Zitto: Anatetea Maslahi ya Taifa zaidi kuliko ya waliompa Ubunge?

Ngoja tudhanie uzushi wote aliosema huyo jamaa ni kweli.Kuna usemi unasema "JE WANAKIJIJI HAO WAMEKIFANYIA NINI KIJIJI CHAO KABLA YA KUMULIZA ZITTO KUWAFANYIA WANAYOYATAKA" au wanataka kutoka kwa Zitto tuuu
 
Heshima yako mkuu FMeS!

Mwakalinga atagombea ubunge Kyela na hili nina uhakika wa asilimia zaidi ya 100,na Mwakalinga ni more than smarter hasa kwa umakini wake wa kuchagua timu yake ya kampeni ambayo itakuwa imesheheni wasomi,makada na watu wa kawaida lkn wazawa waliopo ndani na nje ya tz!

Ilikuwa atangaze nia yae ya kugombea si kabla ya tarehe 5 august,lkn bado hatujajua kama utangazaji huu utafanyika Kyela mjini au ktk moja ya viwanja vya shule kule Katumba au mahali pengine popote,na tutawajulisha lini shughul hii itafanyika!na hata kama kahairisha kutangaza kwa sababu ya Upepo wa kisiasa napo tutawafahamisha!

Lkn kumtoa Dr Mwakyembe ndani ya kura za maoni si kazi haba kwani mbunge huyu kwenye baadhi ya kata anachukuliwa kama 'mungu mtu'na yeyete anayepanga hata kumbishia kitu huchukuliwa kama mhaini!,kwa hiyo mpiganaji Mwakalinga anatakiwa afanye kazi ya ziada!

Yetu macho na mimi kama mpiga kura hai wilayani Kyela nitamsubiri yeyote kati yao atakayepitishwa na CCM tupambane nao kwenye sanduku la kura;kati yao hamna mwenye hati miliki ya ubunge wa jimbo la Kyela!


Malafyale uliandika:
icon1.gif
Mwakalinga Awasili Kyela Kumuangusha Dr Mwakyembe
George Mwakalinga mwana Kyela aliyekuwa anaishi na kufanya kazi kama mtaalaum wa kompyuta nchini UK amewasili Kyela majuzi na tayari ametangaza kuwania ubunge wa wilaya ya Kyela ndani ya CCM!

Mwakalinga ametoka kuongea na wana Kyela sasa hivi kwenye hotel ya kisasa ya Sativa na watu waliokuwepo hapo wanasema hapana shaka Mwakalinga kaletwa Kyela na vigogo ndani ya CCM na serikalini na dhahiri anaungwa mkono na mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mzee Mwakalinga na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Japhet Mwakasumi!

Mwakalinga,ambae pia ana vitege uchumi vingi sana wilayani Kyela zikiwemo hotel kubwa za kisasa tayari yupo Kyela,na kaanza kuzunguka kwa kasi vijijini kujinadi kwa wana CCM na kuna kila ukweli kuwa viongozi wa CCM wilayani na mkoani wamebariki kuanza huku kwake kampeni kabla ya muda wake.

Mkulu Malafyale,

- Heshima yako sana, mwananchi yoyote mwenye akili timamu sana, anahitaji kuyasoma maneno yako ya juu na chini kwa makini sana, kabla ya kuamua tatizo lako lilipo, na sitaki kuamini kwamba DK anajihusisha na wapambe wa aina yako, ninaamini kwamba yeye ni mnakini zaidi kuliko haya mawazo yako, ambayo nimeshindwa hata kuyagusa.

- Halafu naomba nikukumbushe kwamba location yako sio ishu katika kuhukumu mawazo yako hapa, ni hoja tu inayoweza kuchambuliwa, kwa hiyo uko wapi au unaishi wapi ni irrelevant.
Respect.

FMEs!
 
Mimi nikiwa Mbunge nitaanza na wale walionipa ridhaa yao kwanza,wema huanzia nyumbani.
timu Ya mpira ya Taifa lolote huangalia kiwango na mchango wa mchezaji kwenye club yake kwanza.
hatuwatendei wema watu wa jimbo lake.kina Lowassa majimboni kwao ni wafalme kwa kukamilisha mambo muhimu kwa wapiga kura wao.
tuendelee kumdanganya na kilemba cha ukoka cha Utaifa.
 
Mimi nikiwa Mbunge nitaanza na wale walionipa ridhaa yao kwanza,wema huanzia nyumbani.
timu Ya mpira ya Taifa lolote huangalia kiwango na mchango wa mchezaji kwenye club yake kwanza.
hatuwatendei wema watu wa jimbo lake.kina Lowassa majimboni kwao ni wafalme kwa kukamilisha mambo muhimu kwa wapiga kura wao.
tuendelee kumdanganya na kilemba cha ukoka cha Utaifa.
Ondoa ndoto zako za asubuhi hapa.
Zitto aliweka bandiko kuwa hana shaka na mambo jimboni kwake kwa sababu asilimia 75 ya mipango yake aliyoahidi na kukusudia alikuwa katimiza. Nadhani ni asilimia 25 iliyobakia. Hakuna aliyepinga hata sisi M hawakupinga.
Wale waha wakikosea kwa kuiamini kanda mbili watalia kilio wanacholia wenzao wa mjini kwa kumchagua Serukamba.
 
Kwa kawaida si hulka yangu kushiriki kwenye mijadala ya kashfa kama washika dau wengine walivyofanya kwenye post inayohusu mdau Mwakalinga,lkn huwa nafanya uhakiki kabla sijaleta kitu hapa na nilichosema kuhusu harakati za mwenzetu na kugombea ubunge Kyela ni kweli tupu!

Labda ambacho sikueleweka ni kutumia tamathali za semi niliposema "Mwakalinga aingia Kyela" ukweli ilikuwa hajafika Kyela phyisical lkn "kiroho" tayari huyu jamaa alikuwa Kyela muda mrefu!

Jasusi,kuanzia tarehe 1 hadi 5 mwezi August mwaka 2009,uwepo hapa ambako nitakuletea habari moja kwa moja toka ama kiwanja cha Mwakangale-Kyela mjini,au kutoka kule kijijini Katumba ambako labda rasmi mbio za kuwania ubunge Kyela zitakapotangazwa kuwa ndiyo zinaanza!
bwa ha ha ha typical majibu kama ya Kayanza P.....jamani mtu utakuwa kiroho alafu uhutubie wananchi kwenye hotel ya kisasa?
 
bwa ha ha ha typical majibu kama ya Kayanza P.....jamani mtu utakuwa kiroho alafu uhutubie wananchi kwenye hotel ya kisasa?

Hehehe mpwa jamaa alikuwa anaota ndoto za mchana eti Mwakalinga yupo kwa hotel kisha anahutubia wananchi ndoto za mchana hizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom