Zitto ajilipua, tusimtose

Zitto ajilipua, tusimtose

Dhulma imeisha? .Je Watumishi
Kila binadam anastahili kupewa nafasi ya kufanikisha ndoto zake. Huo pia ni msingi wa kidemokrasia kama hujui. Magufuli alikuwa na ndoto zake za kutaka kuiweka nchi sawa kulingana na matakwa yake.

Mwambie mtu makosa yake na kama harekebishiki basi tutapiga kura tena 2020. Sio mda mrefu sana kutoka sasa tuta mweka huyo unaye mwona ana rekebishika.

Na kama wewe ni mtaka demokrasia ya kweli basi kubali aendelee kumaliza kipindi chake kuhitimisha malengo yake. Na ikiwezekana kajaze wewe mwenyewe Form ugombee urais labda wewe ndiyo utaweza vizuri.

Watanzania acheni njozi zenu mnazo ziota mchana. Kutwa kucha lawama na kupiga kelele kuhusu katiba. Hakuna nchi ambayo inaendeshwa kikatiba duniani. Katiba inampa Rais misingi na mwongozo wa policy ya kutawla nchi lakini mengine yote ni Rais mwenyewe.

Mimi sijasikia katika nchi zilizo endelea wapinzani waki mtukana kiongozi wao na kumwita Dikteta uchwara! Hii maana yake ni nini? Au mpinzani kutamka "Bombardier ya Magufuli". Mpinzani ambaye pia ni mwana siasa anatakiwa atoa hoja za kisiasa za kumkosoa Kiongozi na sio kum-attack kiongo Personal!

Tatizo lako wewe hujui kwa nini wananchi wamemchagua Magufuli kuwa kiongozi wao. Watanzania walichoka na dhulma iliyokuwa inafanyika na watu walio aminiwa na umma kushika madaraka.
Waliteseka sana. Katika sekta zote za utumishi watumishi wa serikali walikuwa wanatumia wadhifa wao vibaya kuwanyanyasa wananchi wanyonge. Kila sekta na kila ofisi ya serikali ni rushwa tu na upigaji wa madeal. Leo heshima na nidham ya kazi imerudi kwa kiasi fulani wewe bado unalalamika. Kwanini hukulalamika wakati ule wananchi wananyanyasika?

Nafikiri wewe nidyo ungejiuliza mwenyewe unaishi nchi gani, kwani inaelekea umesahau yote yaliyokuwa yanatendeka nchini Tanzania.
manyanyaso wanayofanyiwa yameisha? Unadhani kiwango cha matumizi mabaya ya fedha na madaraka yameisha kwa sasa? Na je uhuru wa taasisi zinazodhibiti matumizi ya fedha za umma kama ofisi ya CAG utendaji wao upo huru kama Enzi ya awamu iliyopita?
 
Dhulma imeisha? .Je Watumishi

manyanyaso wanayofanyiwa yameisha? Unadhani kiwango cha matumizi mabaya ya fedha na madaraka yameisha kwa sasa? Na je uhuru wa taasisi zinazodhibiti matumizi ya fedha za umma kama ofisi ya CAG utendaji wao upo huru kama Enzi ya awamu iliyopita?

Hivyo wewe unaelewa kweli unacho kiandika humu? Au chuki na hasira zako za kukosa kupigia ma-deals ndiyo zina kufanya upakaze story zisizo na mikono wala miguu? Kakukosea nini Rais wa wanyonge?

Kwa imani yako unaweza ukaapa kwa Mungu wako na kututhibitishia sisi kuwa Rais Magufuli ni mtumiaji mbovu wa fedha za umma kweli?

Toka ashike aapishwe amefanya safari ngapi nje? Unajua Rais akisafiri nje inagharim kiasi gani cha fedha?

Haya yote aliyo yafanya hapa chini ni ufujaji wa fedha za umma?

- Kufufua shirika letu la ndege na kununua ndege mpya sita za kwetu ni ufujaji wa fedha?

- kuwajengea wanafunzi wa chuo kikuu blocks za kuishi wakati wa masomo yao ni ufujaji wa fedha za umma?

- elimu bure na kutengeneza madawati ya wanafunzi kwako pia ni ufujaji wa fedha za umma?

- miradi mbali mbali ya barabara, flyovers, maji, umeme, treni ya kisasa, upanuzi wa bandari Dar, Tanga na Mtwara, upanuzi na ujenzi wa Airports mpya za mikoani na International Airport Dar na KiA na kadhalika nako ni kufuja fedha za umma?

Haya mkuu endelea.
 
Usitupigie kelele za punda. Tafuta nchi nyingine ambayo utataka Zitto Kabwe awe kiongozi wako. Sio nchi ya watanzania.
Mtu mnafiki na mroho wa madaraka kama Zitto hawezi kuwa Rais hata mara moja.

Kwanza naomba jiulize kwenye hicho chama chake aliteuliwa na nani kushika madaraka ya chama aliyo nayo. Katiba na itokadi za chama chake kiko vipi?

Tatua hayo kwanza halafu njoo utuelezee smartness ya Zitto.
yaani unatumia nguvu nyingi na kubwabwaja utafikiri huyo Zitto ndio amekuwa akiongoza hii nchi kwa miaka 50 na ushehi ama ndiye chanzo cha taifa kudumaa kimaendeleo...endelea kukumbatia ujinga wako.
 
yaani unatumia nguvu nyingi na kubwabwaja utafikiri huyo Zitto ndio amekuwa akiongoza hii nchi kwa miaka 50 na ushehi ama ndiye chanzo cha taifa kudumaa kimaendeleo...endelea kukumbatia ujinga wako.
Hivyo mkuu naomba nikuulize kitu, wewe unavyo imba kuhusu maendeleo unafikiri maendeleo ni nini hasa?

Matatizo yenu nyie watoto mlio lemazwa na Facebook, twitter, Instagram, Whatsapp na YouTube mna matatizo makubwa sana!

Baadhi ya matatizo yenu;
-kwanza napenda kukuambia ili uelewe kuwa nyie wengi wenu ni wazembe na wavivu sana (samahani),
-mbili hamtaki kujituma wenyewe kufuatilia vitu na kujishughilisha na historia ya nchi yenu na ulimwengu mnao ishi kwa ujumla.

Hivyo nyie mnafikiri kwamba kila kitu kinakuja chenyewe?

Aisee kijana jitahidi kujua historia ya maisha yako kwanza na ile ya wazazi wako na ikiwezekana ile ya babu na bibi zako wanako toka na jinsi gani waliishi mpaka leo wewe kama kiumbe kuweza ku-appear na ku-exist. Na sio kulopoka tu hapa vitu usivyo vijua, maadam umevisikia kutoka kwenye vijana wenzako kwenye ma-groups yenu. Umeenda shule wewe?

Miaka 50 iliyo pita Mambo yalikuwa mengine. Hiyo mitandao yenu haikuwepo.
Habari za nje sisi tulikuwa tunazipata kupitia radios (enzi hizo sisi waswahili wa Dar tulikuwa tunaziita Bomba)
hasa BBC London, magazines za nje Newsweek na Times na pia vitabu na magazines ambazo watanzania na wageni walio toka nje walituletea. Mara nyingi habari zilizopitwa na wakati. Hatukuwa hata na ile TV sembuse mtambo wa Television.

Kuna kipindi Magazine ya Times ilifungiwa kwa kuandika habari za uongo kuhusu Mwalim Nyerere kwamba amejilimbikizia mahela kibao kwenye account yake Uswiss, kitu ambacho hakikuwa cha kweli.

Mimi nimemzungumzia Zitto kwa sababu kuna watu wame soma naye chuo kikuu ambao nawafahamu na wanamjua jinsi alivyo. Kwa taarifa yako sio mtu wa kumwamini sana. Ni mtu ambaye anataka yeye awe mbele na aonekane kila kitu yeye ndiye anajua zaidi na anacho kisema ni cha maana zaidi kuliko mawazo ya wengine.
Pamoja na haya yote tulimpa credit ya kuwa one day angeweza kuja kutuongoza.

Sasa umejiuliza kitu gani kilimtoa yeye CHADEMA?
Unakumbuka Kufukuzwa kwake CHADEMA kuli kifanya chama na pia UKAWA kupoteza wafuasi wengi, kwani existence yake na activities zake kwenye kile chama kiliwapa watanzania wengi matumaini ya kuwa wapinzani wanaweza wakawashinda CCM na wakaongoza nchi. Lakini yeye kwa pupa zake za kutaka madaraka haraka haraka alitupilia mbali mategemeo hayo yote ya wananchi kwa kuamini kuwa yeye peke yake ndiye anaye weza kukifanya chama kikashinda uchaguzi na kuongoza nchi. Alisahau kuwa team Work ndiyo iliyo kuwa inawapa nguvu kubwa. Ni mistake kubwa sana aliyo ifanya! Nafikri utakubaliana na mimi kuhusu hili.

Kwa kufukuzwa kwake CHADEMA wananchi na wataka mapinduzi wengi ambao walikuwa wafuasi wake walio weka matumaini makubwa kwa CHADEMA walisononeka sana na hatimaye kuona kuwa kumbe viongozi wote ni sawa tu. Viongozi wa CHADEMA na CCM hawana tofauti yeyote.

Kama sio hitlafu ya viongozi wa CHADEMA, hayo niliyo yasema ya Zitto Kabwe na Dr Slaa na CCM kumweka Magufuli kuwa mgombea wao, UKAWA wangeshinda uchaguzi. Definitely! Na hivi sasa tungekuwa na serikali nyingine. Na kukiona CCM ni story. Mbona wa Zenji walifanikiwa kuitoa CCM? Hata sisi wa bara tungeking'oa hicho chama.

Matatizo yaliyotekea ni kwamba watu ambao tuliwapa credibility kama akina Zitto na Dr Slaa ndiyo walio tuangusha na kutufanya sisi tusiweze kukiondoa Chama Cha Mapinduzi, sijui mapinduzi gani Mwalim Nyerere na Karume waliyafanya mpaka chama chao wana kiita hivyo?

Hivi sasa ukiniuliza kama mimi ni member wa chama chochote Bongo, jibu langu ni NO! Lakini nampenda Magufuli na nina mwamini yeye na sio mwingine yeyote katika nchi hii, japo kuwa ana hitilafu fulani fulani, pamoja na hayo nikiziweka hitilafu zake kwenye mzani na kulinganisha na matendo yake anayo wafanyia watanzania naona bado ana credibility mkubwa sana yakuwa kiongozi wetu hata awamu yake ya pili. Sina shaka naye.

Nafikiri utakubalina na mimi mkuu CCM bara imeshinda kwa ajili ya Magufuli tu. Na kama siyo yeye sijui CCM wamekuwa wapi.

Above all these discrepancies my fellow tanzanian, I would like from the bottom of my heart to say only a couple of words to you, please try to be you! JUST YOU AS AN INDIVIDUAL! Jiamini!
 
Dhulma imeisha? .Je Watumishi

manyanyaso wanayofanyiwa yameisha? Unadhani kiwango cha matumizi mabaya ya fedha na madaraka yameisha kwa sasa? Na je uhuru wa taasisi zinazodhibiti matumizi ya fedha za umma kama ofisi ya CAG utendaji wao upo huru kama Enzi ya awamu iliyopita?

Hivyo wewe unaelewa kweli unacho kiandika humu? Au chuki na hasira zako za kukosa kupigia ma-deals ndiyo zina kufanya upakaze story zisizo na mikono wala miguu? Kakukosea nini Rais wa wanyonge?

Kwa imani yako unaweza ukaapa kwa Mungu wako na kututhibitishia sisi kuwa Rais Magufuli ni mtumiaji mbovu wa fedha za umma kweli?

Toka aapishwe amefanya safari ngapi nje? Unajua Rais akisafiri nje inagharim kiasi gani cha fedha?

Haya yote aliyo yafanya hapa chini ni ufujaji wa fedha za umma?

- Kufufua shirika letu la ndege na kununua ndege mpya sita za kwetu ni ufujaji wa fedha?

- kuwajengea wanafunzi wa chuo kikuu blocks za kuishi wakati wa masomo yao ni ufujaji wa fedha za umma?

- elimu bure na kutengeneza madawati ya wanafunzi kwako pia ni ufujaji wa fedha za umma?

- miradi mbali mbali ya barabara, flyovers, maji, umeme, treni ya kisasa, upanuzi wa bandari Dar, Tanga na Mtwara, upanuzi na ujenzi wa Airports mpya za mikoani na International Airport Dar na KiA na kadhalika nako ni kufuja fedha za umma?

Haya mkuu endelea.
 
Ameandika kisomi sana na kisheria sana,kuuangusha kikatiba na mwisho kasema kura,hawezi kukamatwa kwa sababu hajafanya uchochezi kwani kasema kikatiba na kwa kupiga kura ila kaficha jambo nyuma hapo
 
Back
Top Bottom