Dr slaa na Zito wasingerudi nyuma pengine tungekuwa mbali zaid ya hapa
Acha kuwatukana watanzania mkuu. Dr Slaa hakuwa na karisma yeyote ile ya kuwa Rais. Zitto sio mtu mzuri. Zitto ni mbinafsi sana kama hamjui. Waulizeni wale watu walio soma nao chuo kikuu mtapata majibu ya kuwa yeye ni mtu wa aina gani.
Nime mshukuru mungu hawa watu hawakuweza kuwa viongozi wetu.
Magufuli yuko ok. Tatizo ambalo analo ni ukosefu wa kujiamini. Kila anacho kifanya anataka watu wampige makofi. Hicho hakitawezekana. Ndiyo anayafanya mazuri kwa watanzania lakini kwa baadhi wanakwazika. Na wale wanao kwazika kwa bahati mbaya ndiyo wapigaji kelele maarufu.
Kitu nacho mwoomba Rais Magufuli ni kuwa asiwaone wapinzani kama maadui zake. Inatakiwa atambue kuwa wao nao ni wataka madaraka kama yeye. Sasa akija na makusudio ya kuwafunga mdomo na kuwakandamiza matokeo yake ataharibu kila kitu.
Wapinzani na wapingaji wa mafanikio yake wapo na watakuwepo tu. Na inatakiwa atambue kuwa kila nchi iliyo endelea duniani inao watu wa namna hiyo.
Kitu kingine ambacho anatakiwa akielewe wapinzani na wapinga maendeleo na mafanikio yake wapo pia kwenye serikali yake. Baadhi ya watumishi wa serikali ndiyo wanao mpinga. Hao ndiyo watu mahususi katika kutoa siri kwa wapinzani. Na majibu yake yasiwe hathari kwa wananchi wasio husika.
Aache kuwafokea binadam wenzake hadharani kama watoto wadogo. Atambue kuwa hao anao wafokea na kuwa tumbua hadarani wana watoto wanao mtegemea, pengine hata wajukuu. Sasa sioni kama ni busara kwa vizazi vya huyo mtu anaye dhalilishwa hadharani kusikia au kumwona Role Model wao wa maisha anadhalilishwa mbele ya umati wa watu. Ni kitu cha ahibu na kusikitisha kwao. Kama yeye hapendezewi kukosolewa mitandaoni basi ajue kuwa nao hawapendi kukosolewa hadharani.
Tuko katika karne ya 21. Mambo hayako kama wakati ule wa zama za Mwalim. Atumie busara kuwatawala watanzania vizuri. Asitumie ubabe. Watanzania ni waelewa wazuri sana wa mambo japo kuwa ni wavivu na hatutaki kujituma lakini please sio mabavu.
Vyombo vya dola visitumike kama njia ya kuwakandamiza na kuleta terour kwa watanzania. Huo sio uongozi mzuri.
Vingene vyote Rais Magufuli BIG UP! Endelea na vita vya kupambana na Mafisadi na walarushwa. Linda rasilimali zetu na dumisha Amani yetu.
Rais Magufuli tembelea mikoa ya kusini pia; Mtwara, Ruvuma na Mbeya hata kama hawajakupa kura nyingi. Tanzania sio Mwanza na Chato tu.