Katika Taarifa ya Habari ya TBC1 ya Saa kumi Jioni Kamanda wa Polisi wa Kanda maalum ya DSM amekaririwa akisisitiza kwamba Polisi bado wanamtafuta Zitto Kabwe na kwamba watahakikisha anakamatwa ikiwa hatajisalimisha kama kweli yeye ni mzalendo.
UPDATES
Mwenyekiti moja ya kamati za Chama ametuma ujumbe huu
Habari.
Nimepata simu ya Kamanda wa Polisi Wambura saa tisa na nusu. Na akaniomba nimfikie Kiongozi wa Chama na kumwambia afike kituo cha polisi cha kati.
Mimi, Kiongozi wa Chama na Mwanasheria tuko njiani kuelekea kituoni.
Kiongozi wa chama ameomba tuwe watulivu tukawasikie wanachoitaji na tutawajuza yanatoendelea.