshwe kua atatoke mwingine na atapeleka jina lake kwenye kamati kuu na kura zitapigwa na atakaepata kura nyingi ndie atakae kua mgombea wetu.watu wasiwe na hofu na kamanda ZITTO sio mrahisi kama wanavyodhani,kwanza waelewe historia yake kua ni muasisi,mkongwe kuliko wadhaniavyo.
 
Mimi nafikiri kauli ya zitto kuhusu kugombea urais haina shida kabisa ni ya kawaida mno, tatizo kidogo ninaloliona ni la kwenda Karatu kuimarisha chama, mbona kuna maeneo mengi tu chama bado hakijaimarika? Hata hivyo, sitafikia hitimisho lolote huenda kulikuwa na kazi maalumu Karatu ambayo alikwenda kuifanya ambayo sisi hapa jamvini hatuwezi kuijua kwa urahisi. Naomba wanaomtuhumu Zitto wajaribu kupanua mawazo zaidi na kumwelewa vizuri kijana huyu, kwa hakika sidhani kama ni mbaya hivyo kwa chama ila kama zipo dalili kweli za kukihujumu basi mikakati iwekwe kwa makini ya kuhakikisha haleti madhara ila anaendelea kukiimarisha zaidi.
 
Hivi Cheo cha uraisi chadema ni haki ya kudumu ya Mchungaji Slaa pekee au ni haki ya kila mwanachadema ??

Ni haki ya kila mwanachadema lakini tunataka agombee ambaye tunajua ana malengo gani ya kuwa rais. Kwani Dr. Slaa aligombea mara ngapi?
 
Umenena vema mkuu, huu si wakati wa kujadili urais wa zzk bali kujenga cdm, go on kamanda zzk. Mabadiliko lazima.
 
Back
Top Bottom