mgt software
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 13,793
- 7,165
Huu ni ushahidi wa kufoji, hamna kitu hapa.
Msando hajavuta huko PAP? Leka dutigite hawajawahi kulipwa na TANAPA?Huu ni ushahidi wa kufoji, hamna kitu hapa.
Muhongo yule ni dalali hajaonewa bado kumpeleka sero
jamani zito ni mchafu sana.kwanini apewe hela za mashirika ya umma kama nssf?mbona kuna vituo vingi sana vya watu wenye matatizo na hawapewi hiyo misaada?nawanyooshe kidole ole wenu
Kwenye orodha ya watu waliokua wakimtetea zzk kwamba kaonewa na CDM, jina lako pia lipo! Hatimae umeanza kuelewa sasa.
Data za Lusinde na yule mbunge wa Kishapu.Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya hesabu za Serikali (PAC) ameanza kuchunguzwa na Taasisi ya kuzuia na Kupambana na rushwa kwa kutuhuma za kutumia rafiki zake wakiwamo mawakili Beatus Malima na Albert Msondo , kupokea fedha kutoka Kampuni ya Pan Africa Power Solutions(T)Limited. Habari zilizolifikia Gazeri la Jamhuri zinaonesha kuwa April 3 na 8, 2014 kwa nyakati tofauti marafiki zake hao walipokea Sh. Milioni 10 na dola 5,000 kutoka Kampuni hiyo kwa niaba ya ZITTO.Pia kupitia Kampuni yake ya Gombe Advisors and Leka Dutigite Ltd iliyosajiliwa BRELA kwa namba 92959 Agosti 13 , 2012 na kipindi cha miezi minne tu tangu iliposajiliwa ilianza kupata fedha kutoka Mashirika ya Umma tofauti na Kampuni za Watu wengine ambao hawana wadhifa kama alio nao.
Kampuni ya Leka Dutigite Ltd imepata zaidi ya sh. Mil. 12.2 kutoka Hifadhi ya Taifa ya Sadani na mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii(NSSF) , zaidi ya Sh. Milioni 80. Kitendo cha kupokea hizo na zile za IPTL ndivyo vinavyochunguzwa iwapo hakutumia nafasi ya PAC kwa manufaa binafsi.
Hapo chini ni baadhi ya nyaraka zinazofanya Mbunge wa Kigoma Kaskazini , Zitto Kabwe achunguzwe kutokana na madai ya kuchukua fedha Kampuni ya PAP
![]()
Chanzo: Gazeti la Jamhuri
Wakati wa mjadala wa sakata la ESCROW bungeni hili swala liliibuliwa na Nchambi pamoja na Lusinde, wakadai wana nyaraka. Lakini wakati Zitto akijibu hoja nakumbuka aliweka commitment yake swala lipelekwe kamati ya maadili ya bunge na yeye yupo tayari kuwajibika ikiwamo kujiuzuru ubunge wake ikiwa itathibitika ni kweli.
Kwangu nilijua kwa kuwa jambo lile liliibukia bungeni tena baina ya wabunge kutuhumiana nikajua commitment ya Zitto ni suluhu mujarabu ili ukweli ufahamike. Sasa kama wale ndugu Nchambi na Lusinde waliibua hili na kudai wana nyaraka kwa nini wasingekubaliana na Zitto na kuweka commitment zao kama mwenzao? Na kwa nini Spika alilikalia kimya pasipo ufafanuzi wowote? maana hizi zilikuwa ni tuhuma dhidi ya mwenyekiti ambaye kamati yake imeshiriki uchunguzi uliokuwa unajadiliwa.
Tayari tumeshatuma ujumbe kwa RPC wa dodoma kuomba kibali cha kuandamana, pia tunaandaa barua ya kumpelekea mama makinda kumwomba amwondoe kupisha uchunguzi. ieleweke hatujamtuhumu wizi ila tunataka kujiridhisha kuwa ni mtu safi kuendelea kusimamia rasilimali zetu kupitia PAC.
Unaweza kumtetea mtu kwa kosa moja lakini usimtetee kwa kosa jingine. Kwa hili hata mie nashinikiza Zitto achukuliwe hatua kali. Kwa nini yeye na si DeoFilikunjombe?
Lilivyo pumbavu likadhani linaweza kununua uenyekiti wa CDM kwa vijisenti vyalo vya wizi!
asipoachia ngazi tutaenda kumtoa kwa nguzu bungeni, tumeshaanza kuhamasishana na kufikia jmosi haja ng'oka tutaanza kupanda mabasi kuelekea dodoma tayari kwa kazi ya kumng'oa asijifanye kotapini. tundu lissu lema na sugu kama mtamshindwa basi tegemeeni mshikemshike wiki ijayo, hakianani dodoma haitakalika.
Linapokuja suala la Zitto pro-Chadema wote wapo radhi kuutumia ushahidi wa Lusinde, kama reference siasa za Tanzania ni kituko.
Na huyu nyepesi hajaonewa hiyo ni kusema kwamba naye jela inamsubiri
Huna akili kabisa ww!
pole zzk tatzo ulilonalo ni uzalendo uliopitiliza haya yote yanakuja toka siku ulipogusa ruzuku za chagadema hakuna jambo lolote lingne zaid ya hilo wachaga wanakuchukia sana,nakushaur upunguze uzalendo
viva zzk
unanitaka tafadhari usipotoshe, mtu aplot kutoa fedha kwa CO ya PAP na VIP Hotelini Kunduchi, asipewe kitu kwa kweli??
Tupate majina ya wafaidika wa Stanbic Bank, tuwe na uhakika kama Muhongo hayumo!!