Zitto Kabwe, hii ni kweli?

Zitto Kabwe, hii ni kweli?

acheni ushabiki.zitto ni mbinafsi mbona hakushirikisha viongozi wenzake.
mlidhani jk atakurupuka amewapotezea mazima

Ngoja tukupigie makofi ya kuwa msaliti dhidi ya watanzania wenzako masikini,unatamani kula na Serikali ya kifisadi,unatamani kuuza utu wako sababu ya pesa chafu za mafisadi?Kwa mawazo yako Zitto kafanya makosa kuutetea ukoo wako ama kafanya vibaya?
 
Tatizo lipo kwenye ufahamu wa mleta thread wala sio Zitto au mwandishi, Msukumo ulioletwa na Donors na Wananchi ni kutafuta dawa ya Wizi, Zitto ndo akaja na hoja ya kumtoa Pinda ili kuleta uwajibikaji,usijaribu ku escape goat, kama we ni bingwa wa kuktetea katafute utetezi kwa wale wanaosafirisha Tembo,realocation ya 1.3 TRILLION bila ya kibali cha bunge, nenda katafute point za kuhalalisha wale waliopewa Vitalu bila ya kuomba, wenzako wanaotetea wananchi hawajifunzi umaskini kwenye semina elekezi kama nyie!
 
i wish norway could see how their their aids to tz is mishandled.
waache kusaidia budget hakuna maendeleo
others donors also should withdraw from aiding tz
kama walimtuma zito poa tu kwani hakuna transparency serikalini na wizi umekithiri
Norway wameshajitoa kusaidia miradi kama mitano tz sababu ya misuse of fund. Aibu
 
acheni ushabiki.zitto ni mbinafsi mbona hakushirikisha viongozi wenzake.
mlidhani jk atakurupuka amewapotezea mazima
JK kaipotezea na familia yako sio sisi tu kama wewe tu umepona wewe tu kutuletea habari
 
Acha umbea Zitto mwenyewe kakiri ni pressure

Pressure ni nini? Aina gani ya pressure ameipata? Je, hiyo pressure imetolewa katika mazingira gani?. Halafu hivi wewe katika maisha yako ya kila siku ni vitu gani vinakufanya ujengeke kiakili na mawazo na kuamua kufanya jambo fulani la msingi? Ukijijibu basi utaona aliyeleta hii thread ana tatizo la kuona mbali, sasa sijui na wewe unamuunga mkono.
 
Kwenye gazeti la the Guardian on Sunday la tarehe 22 April 2012 kuna habari inayosema kuwa Zitto kusimamia zoezi la petition kwa ajili ya kumng'oa Pinda linatokana na 'pressure' ya wananchi na baadhi ya 'donors' kutoka Norway.

"In a telephone interview with The Guardian on Sunday, Kabwe, who is Kigoma North MP, said, “I acted alone…I asked God to help me after a lot of pressure from Tanzanians and some donors from Norway.”

Mimi nilifikiri msukumo ulikuwa ni wa ndani ya Zitto (patriotism, deep thinking, creativity and political will), lakini kumbe kutoka nje. Je, huku ni kukomaa kisiasa au ndio spanner mkononi?

Source: :: IPPMEDIA (search using a keyword Zitto or Kabwe)

Mkuu mbona sijakuelewa vizuri, nani anaweza kuthibitisha kilicho zungumzwa kwenye SIMU; kama wewe ni mzalendo wa kweli mwenye uchungu na TAIFA lako unaweza kweli kabeza ujasiri ZITO KABWE-tukiachilia mbali mambo ya itikadi za vyama. Sisi tumeona kwa macho yetu jinsi wabunge walivyokuwa wame chachamaa, hata sisi raia yalitutia uchungu sana; kinacho sikitisha zaidi ni kwamba Viogozi walio pewa dhamana na Mh.Raisi kuongoza Wizara, karibu wote walisomeshwa bure mpaka vyuo vikuu - inakuwaje tena wanasahau waliko toka na kufanya madudu ya kulifedhehesha Taifa letu na Raisi aliye wateuwa!

Mimi nina hakika ZITO akuwa na nia ya kutaka Mh.Pinda ang'olewe madarakani - alichofanya pale ni kuwakumbusha wenzake kwamba, hawana mamlaka ya kuwajibisha Mawaziri hata wakisema usiku kucha hakuna litakalo tokea, lakini kuna mbuni inayo weza kuanzisha a chain reaction ya kuharakisha mambo na hiyo ndiyo karata aliyo gangania ZITTO - I am sure hata Mh.Pinda rohoni mwake alijua akulengwa yeye.

Sasa mtu akianza ku-question "patriotism sijui na deep thinking" ya ZITO! basi mtu unakuwa na wasi wasi kama mtu anaye tamka maneno kama haya ni Mtanzania mwenzetu.

Mweshimiwa Raisi aliwahi kusema akili za kuambiwa changanya na za kwako - hilo Gazeti la Guardian lilikuwa na madhumini ya ku-water down ujasiri wa ZITTO wanatumbukiza mambo ya ma-donors as if Watanzania wa leo hawawezi kuwa na akili za kuchambanua mambo mpaka wapate shinikizo kutoka kwa WAZUNGU, hii ni propaganda mbaya sana; mtu ukiangalia kijuu juu unaweza kufikili ni maneno tu, siyo kweli! nia yao ni kuonyesha kwamba kuna external pressure ndiyo inataka kutuvuruga - tuko mahili kuwalaumu watu wengine wakati sisi ndiyo tunakosa mahadiri ya kazi na kuwajibika - mambo ya kutafuta mchawi hayatufikishi POPOTE.
 
Acha umbea Zitto mwenyewe kakiri ni pressure

Kama ni pressure basi hapa kuna tatizo kidogo.

Hiyo pressure anapewa Zitto kama Mbunge awe CDM kama chama cha siasa. Hasa hii pressure toka kwa donors ina maana donors wana deal na Zitto kama individual badala ya kudeal na Chama kama organization?
 
acheni ushabiki.zitto ni mbinafsi mbona hakushirikisha viongozi wenzake.
mlidhani jk atakurupuka amewapotezea mazima

kama angekua mbinafsi saini 74 zingepatikana kweli?
 
Back
Top Bottom