Zitto aivaa CCM, Chiligati apuuza

Mambo Jambo

JF-Expert Member
Jul 11, 2008
1,100
81
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kabwe Zitto (pichani), amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumruhusu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), akague matumizi ya fedha za chama wakati wa Uchaguzi Mkuu, mwaka 2005.

Kwa mujibu wa Zitto, uamuzi huo utathibitisha kauli za viongozi hao kuwa chama chao hakihusiki na wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Zitto alitoa ushauri huo wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika mji wa Lamadi, wilayani Magu, mkoani Shinyanga mwishoni mwa wiki. Alisisitiza kuwa haitoshi kwa viongozi wa chama hicho kutamka tu kuwa chama chao hakihusiki bali wamruhusu CAG ili athibitishe kitaaluma.

Maelezo hayo ya Zitto pia yanaweza kutafsiriwa kama majibu kwa Mweka Hazina wa CCM, Amos Makala ambaye wiki iliyopita alisema chama chake hakihusiki na wala hakikushirikiana na kampuni yoyote kuiba fedha za EPA.

Makala alitoa kauli hiyo alipokuwa akifungua mkutano wa Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam. Katika kukanusha kwake, Makala alisema hata Msajili wa Vyama vya Siasa amethibitisha kuwa CCM hakihusiki na wizi wa fedha Benki Kuu, na kwamba wanasiasa wanaohimiza upotoshaji huo wanastahili kupuuzwa.

Lakini akihutubia wananchi, Zitto alisema; “Iwapo CAG ataruhusiwa kukagua hesabu za CCM na kuweka hadharani matokeo ya ukaguzi huo, Watanzania wataweza kuridhika kwa sababu wengi wanaamini CCM ilichota fedha EPA, Benki Kuu na kuzitumia katika kampeni.”

“Nilimsikia Mweka Hazina wa CCM Amos Makala akisema CCM haikuchota fedha za EPA. Kama kweli hawakutumia fedha za EPA katika kampeni zao basi wamruhusu CAG akague hesabu zao na za vyama vingine na majibu ya ukaguzi huo yawekwe hadharani,” alisema.

Mtanzania iliwasiliana na Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, John Chiligati, kuhusu changamoto hiyo kutoka kwa Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini. Katika majibu yake Chiligati ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi alisema; “Huyo Zitto hana jipya lolote alilosema na hizo ni porojo za kisiasa zisizokuwa na maana au tija yoyote kwa wananchi.”

Alisema hesabu za CCM zilikwishakaguliwa na Msajili wa Vyama Vya Siasa ambaye hufanya kazi hiyo kwa mujibu wa sheria.

“Kila mwaka hesabu zetu zimekuwa zikikaguliwa na si za chama chetu tu na hata vyama vingine vya siasa. Sisi hatuna cha kuficha, kama wapo wengine wanataka kukagua waje tu, ila anachosema Zitto ni porojo zisizo na maana,” alisema Waziri Chiligati. by Na Maregesi Paul, Magu -Mwananchi


My Take:Ofisi ya msajili wa vyama lazima watakuwa wanafanya mahesabu na si kwa CCM tu bali hata kwa vyama vingine.

Je ofisi ya msajili wa vyama imesimamia wapi juu ya hilo, au wenyewe hukagua fedha walizotoa wao tu, kama ndiyo wazo la Mh Zitto ni zuri sana, wananchi wajue fedha za kampeni ile zilitoka wapi, wazibue mirija yote.

MJ
 
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kabwe Zitto (pichani), amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumruhusu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), akague matumizi ya fedha za chama wakati wa Uchaguzi Mkuu, mwaka 2005.

Kwa mujibu wa Zitto, uamuzi huo utathibitisha kauli za viongozi hao kuwa chama chao hakihusiki na wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Zitto alitoa ushauri huo wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika mji wa Lamadi, wilayani Magu, mkoani Shinyanga mwishoni mwa wiki. Alisisitiza kuwa haitoshi kwa viongozi wa chama hicho kutamka tu kuwa chama chao hakihusiki bali wamruhusu CAG ili athibitishe kitaaluma.

Maelezo hayo ya Zitto pia yanaweza kutafsiriwa kama majibu kwa Mweka Hazina wa CCM, Amos Makala ambaye wiki iliyopita alisema chama chake hakihusiki na wala hakikushirikiana na kampuni yoyote kuiba fedha za EPA.

Makala alitoa kauli hiyo alipokuwa akifungua mkutano wa Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam. Katika kukanusha kwake, Makala alisema hata Msajili wa Vyama vya Siasa amethibitisha kuwa CCM hakihusiki na wizi wa fedha Benki Kuu, na kwamba wanasiasa wanaohimiza upotoshaji huo wanastahili kupuuzwa.

Lakini akihutubia wananchi, Zitto alisema; “Iwapo CAG ataruhusiwa kukagua hesabu za CCM na kuweka hadharani matokeo ya ukaguzi huo, Watanzania wataweza kuridhika kwa sababu wengi wanaamini CCM ilichota fedha EPA, Benki Kuu na kuzitumia katika kampeni.”

“Nilimsikia Mweka Hazina wa CCM Amos Makala akisema CCM haikuchota fedha za EPA. Kama kweli hawakutumia fedha za EPA katika kampeni zao basi wamruhusu CAG akague hesabu zao na za vyama vingine na majibu ya ukaguzi huo yawekwe hadharani,” alisema.

Mtanzania iliwasiliana na Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, John Chiligati, kuhusu changamoto hiyo kutoka kwa Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini. Katika majibu yake Chiligati ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi alisema; “Huyo Zitto hana jipya lolote alilosema na hizo ni porojo za kisiasa zisizokuwa na maana au tija yoyote kwa wananchi.”

Alisema hesabu za CCM zilikwishakaguliwa na Msajili wa Vyama Vya Siasa ambaye hufanya kazi hiyo kwa mujibu wa sheria.

“Kila mwaka hesabu zetu zimekuwa zikikaguliwa na si za chama chetu tu na hata vyama vingine vya siasa. Sisi hatuna cha kuficha, kama wapo wengine wanataka kukagua waje tu, ila anachosema Zitto ni porojo zisizo na maana,” alisema Waziri Chiligati. by Na Maregesi Paul, Magu -Mwananchi


My Take:Ofisi ya msajili wa vyama lazima watakuwa wanafanya mahesabu na si kwa CCM tu bali hata kwa vyama vingine.

Je ofisi ya msajili wa vyama imesimamia wapi juu ya hilo, au wenyewe hukagua fedha walizotoa wao tu, kama ndiyo wazo la Mh Zitto ni zuri sana, wananchi wajue fedha za kampeni ile zilitoka wapi, wazibue mirija yote.

MJ
Lamadi haiko mkoani Shinyanga bali iko mkoani Mwanza
 
hili swala wakubwa hawataki lizungumze- naomba Zitto na team waliongezee ukali hili swala maana hili ndilo litakalo watoa madarakani CCM hawana mahala pa kujificha; ukilegeza sauti maana yake umeshindwa; waongeze sauti uchunguzi ufanywe na CAG sio msajili; msajili anakagua hela alizotoa tu; after all msajili report yake ni open? to what extent ( wasi ni integrity ya hizo finding za msajili)
 
CHADEMA kama mpo serious basi CAG akague hesabu za vyama vyote na atoe ripoti kuonyesha fedha zinazoingia na kutoka maana mnaongelea CCM tu je hivi vyama vingine vina matumizi mazuri ya fedha? Nyie nanyi si mnagombana mara kwa mara? Ooh nusu ya fedha anakula Mbowe mara ooh sijui nini?
Nyie CHADEMA na vyama vingine ni wasafi kiasi gani?
 
You gotta love Zitto.

Haya ndiyo nilikuwa nazungumzia the other day niliposema tunahitaji issues zenye kishindo, sio kulalamika na marginal issues.

Sasa hapa CCM, kwa watu wenye akili zao, wameonyesha kujigamba kwamba wako clean halafu Zitto kawaambia why should we take your word? Why can't we conduct an audit, from a supposedly neutral observer and then find out for real?

Brilliant proposition.

My only major concern is that the AIG is not beyond the clutches of CCM and may be compromised.
 
Last edited:
CHADEMA kama mpo serious basi CAG akague hesabu za vyama vyote na atoe ripoti kuonyesha fedha zinazoingia na kutoka maana mnaongelea CCM tu je hivi vyama vingine vina matumizi mazuri ya fedha? Nyie nanyi si mnagombana mara kwa mara? Ooh nusu ya fedha anakula Mbowe mara ooh sijui nini?
Nyie CHADEMA na vyama vingine ni wasafi kiasi gani?

Jamani muwe mnasoma post za watu kabla ya kuzijibu au kujadili maana ungepata jibu la post yako hii.
Jibu ni hili lilikuwa katika post unayojadili.
Kama kweli hawakutumia fedha za EPA katika kampeni zao basi wamruhusu CAG akague hesabu zao na za vyama vingine na majibu ya ukaguzi huo yawekwe hadharani,” alisema.
 
You gotta love Zitto.

Haya ndiyo nilikuwa nazungumzia the other day niliposema tunahitaji issues zenye kishindo, sio kulalamika na marginal issues.

Sasa hapa CCM, kwa watu wenye akili zao, wameonyesha kujigamba kwamba wako clean halafu Zitto kawaambia why should we take your word? Why can't we conduct an audit, from a supposedly neutral observer and then find out for real?

Brilliant proposition.

My only major concern is that the AIG is no beyond the clutches of CCM and may be compromised.

I agree with you that there'll be limitation of scope, but for "Contoller & Auditor General" (CAG) to be seen as independent he has to choose one of the big four (i.e PwC or EY or KPMG or Deloite) to perform an audit for "all Political parties"
 
Swala la EPA limewafikisha CCM pabaya ingawa wamejaribu kumuuzia kesi Manji; hata hivyo huyo marehemu baba yake alikuwa haishi hapa sasa hizo fedha alikuanachukuaje? Kuna mtu aliyekuwa anaonekana benki mara zote fedha zilipokuwazinachukuliwa na huyo mtu ni Rostam na hivyo ndivyo wasemavyo watu waliokuwa wanamlipa benki!! Sasa kutuzuga zuga kuwa eti Kagoda ilikuwa kampuni ya marehemu baba yake Manji ni uongo mkubwa. WAdanganyika tumezinduka hatuamini hizo fix zenu!!
 
Swala la EPA limewafikisha CCM pabaya ingawa wamejaribu kumuuzia kesi Manji; hata hivyo huyo marehemu baba yake alikuwa haishi hapa sasa hizo fedha alikuanachukuaje? Kuna mtu aliyekuwa anaonekana benki mara zote fedha zilipokuwazinachukuliwa na huyo mtu ni Rostam na hivyo ndivyo wasemavyo watu waliokuwa wanamlipa benki!! Sasa kutuzuga zuga kuwa eti Kagoda ilikuwa kampuni ya marehemu baba yake Manji ni uongo mkubwa. WAdanganyika tumezinduka hatuamini hizo fix zenu!!

Nani alisema hivyo kwamba Kagoda mali ya babake Manji? Ndio nasikia kwa mara ya kwanza.
 
Hivi sheria ya Jamhuri inasema nini kuhusu hili la Zitto?, au ndiyo yale yale ya mapungufu ya sheria za Jamhuri yetu?

Yaani kweli tutaendesha taifa kwa kupigiana makelele, yaani mimi huku natoa na wewe huko toa tuone nani msafi, just like that on the national level? is that so? Pleeeease sheria guys!
 
Alisema hesabu za CCM zilikwishakaguliwa na Msajili wa Vyama Vya Siasa ambaye hufanya kazi hiyo kwa mujibu wa sheria.

"Kila mwaka hesabu zetu zimekuwa zikikaguliwa na si za chama chetu tu na hata vyama vingine vya siasa. Sisi hatuna cha kuficha, kama wapo wengine wanataka kukagua waje tu, ila anachosema Zitto ni porojo zisizo na maana," alisema Waziri Chiligati.

- Kumbe sheria ipo sasa tatizo lipo wapi?
 
Sioni tatizo katika kutumia fedha nyingi katika kampeni za uchaguzi ,na kama lipo hebu tuanikieni hapa tuone faida na athari kwa vyama vingine na wanainchi kwa ujumla ?

Nguvu za kampeni naweza kusema zilikuwa kubwa kwenye vyama vingine vya upinzani na pengine viliishinda CCM ,hata kwenye mikutano ilidhihirika hivyo kuwa mambo ni 50/50
Nafikiri yapo mambo ya kuzingatia katika harakati za uchaguzi na khasa kwenye upande wa ulinzi na usalama wa wananchi ambao huonekana kuburuzwa na kusumbuliwa na vyombo vya dola wakati wanapohudhuria mikutano ya vyama vyao ,aidha kuna mitafaruku ya kugombea viwanja vya mikutano ikidaiwa kila mmoja alikuwa au ana haki ya kufanya mkutano kwa siku hio au wakati huo ,hizi ni mbinu ambazo hutumiwa na CCM na tume ya uchaguzi kuanzisha kutoelewana katika siku na saa ya mkutano. Kwa mikakati hiyo inayowekwa na CCM na kupewa nguvu na tume na vyombo vya dola ndipo pale unaiona CCM inakuwa na ruhusa ya kufanya mkutano na wapinzani kutimuliwa na FFU ,jambo hili kisaikolojia linawapa hisia wananchi kuwa bado au CCM ndio chama chenye nguvu ,kitu ambacho si kweli , matumaini yangu ni kuwa wapinzani wawe makini katika jambo hili na walipatie kibali kisheria kwa makosa ambayo yanaonyesha yanatatanisha mhusika anaetoa vibali kwa kuchonganyisha awe ndie anaebeba dhamana kwa fujo ikiwa kutatokea mapigano kati ya wananchma kwa wanachama au na polisi na kufikia kupata vilema au kupoteza maisha ,ingawa inaonekana ni uzembe wa tume lakini sivyo mambo haya yanapangwa kwa makusudi ili kuipa nguvu CCM.

Ikiwa wananchi wanaelewa kuwa chama fulani ndio chaguo lao na CCM sio chaguo la wengi basi hata CCM ikatumia hazina yote ya Taifa bado hawataweza kubadili mawazo ya wenye msimamo mkali ambao wameamua kutaka mabadiliko na fedha na mali waliyokuwa nayo CCM haitowasaidia kitu , tumeona Pemba ambako fedha za CCM hazikufua dafu ,wananchi wame elimishwa na wamefahamu na kuelimika kuwa sasa CCM basi ,muda waliokuwa madarakani umetosha na hadi hii leo nyimbo ndio hiyo hiyo hata CCM wafanye kitu gani ,wananchi wameshajaa kasumba ya kuwa CCM haina nafasi tena katika ngazi ya Utawala wa Nchi na ndio kila msimu CCM wanapigwa na chini,kama mmesikia eti wanapeleka umeme Pemba kupitia Hale Tanga ,ila watu wa Pemba washaanza kuimba kuwa hakuna utawala wa CCM utakaochaguliwa kwa ridhaa zao kwani muda wa CCM kutwala umekwisha,hivyo elimu inayotakiwa katika kampeni za kuing'oa CCM si kugombea fedha bali ni kuzidi kuelimishwa kwa wananchi waikatae CCM na kuelezwa kuwa muda wa Chama cha CCM kuwepo madarakani umetosha ni wakati wa kubadili Chama Tawala ,hii ni kasumba ambayo ni lazima kwa hali yeyote ile iwe inatolewa katika kila mkutano wa Chama Pinzani kuwaeleza wananchi mpaka wananchi wataelewa na kuifahamu ,ni kama kuwafundisha watoto wa darasa la kwanza a,e,i,o,u mpka inakuwa kama nyimbo hata utakapomuona mtoto barabarani utaona anaimba a,e,... na inakuwa ni nyimbo na mazoea kabisa ,hivyo CCM ni lazima ikwamishwe kwanza kwenye mawazo ya wananchi ,isafishwe kwenye mawazo ya wananchi na njia za kuisafisha ni kuwafundisha wananchi kuwa CCM basi,isipewe muda mwengine ,muda iliotawala na kuiongoza Tanzania umetosha........! Lakini mambu ya kuwabana CCM katika matumizi yao na wapi walipata feza ,kuwabana katika mikataba feki,kuwabana kwenye rushwa huko hakutatufikisha mbali wakati badu mwananchi anaimba CCM ndio baba huu wimbo lazima kwanza uondolewe kwenye akili za wananchi.

Siku hizi huwasikii viongozi wa CCM wakisema CCM JUU na wananchi wakiitikia JUU JUU JUU Zaidi kwa maana kwa kiasi fulani wananchi wameshafuta nadharia ya kuona CCM iko juu ila bado kuna vikolombwezo vya kasumba ya CCM ndani ya wananchi hii ni lazima nayo iyondolewe kwa haraka sana ili kupata muelekeo mzuri wa wananchi ambao watakuwa hawaimbi tena CCM ndio Baba bali watakuwa wanaimba CCM basi,muda wa madaraka yao umetosha.

Chama kinachokubalika hakihitaji fedha nyingi bali kinahitaji wananchi wenye muamko wa kisiasa na kimaendelea kama walivyo Wapemba nao tumeongezea na wa Tarime. hizi ni sehemu ambazo CCM imeshakatishwa tamaa na kushinda kwa mara nyingine itakuwa ni miujiza ,ila kama wananchi wa Tarime wanaimba Muda wa CCM kutawala na kuongoza Tanzania umekwisha ,nyimbo hiyo tu ienee wilaya zote na imfikie kila mwananchi si kwa redio za umeme bali ni kutumia redio za Zanzibar ambazo wenyeji wamezipa jina na kuziita Redio kifua ambazo habari zake zinamfika hata yule asiefahamu redio ni kitu gani.

Kwa mfano hii operation Sangara ,hii iwe ni chachu ya kueneza habari za kuikwamisha CCM katika mawazo ya watu kwa kuwafundisha kuwa Utawala wa CCM umetosha ,muda wa CCM kuwepo madarakani umetosha piga uwa galagaza lakini CCM imefikia mwisho wa utawala wake.
Money can not buy Love ,late people hate them first. Maana CCM bado wanakimbilia kwa wananchi wakijua badu wanaichi wanaimba CCM ndio Baba.
 

Kumbe sheria ipo sasa tatizo lipo wapi?

Tatizo ni kwamba ukaguzi ambao Chiligati anasema umefanywa ni ule ulofanywa na mkaguzi wa CCM!

Jinsi sheria ilivyo, chama kinatakiwa kimpelekee Msajiri ripoti ya akaunti zake ambazo zimeshafanyiwa ukaguzi tayari. Ni jukumu la chama ku hire mkaguzi wao wanaomtaka wao. Kwa hiyo, kama kada wa chama Chiligati anae cousin ambae ni mhasibu basi huyu cousin anaweza kufanya ukaguzi wa akaunti za CCM halafu wakaupeleka kwa Msajiri wa vyama.

Gazeti ni bovu kwa sababu haliku double check alichopotosha Waziri Chiligati (kama kweli alisema ) kwamba ni msajiri ndio anafanya ukaguzi wa kihasibu. Sio kweli. CCM wanaweza kumpa madaftari mtu yeyote yule afanye ukaguzi almuradi ni mhasibu. Zitto anataka mkaguzi kutoka nje ya CCM.

THE POLITICAL PARTIES ACT, 1992-5, Sect. 14 (1)(b)( i )
Submission of Accounts and Declaration of Property

Every political party which has been fully registered shall submit to the Registrar an annual statement of the accounts of the party audited by an auditor registered as an authorised auditor and the auditor's report on those accounts
 
Hoja hiyo ni ya msingi,kama CCM wanauhakika na kile wakisemacho wamruhusu CAG afanye ukaguzi huo tena ikiwezekana awa consult Ernst&Young tuone mziki utakavyo kua hapo!!
Maana tutacheza wimbo uleee wakila siku!!Mafisadi hao!!
 
Ingieni kwenye Tovuti maridhawa ya CAG msome ripoti zake hasa kuhusu MSAJILI, utaona kuwa ripoti ya hivi karibuni na ile iliyopita vyote vinaonesha kuwa CHAMA hakiku-comply na hata baada ya kuambia hakiku-comply bado kiliendelea kuto-comply!Ndio maana tunasema CAG apewe meno ya ku-enforce compliance!Njia mojawapo ni ku-prosecute wasio-comply na kurudia kuto-comply!
 
Lamadi haiko mkoani Shinyanga bali iko mkoani Mwanza

Sasa hii inabadilisha kitu gani katika thread yetu, badala ya kuchangia mada ili tusaidiane kumkoma nyani kwenye paji lake la uso unatafuta typing errors.

ndiyo tulivyo
 
Hivi sheria ya Jamhuri inasema nini kuhusu hili la Zitto?, au ndiyo yale yale ya mapungufu ya sheria za Jamhuri yetu?

Yaani kweli tutaendesha taifa kwa kupigiana makelele, yaani mimi huku natoa na wewe huko toa tuone nani msafi, just like that on the national level? is that so? Pleeeease sheria guys![/
SIZE]


Heshima mbele mkulu ES,

Mimi ningependa sana mbali na yote UCHUNGUZI WA CAG UFANYIKE KWA KIPINDI CHA JANUARY 2005 - DECEMBER 2005 waanishe fedha zilizoingia zilitoka wapi na zilizotoka zilikwenda wapi na kwa madhumuni gani, kwa sababu kipindi hiki ndicho chechenye, kipindi muafaka.

MJ
 
Waipeleke kampuni ya KAGODA tu mahakamani katika kesi ya EPA na hayo yote ya CCM kuiba fedha BOT kwaajili ya uchaguzi mkuu wa 2005 yanajitokeza hadharani.
 
Wajamani; naendelea kusema; kelele humstua hata mdudu au tembo porini; CCM wapigiwe makelele ali mradi kuwe na watu wanaopiga makelele kuhusu hili; tumewazoea kupuuza ukweli; hata Richmond CCM ilipuuza; hata EPA Slaa alitolewa mkuku na Sitta bungeni; hata walimu ilitaka viongozi wawekwe rumande(Chiligati alisema jamani puu hata ktk haki ya mtu), wanafunzi ndio kabisa maana inahusu maslahi yao, wazee EAC hamna kitu; Ndege ya rais, Buzwagi mpaka Zitto akafukuzwa;
Mapambano ndio yanaanza; tupaze sauti watakimbia wenyewe; dalili zimeshaonekana wazi wazi; mafisadi watakimbia nchi na CCM itakimbia nchi;tutabaki wazalendo tukianza kujenga nchi yetu; Zitto wewe fanya kazi; simama hapo hapo hakikisha kinaeleweka; CCM watakimbia wenyewe; JK atakimbia mwenyewe; hamna haja ya kulumbana; Mada mbele kwa mbele wananchi waelewe zaidi.
Pia Mwana mama wa CUF kule Mbeya anakubalika; nashauri kama inawezekana kuforge uhusiano ili apitishwe kwa ushirikiano wa CUF/Chadema tu ( wengine hapana) kuongeza nguvu; bungeni msigawane kura chonde chonde
 
Tatizo ni kwamba ukaguzi ambao Chiligati anasema umefanywa ni ule ulofanywa na mkaguzi wa CCM! Jinsi sheria ilivyo, chama kinatakiwa kimpelekee Msajiri ripoti ya akaunti zake ambazo zimeshafanyiwa ukaguzi tayari. Ni jukumu la chama ku hire mkaguzi wao wanaomtaka wao. Kwa hiyo, kama kada wa chama Chiligati anae cousin ambae ni mhasibu basi huyu cousin anaweza kufanya ukaguzi wa akaunti za CCM halafu wakaupeleka kwa Msajiri wa vyama.

"Alisema hesabu za CCM zilikwishakaguliwa na Msajili wa Vyama Vya Siasa ambaye hufanya kazi hiyo kwa mujibu wa sheria."

- Very weak argument, kwani sekta zote za serikali si zinaongozwa na CCM compromise au?

Yaani kweli sasa tutaanza kuongoza taifa na makelele ya haya fungua vitabu vyako huko na mimi nafungua huku unaona! unaona!, kwani sheria iansema nini?

Mheshimiwa Zitto twende kule kwenye sheria tunahitaji ushaidi dhidi ya mafisadi mkuu, lete ushahidi wa Karamagi na mikataba ya London tufunge mafisadi kwanza, one at a time!
 
Back
Top Bottom