Zitto Kabwe anena haya kuhusu ESCROW

Zitto Kabwe anena haya kuhusu ESCROW

Kwa wote wenye huruma na umaskini wa kusababishiwa na wajasiliamali wa kisiasa waliumizwa sana na inshu ya escrow..

Ilisisimua,ilitisha na kuwavua nguo za ndani wengi sana japo hekima ya ufisadi ilitumika kufunika kombe..

Pongezi kwenu nyote mliohusika katika kututoa matongotongo tulio wengi juu ya uharamia wa haki zetu na za walioporwa {SCB HK}.

Pamoja na mengine nilijifunza kuwa unapaswa kuwa na moyo mgumu kukubali maneno,porojo,ahadi,utetezi,hoja,..za wanasiasa..Nguvu ya Propaganda
 
Kuna mwaka Richard Mgamba alipata ajali mbaya pale mwenge,gari lake liligongwa.
Hii vita ilikua ni kubwa sana.

Huyu ndugu nimemfahamu kupitia taarifa kadhaa..Ni moja ya hazina kubwa sana kwa taifa hasa katika mambo yenye taswira ya uzalendo usio na shaka.Anaweza kuitumia kalamu yake vema ili kufanikisha lengo la kimkakati ili kuisaidia nchi.Tatizo ni pale wenye nguvu wanapokuwa kinyume na wapenda haki,kweli...
 
Gazeti la uhuru hata lingepewa taarifa hii lichapishe lingetoka na kichwa cha habari, KUNA NJAMA ZA KUICHAFUA SERIKALI, hilo ndilo gazeti la uhuru
 
Dhumuni ni jamii kufaham kuwa siyo wanasiasa tu waliofanikisha hilo tukio bali wapo ambao jamii ilikuwa haiwatambui.

Kwa sisi tunaowafaham wanaomchukia Zitto hatupati taabu kuona yale unayoyaandika yapo mlengo gani.

Take care, is soo bad to hate someone for such ideology.
Wenzako wamemchukia mpaka wanaona siyo sahihi wanachokiwaza.
Andiko langu halikulenga kufafanua chuki ama pendo.

Unajiaibisha kudhani namchukia Zitto, ungeeleweka na kiukweli ungekuwa sahihi kabisaa kama ungesema "Humwamini Zitto"
Ningekujibu Ni kweli Zitto haaminiki.
 
Makala hii imenifungua macho zaidi kuwa serikali iliyopita ilikuwa mifukoni mwa watu wachache ambao walikamata Bunge (spika alipewa ziara akazurure Paris), Mahakakama, madhehebu ya dini, vikundi vya mauaji,nk sijui kama jeshi letu tukufu la Wananchi nalo lilibaki salama.
 
Mimi nafikiria tu itakafika mahali Rais mstaafu anatajwa katika kesi hii, kesi itaendekea? Na tunaambiwa ni marufuku kuwagusa hai waheshimiwa

Rais ni mwanadamu hivyo anayo mapungufu kwa namna moja ama nyingine hivyo kukosea ama kutuhumiwa kukosea si ajabu.Lakini pia tukumbuke kuwa Urais ni kazi ngumu mnoo na pana sana kiutekelezaji ndio maana kila mara wenye kushika nyadhifa husika wamekuwa wakilalama juu ya ugumu na uzito wake..
 
Bunge lingekuwa huru 100% hakika nchi ingesonga tu, Maana serikali hata kama haitaki mshipa wa aibu ungepasuka tu.
 
Andiko hili limenikumbusha Willy Gamba ktk ile riwaya iitwayo Njama kama ilivyoandikwa na RIP E. Musiba. Riwaya za wakati ule zikiwemo Kikosi cha Kisasi na Hujuma ziliwapa sana vijana ujasiri!
Hizo liwaya ndio zilitakuwa bongo movi waumize kichwa kuzitoa. yaani zingeuza tu bila ya shuruti ya kuzuia movi za nje
 
Ujinga wa siasa za Tanzania waliopo nyuma ya pazia wanalindwa na katiba. Mimi naomba maoni yako mh Zito, mtapigana vita ila hamtashida kwa sababu tuna-deal na matokeo na siyo chanzo. Katiba katiba ndiyo tatizo. Nawaonea huruma sana kwa sababu mnahatarisha maisha yenu
 
Huyu jamaa hata aandike kwa kutumia wino wa damu,kujisafisha na kupendwa tena itakuwa ngumu sana
 
Mkuu bandiko lako limenigusa mno
Wabunge mkiondoa uvyama mkiwa bungeni mtatufikisha sehemu salama
 
Hili suala walilitendea haki Kafulila ,Zitto ,Deo na wengine nakumbuka hii ripoti ililindwa usiku kucha .
 
Duh si mchezo, binafsi nilihisi toka zamani kuwa Kuibuliwa na kufanikiwa kwa Maazimio ya bunge dhidi ya ESCROW kuna brainpower kubwa sana nyuma yake.

Viva Kafulila
Viva Zitto
Viva Marehemu Deo
Viva Kigwangwallah
Viva Mpina
Viva Lissu
Viva Mbowe
Viva Lugula
Viva Makinda
Aisee ukiweka uzalendo mbele mambo yote yana kuwa poa
 
Inawezekana chuki ina tafsiri nyingi, if that the case no problem.
Sikulaumi kutomuamini Zitto kwani hata yeye mara nyingi anasema "tusiwaamini wana siasa"
Lakini andiko lako halikuonyesha kutokumuamini ila kuonyesha kuwa Zitto anataka sifa na hata ukadiriki kumtaja Ramadhan Dau...sijui naye amekufanya nini?

Siasa za KUSHIKIWA mbaya sana.

Andiko langu halikulenga kufafanua chuki ama pendo.

Unajiaibisha kudhani namchukia Zitto, ungeeleweka na kiukweli ungekuwa sahihi kabisaa kama ungesema "Humwamini Zitto"
Ningekujibu Ni kweli Zitto haaminiki.
 
Back
Top Bottom