Zitto kaanze na Mwongozo wa Spika!

Zitto kaanze na Mwongozo wa Spika!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Kama wewe kweli una nia ya kutusaidia kama watanzania wenzako,anza na hili Bunge lijalo. Bunge likianza tu,omba Mwongozo wa Spika na uwataje Waficha Mabilioni Uswisi na kwingineko ulikodai kwenye hoja yako.Usiisubiri Serikali iwataje. Yaweza isifanye hivyo kamwe.

Ukiwataja,hoja yako itapata nguvu mpya na itajadilika angalau kama Richmond. Kama huna majina,omba Mwongozo wa Spika na ufute hoja yako. Kwakuwa haitakuwa na nguvu na maana tena bila majina ya waficha mabilioni. Sisi watanzania tumewachoka viongozi waficha-siri kwa kila kitu.Wale wa 'nitaje-nisitaje' hawana nafasi tena.

Kawataje,mjadili na tuwaone na tuwasikie misimamo yenu.

cc Zitto
 
Kweli Bana, hii tabia ya kuleta vitu nusu nusu imeshapitwa na wakati...
 
si Lahisi kama mnavyofikiria,sababu wausika ni wakuu kwenye nchi
 
Zitto ulitufanya wajinga kusema ungewataja waficha fedha, lakini unakuja na mambo ya hajabu tu! tunaomba uwataje hao mabwana! hata kama hatuwezi kuwafanya kitu lakini itasaida kupunguza kura zao 2015, vinginevyo unacho fanya ni unafki, au unatuchezea mchezo ili kushirikiaana nao kupoteza mango na mwisho wa siku hili jambo linaishia hewani au linapoteza uzito wake
 
Akishawataja ndo inakuwaje? Ndo zitarudishwa au? Mangapi yamejadiliwa kwenye bunge na yameishia yalivyoishia?
 
Mkuu Petro katika majina 26 aliyokuja nayo Mzee Tupatupa hapa na mods wakatoa haraka jina la Zito lilikuwepo, mi napata kizunguzungu kwa kweli tumuombe mzee tupa tupa atuambie kama alikuwa anatania, inakuwaje kuwaje haya makitu.
 
Kama kweli ana nia njema na umma wa Watanzania wengi masikini awataje kwa majina hao mafisadi na mabilioni yao huko ughaibuni, , upande wa pili tunahitaji hayo mabilion maana uchumi uko hoi na Zitto tusaidie kuuliza je hadi lini tutatumia pesa halali na haya makaratasi yaliyochapishwa baada ya uchaguzi wa 2010, this is ridiculous , using different denomination notes within a country! Blablahhh zimepitwa na wakati.
 
Mnadhani atafanya hayo? Thubutu majibu alishatoa siku ile pale star tv hamkumsikia?
 
....majina majina majina....yamegoma.
 
Mkuu Petro katika majina 26 aliyokuja nayo Mzee Tupatupa hapa na mods wakatoa haraka jina la Zito lilikuwepo, mi napata kizunguzungu kwa kweli tumuombe mzee tupa tupa atuambie kama alikuwa anatania, inakuwaje kuwaje haya makitu.
Tanzania sasa wamejaa watu wakuficha tu.Tuanaupungufu mkubwa wa watu wa kufichua.
 
Akishawataja ndo inakuwaje? Ndo zitarudishwa au? Mangapi yamejadiliwa kwenye bunge na yameishia yalivyoishia?

Ok hajawataja kwani zimerudishwa bora awataje waishi kama POPO ata wasipochukuliwa hatua huoni CHENGE,KARAMAGI,MSABAHA na NGOYAI wanavyoweweseka kila kukicha.
 
Kaka Zitto tunaomba ututajie majina hayo ili sisi wananchi tuendele kujua ni wakina nani ni maadui zetu lakin mkisema kuna wezi bila kuwataja majina basi itakuwa work done is equal to zero.
 
Back
Top Bottom