Zip/postal codes ya Dar es salaam

Zip/postal codes ya Dar es salaam

Siku moja nikawa najisajili kwenye yahoo, nilipofikia kwenye zipocode kijasho kiliaza kunitoka maana kila nikajaribu kubuni namba naambiawa wrong! lakn baadaye nikaweka p.o.box la shule niliyosemea ikakubali hadi leo napeta na yahoo answer kwa kwende mbele.
 
Zip code zipo website ya TCRA, kwa ukanda wa Ubungo + udsm ni 14115. Wataka zip code ya eneo lipi Dar?
 
mbona mnakuwa kama serkali ya Magamba kila mtu na lake.
 
Usinichoshe.
Hivi lini tunaenda kumsalimia mgonjwa wetu? Manake inabidi uonje raha ya ndege masaa mengi mengi, hadi unatimiza haja hewani.
Aha aha aha ahaaaaaaa king'asti itabidi nikusake bhana unitoe ushamba na hapa.....maana dunia hii bila haya mambo daah!!....
 
mi huwa nikijaza +255 kwenye swali au space ya aina hiyo,form huwa haikatai na inaenda. Au labda malaika wa bwana huwa ananisaidia! Ngoja wataalamu waje.

bwana na malaika zake awae nawe siku zote za maisha yako mkuu
 
Mambo mengine bwana shida sana. Niliwahi kutumiwa kipaseli, kwenye anwani pameandikwa postcode. Mfanyakazi wa posta eti anauliza hii namaba ni ya nini?
Nilipomwambia ni postcode ya mahali ninapoishi sasa eti akauliza kama nimeibuni mwenyewe, ebo!

Get your postcode here

 
zip code inatumika marekani. ..mi nipo uingereza na natumia postcode, huu ni mfumo wa kidigital wa kutambua eneo husika, maeneo ya ulaya yamegawanywa kwa postcode hivyo inawarahisishia watu wa mail na courier kukuletea barua/kifurushi chako mpk mlangoni (kumbuka ulaya na marekani barua unaletewa nyumbani, na kila nyumba ina namba na pia kila mtaa una jina. ....ila mitaa na namba huwa zinajirudia lkn postcode ya eneo husika huwa haijirudii sehemu nyingine).....Tanzania hatuna mfumo huo na bado tunatumia p.o box
Upo vizuri mkuu. Inaonekana una weledi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom