Lakuchumpa123
Senior Member
- May 26, 2015
- 138
- 74
Nikiwa hapa Bukoba leo nimehudhuria mkutano wa ACT-Wazalendo katika uwanja wa Mashujaa. Kiongozi mkuu wa chama hicho,niko Zitto Kabwe alikuwa akihutubia.
Awali alianza kueleza sababu za kuondoka CHADEMA, akisema sio kosa kubadilisha jukwaa la siasa. watu walikuwa wakimpigia makofi tu.
Lakini hali ya mkutano ilibadilika na kuwa mbaya pale alipoanza kujisifu kuwa yeye ndiye aliyeagiza hesabu za CHADEMA zikaguliwe na CAG, kisha akaitwa msaliti na kamati kuu ya CHADEMA.
Hapo wananchi waliokuwa uwanjani hapo wakaanza kupiga kelele wakisema 'sio kweli, sio kweli, sio kweli".
Ilibidi Zitto abadilishe mahubiri na kuanza kueleza msimamo wa chama chake. Lakini watu wakawa hawamsikilizi tena. Wengine walisikika wakisema, "kama umekuja hapa eleza ya chama chako, ya CHADEMA uyaache,".
Kama hiyo haitoshi, Zitto akaanza tena majigambo akisema eti alipokuwa bungeni aliiangusha serikali mara tatu, "Hao wanaokuja kunitukana waseme wamefanya nini bungeni" alisema Zitto.
Watu waliendelea kuzomea hadi Zitto akasema, "Kama hamtaki kunisikiliza naondoka zangu,". Watu wakajibu,waliendelea kuzomea " Nendaaa...!
Hata hivyo mkutano umeisha salama.
Kwa kweli Zitto ana kazi ngumu kuijenga ACT-Wazalendo?
Awali alianza kueleza sababu za kuondoka CHADEMA, akisema sio kosa kubadilisha jukwaa la siasa. watu walikuwa wakimpigia makofi tu.
Lakini hali ya mkutano ilibadilika na kuwa mbaya pale alipoanza kujisifu kuwa yeye ndiye aliyeagiza hesabu za CHADEMA zikaguliwe na CAG, kisha akaitwa msaliti na kamati kuu ya CHADEMA.
Hapo wananchi waliokuwa uwanjani hapo wakaanza kupiga kelele wakisema 'sio kweli, sio kweli, sio kweli".
Ilibidi Zitto abadilishe mahubiri na kuanza kueleza msimamo wa chama chake. Lakini watu wakawa hawamsikilizi tena. Wengine walisikika wakisema, "kama umekuja hapa eleza ya chama chako, ya CHADEMA uyaache,".
Kama hiyo haitoshi, Zitto akaanza tena majigambo akisema eti alipokuwa bungeni aliiangusha serikali mara tatu, "Hao wanaokuja kunitukana waseme wamefanya nini bungeni" alisema Zitto.
Watu waliendelea kuzomea hadi Zitto akasema, "Kama hamtaki kunisikiliza naondoka zangu,". Watu wakajibu,waliendelea kuzomea " Nendaaa...!
Hata hivyo mkutano umeisha salama.
Kwa kweli Zitto ana kazi ngumu kuijenga ACT-Wazalendo?