Kiongozi Mkuu wa ACT-
Wazalendo, Zitto Kabwe
amesema anakusudia kuwa
mbunge wa Kigoma Mjini kwa
kipindi kimoja cha miaka mitano
kuanzia 2015 hadi 2020, kabla
ya kuomba kazi nyingine ya
kufanya kwa Watanzania.
Mbunge wa Jimbo hilo kwa sasa
ni Peter Serukamba wa Chama
cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza baada ya
kujiandikisha katika Daftari la
Kudumu la Wapigakura katika
Kituo cha OTTU Mwanga Mjini
Kigoma juzi, Zitto alisema ana
dhamira ya kuhakikisha ACT
inashinda majimbo yote manane
katika Uchaguzi Mkuu mkoani
hapa.
Tumejipanga vizuri kushinda
majimbo yote ya Mkoa wa
Kigoma, lakini tuna uhakika wa
kupata nusu ya majimbo mkoani
Tabora na lazima tupate majimbo
yote ya Kahama. Tumejipanga
vizuri kushinda bila shaka baada
ya Oktoba 25 watu watajua hiki
tunachokisema leo, alisema
Zitto.Chanzo:Mwananchi