Zitto Kabwe More Than Meets the Eye!

Zitto Kabwe More Than Meets the Eye!

akili ya zito ni zaidi ya viongozi na wanachama wote wa chadema kwa pamoja
 
kusema zitto alikuwa gugu ni kukosea sana. hata kama humpendi zitto kiasi hicho sio vizuri kusema uongo. mie navyojua zitto alikuwa malaika wa Nuru na akijikweza sana hata kiasi cha kutamani kiti cha enzi kwa njia haramu! no nadhani ilikuwa mbegu njema iliyoota katika udongo mzuri nailipokomaa tayari kuzaa matunda kwa msimu wake likaja buu usiku mmoja likaitafuna mizizi ya mbegu zitto na taratibu ikaanza kunyauka
 
Asalaam aleykum Jf.

Kwanza kabisa naomba moderator huu uzi ukae hapa hapa umelenga hasa kutujenga zaidi kisiasa na kiroho.

Injili: Mathayo: 13:24-43
Yesu aliwatolea mfano, akisema, ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu. Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi magugu?

Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, basi, wataka twende tukayakusanye? Akasema, la; msije mkakusanye magugu, myafunge matita matita mkayachome; Bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

Ndugu zangu; nimetafakari huu mfano na mwenendo wa Zitto ndani ya chama cha chadema kumbe alikuwa ni Yale majani yaliyokuwa yanafanana na ngano baada ya kuzaa ndipo yakaonekana kumbe si ngano ni magugu!

Baada ya chadema kugundua kumbe Zitto na wafuasi wake yalikua magugu ndani ya chadema, mchakato wa kuyachoma moto ulianza mara moja. Moto umekuwa mkali sasa wanakimbia mmoja baada ya mwingine si mmesikia Kigoma, Temeke, Ubungo na huko kanda ya magharibi.

Ifahamike kwamba chadema walishajua haya magugu muda mrefu kwa kuwa viongozi ni wenye huruma waliwapa muda wa kujirekebisha ili warejee njia ya haki wao waliendelea kujimvinjari katika kukiumiza chama.

Rai yangu kwa chadema mnapo fanya chaguzi zenu ndani ya chama, epukeni mapema kupanda mbegu mkalala usingizi na kumpa nafasi adui, kupanda magugu katikati ya ngano itakuwa vigumu kutambua yupi ni chadema damu na msaliti.

Mwenye tafakari zaidi ya hii anakaribishwa kuchangia na kuboresha.

Naomba kuwasilisha.

hivi kwanini chadema mifano yenu yote ni ya kunukuu biblia tu..au chadema ni kanisa?
 
Hoja imepita na kuungwa mkono. Sasa nitawahoji; wanaoafiki waseme ndiooo... na wasioafiki waseme sio. Waliosema ndio wameshinda. Mjadala umefungwa.

Kuhusu taarifa mh spika..mh spika naomba muongozo kuna mtu kaniita tumbili
 
Zitto ni mchawi wa harakati za ukombozi namfananisha na lyatonga mlema. Kwa chadema haya ni mapito tu na lazma tupitie.
 
-huo ni ukweli mkuu pia niongeze kuwa hawa wasaliti wamo na wasiri wetu ambao mwisho wa siku act+ccm watajajua kwanini tunasema chadema ni mpango wa mungu.
-nimekuja kigoma juzi,nilicho kiona ni kuhama kwa wasaliti wao kama wao bila chembe ya wafuasi wa cdm.
-cha kufurahsha misingi inaendelea kwekwa kila pembe ya kigoma na wilaya zake.
 
Hoja imepita na kuungwa mkono. Sasa nitawahoji; wanaoafiki waseme ndiooo... na wasioafiki waseme sio. Waliosema ndio wameshinda. Mjadala umefungwa.


Nikweli hoja imepita lile lilikuwa gugu tena kule unyamwezini-Tabora wanasema Lugowi nimoja ya gugu baya sana.

Lugowi ni gugu hatari likimea likajizatiti kuliangamiza kunahitaji nguvu za ziada na agharabu hutambaa huku likiweka mizizi kila liendako.
 
kusema zitto alikuwa gugu ni kukosea sana. Hata kama humpendi zitto kiasi hicho sio vizuri kusema uongo. Mie navyojua zitto alikuwa malaika wa nuru na akijikweza sana hata kiasi cha kutamani kiti cha enzi kwa njia haramu! No nadhani ilikuwa mbegu njema iliyoota katika udongo mzuri nailipokomaa tayari kuzaa matunda kwa msimu wake likaja buu usiku mmoja likaitafuna mizizi ya mbegu zitto na taratibu ikaanza kunyauka

-hakika zzito ni mithili ya mtoto aliye mwuliza baba yake atakufa lini ili yeye apate kurithi mali za babaye.
-na nikweli hili lilikuwa gugu lililomea kama mdhabibu kumbe ni gugu maji,
hii dhambi ya ubinafsi na umimi itamtafuna hadi kifo!
 
nikweli hoja imepita lile lilikuwa gugu tena kule unyamwezini-tabora wanasema lugowi nimoja ya gugu baya sana.

lugowi ni gugu hatari likimea likajizatiti kuliangamiza kunahitaji nguvu za ziada na agharabu hutambaa huku likiweka mizizi kila liendako.

haliwezi kamwe kumea katika maji maana sisi wa kulikata tupo tena tumejiandaa ipasavyo kulidhibiti,ni suala la muda tu.
 
Back
Top Bottom