Speaker Anne Makinda akiwa hospitalini Mhimbili kumjulia hali Zito Kabwe, na anasema hali yake si mbaya sana. Bunge linafanya mpango wa kumsafirisha nje kupata matibabu zaidi, na taratibu zikikamilika taarifa itatolewa.
anaendelea vizuri lakini atapelekwa India???????
siku hizi watu hupelekwa India kwa malaria na homa???????
kuna kitu hatukijui.....unknowns unknowns.....
Dah, mwanzo sikupenda kushtuka sana na hali ya Mh, Zitto lakini sasa naanza kuogopa...Inshaallah Mwenyezi Mungu atampa uzima. Naomba sana mtu yeyote aliye karibu naye atueleze kwa ufasaha kimetokea nini na nini hali ya Zitto maanake nashangaa sana kuona viongozi wa Chadema kimyaaa! - Whats going on?Kuna mambo bado hayajakaa sawa hapa. Kutokana na maelezo ya Dr Kashilila (katibu wa bunge) Muhimbili wamegundua kuwa Zitto alikuwa na malaria. Wote tunajua kabla ya kupelekwa Muhimbili Zitto alikuwa amelazwa Agha Khan Hospital, hivi kweli Aghan Khan walishindwa kugundua Zitto alikuwa na malaria? Na kama Muhimbili wamegundua malaria kwa nini wanaongea kumpeleka India? Muhimbili hawawezi kutibu hata malaria siku hizi?
Kwa ujumla haya majibu yanaancha nafasi ya rumours zaidi kuliko kutuliza akili za watu.