Frumence M Kyauke
JF-Expert Member
- Aug 30, 2021
- 630
- 1,245
Katika mahusiano kumekuwa na tabia ya wanaume kukimbia ujauzito na kutelekeza watoto pasipo sababu za msingi. Ukizingatia kuwa mwanaume ndiye aliyemshawishi mwanamke kwa kinywa chake mwenyewe kwamba washiriki tendo la ndoa.
Wanawake wamekuwa mstari wa mbele kuhimiza matumizi ya kinga huku wakifahamu fika kuwa wao ndio wanaobeba ujauzito lakini wanaume wamekuwa wakitaka kushiriki tendo la ndoa bila kinga na ujauzito unapotokea basi wanaume wanakuwa wa kwanza kukimbia majukumu ya kulea kichanga sababu inayowapelekea wanawake kuharibu ujauzito.
Wakati mwingine nimekuwa nikijiuliza pengine wanaume wamekosa uwezo wa kulea watoto lakini la hasha! Wapo wanaume matajiri wanaotelekeza ujauzito na inapelekea mtoto kuzaliwa na kuishi maisha duni ingawa baba yake anamiliki mali nyingi.
Je zipi sababu za wanaume kutelekeza ujauzito?
Wanawake wamekuwa mstari wa mbele kuhimiza matumizi ya kinga huku wakifahamu fika kuwa wao ndio wanaobeba ujauzito lakini wanaume wamekuwa wakitaka kushiriki tendo la ndoa bila kinga na ujauzito unapotokea basi wanaume wanakuwa wa kwanza kukimbia majukumu ya kulea kichanga sababu inayowapelekea wanawake kuharibu ujauzito.
Wakati mwingine nimekuwa nikijiuliza pengine wanaume wamekosa uwezo wa kulea watoto lakini la hasha! Wapo wanaume matajiri wanaotelekeza ujauzito na inapelekea mtoto kuzaliwa na kuishi maisha duni ingawa baba yake anamiliki mali nyingi.
Je zipi sababu za wanaume kutelekeza ujauzito?