Zitto Kabwe Na Ajenda Yake Moja

Sumaku

Member
Feb 17, 2009
53
1
Na Andrew Mushi

KATIKA kipindi cha muda mfupi wa miaka minne iliyopita, Zito Kabwe amefanya mambo makubwa sana katika nyanja ya siasa za Tanzania. Ni mambo watu wachache sana wanaweza kuyafanya.

Katika utafiti wa Redet wa mwaka 2006, Zitto alikuwa anamfuatia rais Kikwete kwa umaarufu kwa wanasiasa hapa Tanzania. Unapouwa na kijana mdogo kama Zitto, ambaye jina lake likitajwa, inabidi watu wakae kimya kwanza kusikia kuna jipya gani, ni vizuri kufanya tafakuri ya hii hazina tulio nayo.

Kwa wale wanaofahamu watu wenye umaarufu kama Zitto, tunawaita ‘taasisi' (institution). Kwa hapa Afrika, watu tunowahesabu ni taasisi ni kama Mwalimu Nyerere, Mandela, Kwame Nkurumah, na Raila Odinga kwa uchache. Kwa kawaida taasisi zina nafasi kubwa sana ya kutoa mwelekeo wa mambo.

Nia kubwa ya kumleta Zitto kama mada hapa, ni ili kuweza kujifunza mikakati na mbinu mbalimbali anayotumia kuweza kuleta mabadiliko hapa nchini mwetu. Kwa hiyo, Zitto tunamtumia kama shule, pia ni njia ya kuweka kumbukumbu kwa ajili ya vizazi vijavyo. Hapa wanasiasa ngazi ya taifa hadi mtaa, wanaharakati, wakulima, wafanyakazi, washika dini na hata machinga wanaweza kujifunza mengi toka kwa Zitto na kuyaingiza katika mikakati yao ya kujikomboa.

Wana-Kigoma Kaskazini waliona hii hazina iliyo ndani ya Zitto mapema na ndio maana mwaka 2005, Zitto akiwa na umri wa miaka 29 tu, wakamchagua kuwa Mbunge wao. Zitto kazaliwa 1976. Hawakujali umri wake wala chama chake cha upinzani-Chadema. Mpaka leo hii, jimbo lake linachekelea kwa mafanikio mengi walioyapata. Lakini pia, Watanzania wamebaidi maana ile kasi ya madini yetu kuchimbwa na sisi kuambulia asilimia tatu tu imekutana na matuta, inasuasua.

Mkakati mkubwa sana wa Zitto ambao amekuwa akiutumia tangu ameingia bungeni ni wa kuwa na hoja moja na kuisimamia siku zote. Hoja yake imekuwa ni madini au kwa lugha ya ujumla rasilimali za taifa. Kila akiongea yeye anaongelea rasilimali za taifa. Anataka kila Mtanzania afaidike na hizi rasilimali na si makampuni machache ya Ulaya, Marekani, na Afrika Kusini pamoja na wachache wazawa. Imekuwa rahisi kujua Zitto anasimamia nini.

Ukitaka kujua Zitto anajua anachofanya, hoja ya mafisadi iliyoletwa na Willbroad Slaa, Mbunge mwenzake wa Chadema, hajawahi kuhangaika nayo sana. Maana anajua akihamia huko, je ya kwake nani ataisimamia.

Ili kuweza kusimamia hoja zake vizuri anafanya sana utafiti kujua undani wa hilo jambo. Agosti 2007 wakati wa bunge la bajeti, alisimamishwa kuhudhuria bunge kwa madai ya kuwa alidanganya Bunge kwa kusema Waziri wa Madini na Nishati wa wakati huo, Nazir Karamagi alisaini mkataba wa madini hotelini London, Uingereza kinyume na taratibu za nchi.

Miezi mitatu baada ya kusimamishwa, Rais Kikwete akamteua kuwa mmoja wa wajumbe wa kamati aliyounda ya kupitia upya mikataba ya madini. Ingekuwa Zitto alidanganya Bunge, isingekuwa rahisi, kwa Rais kumteua katika hii kamati. Rais Kikwete alikuwa mbele hatua moja zaidi ya Bunge. Kilichomsaidia Zitto, alikuwa amefanya utafiti na alichosema ndio maana wabunge walioshauri asimamishwe, wakaoneka wao ndio hawajui kinachoendelea.

Zitto anaongea kile kinachowagusa wanachi wengi. Mfano, suala la madini na rasilimali nyingine linamkera kila mtu. Tofauti na wanasiasa wengine wanaongelea vitu ambavyo haviwagusi wananchi. Ni mara ngapi tumesikia, wabunge akina ‘naunga hoja mkono ndugu spika' wakishabikia kampuni za wawekezaji wa nje, wakati wananchi hawataki. Zitto yeye anapinga haya makampuni kwa nguvu zote.

Kuna wanasiasa waliibuka kuwa maarufu, ila pale walipoanza kuongea mambo ambayo wananchi hawataki kusikia walizimika kama moto wa kifuu .Mfano, Mtikila ameshikilia sana hoja ya Utanganyika, hiyo haina uhusiano wa moja kwa moja na wananchi. Mrema yeye kila akiongea ni yeye kuhujumiwa, hana wananchi wala hata chama chake.

Nguvu nyingine ya Zitto ni kusimamia anachokijua na kukiamini kwa nguvu zote. Halegezi msimamo.Mwaka 2007 alipodaiwa amedanganya bunge alisimamia msimamo wake, hakutereka, ingekuwa hana msimamo, angekimbilia kuomba msamaha.

Kitu kingine ambacho tunaweza kujifunza ni kuweka msimamo wetu wazi. Mwishoni mwa 2006 Zitto alisema akimaliza kipindi chake cha ubunge wa miaka mitano hapo 2010, hatagombea tena, Mwaka 2007 akarudia tena huo msimamo wake. Mwaka huu pia amesisitiza hilo tena. Niambie ni mwanasiasa gani anaweka msimamo wake wazi kama yeye. Tunaomjua Zitto, mwakani hatakuwa katika mbio za ubunge.

Nihitimishe makala hii kwa kukumbushia sifa tano kuu zinazomfanya Zitto ang'ae na kupaa kuliko wanasiasa wengi hapa Tanzania. Zitto ana ajenda moja tu, hashiki mambo mengi kwa wakati mmoja. Anafanya utafiti. Tatu Zitto ni mtu wa msimamo, nne anaongelea vitu vinavyogusa wananchi moja kwa moja. Mwisho, anaweka msimamo wake wazi.

amushi1@yahoo.com

CHANZO: KwanzaJamii.com
 
'the real ZITTO i know' is not existing!am sorry to say this

the zitto u're talking youngman SHOULD GO TO HELL
thw zitto who was implicated in the final DOWANS' DEAL SHOULD GO TO HELL

Geoff,
Maneno yako makali sana. Punguza munkari ndugu yangu japo mimi pia nilishapoteza matumaini yangu kwa Zitto through the so called Dowans deal. Wanasiasa wetu wananunulika kirahisi tu pamoja na ujuaji wao wa kupangilia maneno yenye ushawishi. Watu kama Nyerere, Mandela etc walikuwa na misimamo ambayo waliweza kuisimamia ndo maana umaarufu wao haukuchujuka.
 
Zitto binadamu kama watu wengine. Tatizo watu mnawarate juu sana wasipo live up to those expectations ndiyo mnakuwa disappointed. Zitto ni Zitto sasa mliomfanya as if yeye ndiye "The Chosen One" ndiyo mnaishia kuhuzunika na kusema Zitto why? Muoneni tu binadamu kama wengine. Let him exceed the odds na siyo kumkweza hata kabla hajafanya hicho kitu. Let him do him.
 
'the real ZITTO i know' is not existing!am sorry to say this

the zitto u're talking youngman SHOULD GO TO HELL
thw zitto who was implicated in the final DOWANS' DEAL SHOULD GO TO HELL
Whatch out maaan! Zitto ni Iconic.
 
CCM hawatachelewa kumcorrupt ili waue CHADEMA.but then again,sidhani kama Zitto ni mtu wa kununuliwa kirahisi.
 
JIMBONI KWAKE KAJENGA SHULE NGAPI?MAJI,VITUO VYA AFYA N.K naomba Mwandishi wa Zitto aende jimbo la MKONO au kwa LUKUVI ISMANI-IRINGA.
 
'the real ZITTO i know' is not existing!am sorry to say this

the zitto u're talking youngman SHOULD GO TO HELL
thw zitto who was implicated in the final DOWANS' DEAL SHOULD GO TO HELL

Geoff, Acha hizo kwani wewe mpaka sasa hivi umeifanyia nini nchi yako???
 
JIMBONI KWAKE KAJENGA SHULE NGAPI?MAJI,VITUO VYA AFYA N.K naomba Mwandishi wa Zitto aende jimbo la MKONO au kwa LUKUVI ISMANI-IRINGA.

huko Isimani kwa Lukuvi kwanikajenga hizo shule na vituo vya afya kwa hela yake mfukoni??
 
Mhh hii kali,lakini Zitto ni member hapa atakuja tu kujibu hizi tuhuma kama ni kweli.
 
Wrong approach, ndo maana hatuendelei. Siasa zetu ni mchiriku na bongo fleva, zinakuwa shaped na personalities. Mfumo wa aina hii daima utanufaisha kikundi kidogo cha jamii na wengi tutabaki kuwa masalia ndani ya nchi, haijalishi chama gani kitatawala.
 
JIMBONI KWAKE KAJENGA SHULE NGAPI?MAJI,VITUO VYA AFYA N.K naomba Mwandishi wa Zitto aende jimbo la MKONO au kwa LUKUVI ISMANI-IRINGA.


Hata mitume akiwemo Yesu alikataliwa na Wayahudi kwa kuwa alikuwa mtoto wa fulani waliye mjua kama fundi , leo sitashamngaa watu kumkwaza Zitto na hata kusema hovyo , lakini mambo ya Zitto aliyo yafanya ni zaidi ya kujenga shule jimboni .Zitto si mbunge wa jimbo moja bali amekuwa Mbunge wa Tanzania nzima utakataa lakini ukweli ni huo.
 
Watanzania wenzangu let us appreciate the good work that Zitto has done at such a youth age. Zitto is a potential MP. Even as he leaves, I will remember him for the great work he has done for his country. Let me take this opportunity to say thank you Zitto for your work, you were not only for Kigoma but for Tanzania at large. May God always guide you, protect you and give you good health.
 
Zitto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya UMMA. Muulizeni kapokea bahasha ngapi na za kiasi gani toka TANESCO, DAWASA, ATC, PPF,.....
 
Bahati mbaya Zitto hana 'dynamism' yoyote. Anahitaji muda mwingi bado wa kuweza kuelewa siasa ni nini. Alichoweza kufanya ni kutumia zaidi nguvu zake kwa kuongea kwa jazba bungeni na kutaka aonekane zaidi ya wabunge wenziwe - jinsi alivyochangamikia mambo ya TANESCO na DOWANS dhidi ya Mwakyembe and co. ni mfano mzuri. Nje ya Bunge he has done nothing spectacular!
 
Bahati mbaya Zitto hana 'dynamism' yoyote. Anahitaji muda mwingi bado wa kuweza kuelewa siasa ni nini. Alichoweza kufanya ni kutumia zaidi nguvu zake kwa kuongea kwa jazba bungeni na kutaka aonekane zaidi ya wabunge wenziwe - jinsi alivyochangamikia mambo ya TANESCO na DOWANS dhidi ya Mwakyembe and co. ni mfano mzuri. Nje ya Bunge he has done nothing spectacular!
Tupe basi mfano wa mbunge aliyefanya makubwa nje ya Bunge, au tuambie ni yapi alitakiwa kufanya nje ya bunge na asiyafanye!
 
Zitto binadamu kama watu wengine. Tatizo watu mnawarate juu sana wasipo live up to those expectations ndiyo mnakuwa disappointed. Zitto ni Zitto sasa mliomfanya as if yeye ndiye "The Chosen One" ndiyo mnaishia kuhuzunika na kusema Zitto why? Muoneni tu binadamu kama wengine. Let him exceed the odds na siyo kumkweza hata kabla hajafanya hicho kitu. Let him do him.
ni kweli kwamba hapa kuna overrating ya watu, mimi natambua sana mchango wa Zito lakini mi naona kama ni mwanzo wa safari ndefu sana...ndio kwanza ameanza..na hata hoja zake nyingi ambazo ni kweli amezisimamia na kugusa jamii, bado hazionyesha au kuleta manufaa kwa hao wananchi...kwahiyo bado zinatakiwa ufuatiliaji zaidi..tofauti na Dr.Slaa, yeye hoja yake ya ufisadi..EPA pesa zimerudishwa na kupelekwa kwa wakulima...kwa hiyo zito anakazi kubwa bado na suala la kuingia bungeni mwaka mmoja na kutangaza kutoendelea bado nasisitiza ni kuwakatisha tamaa wale wanaomuunga mkono especially jimboni kwake...
 
Zitto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya UMMA. Muulizeni kapokea bahasha ngapi na za kiasi gani toka TANESCO, DAWASA, ATC, PPF,.....
mbona umeona suala la bahasha tu??? ndio ilikuwa kazi ya mwenyekiti??? Uliza ameyasaidiaje makampuni hayo labda utatambua mchango wake...being critical doesnt mean you are right...democracy means majority wins....
 
Zitto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya UMMA. Muulizeni kapokea bahasha ngapi na za kiasi gani toka TANESCO, DAWASA, ATC, PPF,.....

Mkuu siamini kabisa kama ubongo wako unakutuma kuandika haya! siamini!

yaani hutaki apate hata posho?? ale wapi??

Please delete that post au sema umekosea!

Huyu ndio zito

''Nihitimishe makala hii kwa kukumbushia sifa tano kuu zinazomfanya Zitto ang’ae na kupaa kuliko wanasiasa wengi hapa Tanzania. Zitto ana ajenda moja tu, hashiki mambo mengi kwa wakati mmoja. Anafanya utafiti. Tatu Zitto ni mtu wa msimamo, nne anaongelea vitu vinavyogusa wananchi moja kwa moja. Mwisho, anaweka msimamo wake wazi''

hii wengi hawawezi, kiongozi ni msimamo!
 
Mkuu siamini kabisa kama ubongo wako unakutuma kuandika haya! siamini!

yaani hutaki apate hata posho?? ale wapi??

Please delete that post au sema umekosea!

Huyu ndio zito

''Nihitimishe makala hii kwa kukumbushia sifa tano kuu zinazomfanya Zitto ang’ae na kupaa kuliko wanasiasa wengi hapa Tanzania. Zitto ana ajenda moja tu, hashiki mambo mengi kwa wakati mmoja. Anafanya utafiti. Tatu Zitto ni mtu wa msimamo, nne anaongelea vitu vinavyogusa wananchi moja kwa moja. Mwisho, anaweka msimamo wake wazi''

hii wengi hawawezi, kiongozi ni msimamo!
Posho yake analipwa na Ofisi ya Bunge sio Mashirika haya. Kinyume chake Kamati hii inaongoza kwa rushwa hii ya wazi. Mwenzake Dr Slaa alizikataa bahasha za Halmashauri.
 
mbona umeona suala la bahasha tu??? ndio ilikuwa kazi ya mwenyekiti??? Uliza ameyasaidiaje makampuni hayo labda utatambua mchango wake...being critical doesnt mean you are right...democracy means majority wins....
Nakumbuka alitaka kuisaidia TANESCO kununua mitambo chakavu ya DOWANS/RICHMOND? Akaona ni heri DAWASCO ifutwe ili ibaki DAWASA ambayo ni mfuko wa nyuma wa suruali za wanasiasa!
 
Back
Top Bottom