Zitto aitibua CHADEMA


you got a point. tatizo langu however ni kwa chama cha siasa kuanza kutengeneza miungu watu ndani yake.

je, hivi ni kweli kuwa bila ya Zitto, Mbowe, Slaa, etc Chadema hawawezi kusimama? kama huo ndiwo ukweli, basi sidhani kama this is a party that should be taken seriously and relied upon to run a govt.

lakini kama Chadema is an institution as it would be expected, sikubaliani kabisa na dhana ya mwanachama au mtu awaye yote kuanza kutoa masharti dhidi ya such an established institution.

siukumbuki vizuri mchakato uliopelekea Zitto kuondolewa chamani lakini i suppose lazima kutakuwa kulifanyika mawasiliano rasmi kimaandishi kwa Zitto kumfahamisha kuhusu uamuzi huo. sasa kama Zitto anaona alionewa na tayari ameonyesha utashi wa kurudi chamani, kwa nini washauri wake wasimshauri kuwa aanzie hapo without necessarily involving the media?
 
You just hit the nail on the head!

Kuna sehemu nimeeleza katika maudhui kama uliyoeleza.

Kwa sasa wafuasi wa Mhe. Zitto wanaweweseka kwa sababu hawafahamu msimamo wake.

Kuna wengine hapa wanapiga kelele wakisema hawataki Zitto arudi CHADEMA lakini hawafahamu kuwa wanaishi katika maneno ya Mbowe na Dkt. Slaa.

Siku Mbowe au Dkt. Slaa wakubaliane kuyamaliza na Zitto, hata kauli za wale waliokuwa wanapinga zitabadilika.

Tutawasikia wakisema, Oooh, hakuna adui wa kudumu au rafiki wa kudumu.
 
Kwa ushauri tu kwa sasa viongozi wa chadema wasijadili kitu chochote kuhusu Zitto hata kama atakuwa anaropoka waachane naye. Wasimfukuze wala wasijadiliane naye chochote maana yeye kwasasa hana tofauti na mimi pale chadema ukiondoa ubunge alio nao. Wakifanya hivyo hata hilo neno sharti litakufa natural death. Akiamua kuondoka mwenyewe chadema itakuwa ni nzuri zaidi kwa chadema lakini akibaki basi kusiwe na mjadala.
 

makosa yake alisha somewa siku anapewa adhabu, kama anayaona hayana ukweli hana haja ya kuyaombea msamaha, abaki aliko, hivi ni lazima zitto awe cdm?
 
Zitto aende akaendeleze chama chake cha ACT !. Alianzisha chama hiki akishirikiana na Kitila na wapuuzi wengine ili kupambana na CDM !. Sasa ameona project yake ya ACT imebuma eti ndio arudi tena CDM !

Hafai kabisa huyu dogo na sidhani kama atabadilika katika kufanya usaliti na ubinafsi !. Huyu dogo nime-study tangu 2009 na nimejiridhisha hawezi badilika.....

 
Issue ya Zitto ni kati ya yeye na Chama si yeye na Mbowe !. Hatua alizochukuliwa zilichukuliwa na kamati kuu na si Mbowe peke yake !

Vile vile Zitto alipoamua kwenda mahakamani ndio amejifukuzisha mwenyewe kwa mujibu wa katiba ya Chama.....

By the way si ana chama chake cha ACT ambacho alikianzisha kupambana na Chadema ? Sasa anataka arudi Chadema kufanya nini ? Si aliona yeye ni zaidi ya Chama ?

Abaki na ACT yake akishirikiana na wasaliti wenzake (Kitila, Mwigamba na wapuuzi wengine).....


Mwenyekiti nae anataka kutuaminisha hiki chama ni chake sasa, kwani kuna shida gani wakasameheana kujenga upinzani wenye nguvu, najua Zitto amejutia usaliti wake na sidhani kama atarudia tena, asamehewe tu.
 
Watu humu ndani mnaongea sana.yani hata hukumu mahakanani haitolewi hivi.mtu lazima ajitetee ajue kosa lake kisha Kama kuomba radhi ndio aombe .Na Kama ameonewa je?ndio maana nayeye anataka kuwe na masharti kwenye kurudi.

hawezi somewa makosa mara mbili ili aombe msamaha kama anaona alionewa sio lazima awe chadema ila awe mpinzani
 
Mbowe ameogopa masharti ya zitto akijua wazi kuwa yeye ndio mwenye makosa. Kwanini asikubali kutoa ushahidi kama ni kweli zitto ana kosa
 
Yalikuwa maamuzi ya kamati kuu si ya Mbowe na Slaa pekee,

By the way watamsamehe kwa makosa yapi ? Kwani Zitto amekwambia amekosa ?

Viongozi wangu Mbowe na Dr Slaa, tunawapenda sana pia tunawaamini, hebu msameheni Zitto, tunataka tuone ile triple army kama ya zamani, msameheni bila masharti.

Zitto na wewe hebu tunaomba utulie kamanda, epukana na kauli tata tujenge chama.
 

Wale vilaza waliokuwa wanatumiwa kumchafua Zitto ndo hawataki jamaa arudi kundini maana wanajiona mabwege wakutupa.

Kama makosa yake yanaushahidi mnashindwaje kumwambia ili asije kuyarudia badala yake mmeanza ngonjera?

.
 
Vikao gani ulikaa na wanachama wepi hata uje hapa usema eti wanachama m-mebariki ?!

 
..nilichokueleza mimi ni "POLITICAL REALITY."

..kisiasa Zitto ni muhimu na mtu mzito kuliko Mwigamba na Mkumbo.

..kama unabisha hilo waambie Mwigamba au Mkumbo waendelee na ACT yao bila Zitto Kabwe.

cc Pasco, Ghostryder
Sikatai kuwa Zitto ni popular figure ukilinganisha na Mwigamba au Prof. Kitila.

Inaeleweka mtu ambaye anafanya kazi za kisiasa akiwa background kama ilivyokuwa kwa Prof. Kitila hawezi kuwa popular kwa wananchi kwa sababu hawamfahamu.

Zitto amekuwa frontline katika siasa kwa muda mrefu lakini vile vile sikatai kuwa ana kipaji katika siasa za frontline.

Umenichekesha sana!

Kwa hiyo ACT without Zitto is dead and buried!
 

Hebu tuache uongo, kati ya vyama hivi 4 vinavyounda UKAWA kipi maarufu kukizidi CDM?
 
Kama umenielewa vizuri, kabla ya kuombana msamaha, kitu cha kwanza ni kuwepo maridhiano, ambapo mkosaji atakubali kosa lake, ila kwa vile Chadema ndio baba, baba hawezi kuomba msamaha kwa mtoto, ila lazima afanye gestures za kutambua kosa lake alilomtendea mtoto, na mtoto kwa kujua baba ametambua kosa lake, amelijutia, atasamehe na kusahau ndipo wasonge mbele!.

Hili la mbona CCM haijajishusha, inamaanisha kwako model ya vyama bora ni CCM?!. hivyo kila CCM inachofanya ndio the right way?!.

Msamaha wa kweli unatokana na kutambua makosa na kuyajutia makosa hayo ndipo msameheane!.

Chadema ina viongozi myopic wasiona mbali!, in a wanasheria nguli wasio na uwezo wa kufuata sheria taratibu na kanuni, na kibaya zaidi hawana kabisa uwezo wa ku determine legal consequences of their illegal questions ndio maana sio tuu chama kinafikia level ya kuwakumbatia wahalifu, bali hadi kuwaacha makada wake, wakiendesha uhalifu huku wakiwapongeza!. The consequences za kesi ya Zitto sio nzuri kwa Chadema hata kidogo, Zitto katika kutafuta haki yake, atajikuta ni lazima ataibomoa Chadema, thank God nili overhear kashauriwa na kakubali kufuta kesi, na hii ndio salama yao.

Kwa sasa Chadema inajijua inapendwa, hivyo inajiona "kidume!", kufikia kufanya baadhi ya mambo ya hovyo, mengine ya kijinga kwa ukosefu wa busara kidogo tuu, huku Wanachadema wenyewe wakisifu ujinga!.

Kwenye ule uzi wangu, CCM Imechokwa; CHADEMA Haijajipanga!, nilisisitiza
Pasco
 
I think approach ya Zitto ni sahihi, kwa kiwango kikubwa ugomvi wao ulichangiwa na mwenyekiti kufuata ushauri wa vifaranga.

Msingi wa maridhiano ni ukweli uzungumzwe, wakosefu wajulikane na kisha msamaha ufuatie, approach hiyo itasaidia kuhakikisha ujinga ulosababisha utengano usirudiwe tena, kwani thru face to face discussion, waongo na wafitini mf akina saa8 watajulikana.
 
Hanashidana msamaha huyo akafie mbali na ACT kama ni machozi tumesha lia mpaka ya mekauka.

Tumesha anua matanga tayari asije akatuliza kwa mara nyingine tena.b
 
Nyie ndio mnampa Zitto kiburi na yeye kujiona kama vile yuko katika level moja na Chama.....

Ninamsikitikia kwa sababu akiona maneno kama yako na wengine kama wewe basi anaona kwamba yeye ni mtu wa muhimu sana pengine hata kupita Chama na hivyo Chama kinaweza kumnyenyekea yeye..........

Kwa kujiona hivyo, akaanzisha chama chake cha ACT akishirikiana na wasaliti wenzake akifikiri watu wataondoka CDM na kumkimbilia yeye !.

Sasa nini kinamfanya asiendelee na ACT yake ? Yeye si maarufu zaidi ya CDM ?

Mgogoro ulipoibuka mwishoni mwa mwaka jana tuliyumba kidogo mainly kwa sababu CCM na serikali yake walijaribu kuukuza mgogoro kwa propaganda za kipuuzi......Mgogoro umekuwa managed vizuri na CDM na tupo vizuri na tunaendelea Mbele !

Zitto aende akaendeleze chama chake cha ACT !



 
Salama yako ni hii kauli yako kwenye bold, vinginevyo ningejua tunajadili na watoto waliozaliwa leo!.
Maadani ni hukumbuki vizuri, then its ok, ukitulia utakumbuka!, ila ingekuwa huujui mchakato huo, hapo tungeelimishana!, ila kwa kukusaidia tuu, Zitto hajaondolewa Chadema bali alivuliwa nyadhifa zake zote ndani ya Chadema kinyume cha sheria, taratibu na kanuni za Chadema!.

Pasco.
 

Pasco tukisema na wewe umechagua side kabla ya kujua detail ya pande zote au angalao kuweka tahadhari "For the least info niliyonayo"

Halafu ondoa huo ushauri wako wa chama kumnyenyekea mtu.Huo ni ushauri mbaya kabisa kati ya ushauri niliowahi kukutana nao siku za karibuni.
 
Last edited by a moderator:
Hanashidana msamaha huyo akafie mbali na ACT kama ni machozi tumesha lia mpaka ya mekauka.

Tumesha anua matanga tayari asije akatuliza kwa mara nyingine tena.b
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…