Zingatia mambo haya ukiwa gerezani

Notorious thug

JF-Expert Member
Dec 29, 2021
2,817
10,596
Gerezani ni sehemu ngumu sana na isiyoelezeka kwa mambo yaliyopo kule ili kupunguza makali ya gerezani unaweza fanya haya mambo.

1-Mfungwa hachagui gereza ni kweli ila unaeza kuchagua gereza wengi wanapohukumiwa huingia gerezani hapa unaeza kutambua gereza ulilopo ni la kilimo au vipi kama ni la kilimo fanya juu chini wewe na ndugu zako uhamishwe hapa ni wewe kusuka mipango na mabwana wakubwa toa fungu ndugu yangu utafia shambani. Bora ukae gereza la mjini huku kazi ni ndogo ndogo magereza ya kilimo ni mateso kazi ni ngumu vifaa butu askari wakali nyapara hawana huruma mbele bunduki nyuma fimbo.

2-Hela ya kula. Gerezani mlo ni mmoja saa nane achana na uji mlo wa gerezani ni kukufanya usife njaa ila sio mlo wa kula mwanadamu wakuu sasa hapa unaweza kuacha hela kwa mapai kwa mwez ukawa unapata msosi kutoka kwa wake za wadau wa pale ongea na ndugu zako angalau waache laki kwa mwezi kama inawezekana usijepata vidonda vya tumbo.

3-Nidhamu. Gerezani nidhamu unafundishwa kwa lazima ila watu sugu wapo pia epuka makundi gerezani utapata shida sana kuna wafugwa wao ni watata labda kuzaliwa au makabila kuna mfugwa alikua ni Mmasai kabila huyu alikua si mwelewa anaeza akaanza kkushambulia muda wowote kutokana na msongo wa mawazo na namba aliyokula kutoka ni 2035 watu kama hawa usijenge urafiki nao akili hua zinafyatuka.

4-Uongozi. Hapa namaanisha upate kitengo kizuri jikoni hua ni ngumu ila unaweza kupata uongozi wa kuongoza wenzako mnapokua kazini simaanishi uwe nyapara hapana unyapara unapewa kwa kuangalia muda uliokaa gerezani na nidhamu yako, hapa nazungumzia kusimamia genge mnapokua kazini kumbuka gerezani kazi ni nyingi na watu ni wengi muhimu ni wewe upatee nafasi ya kuwasimamia vinginevyo mikono itaota sugu na ngozi itapigwa jua kama la mbarali.

5- Marafiki. Anzisha urafiki na askari gereza ambaye labda ni kabila lako lafudhi hazipotei utaweza kumgundua huyu atakusaidia utakapokua mgonjwa au kwenye mambo mengine madogomadogo, askari mara nyingi hua wakali sana ila hamna mwanadamu anayekosa chembe chembe ya huruma atakusaidia kwa kujua huyu ni wa nyumbani. Pia kuna viongozi wa dini ambao ni wafugwa pia hawa watakusaidia kiroho na kukushauri ni watu muhimu pia.

6-Punguza mawazo. Hamna jambo gumu kama kuishi mbali na familia baba,mama,dada,kaka,mke na watoto utakua unawaza sana kuhusu maisha yao na pengo lako jipe moyo sana na jione bado wewe ni mtu kwenye jamiii. Unapokua na kifungo cha chini ya miaka30 ina maana bado una nafasi ya siku moja kutoka gerezani na kuendelea na maisha yako kma zamani usiangalie mwaka utakao toka utakata tamaa wewe amini tyu nitatoka siku si

7-Jifanyie usafi, linda afya yako. Ngozi yako epuka kushare share baadhi ya vitu unapokua kule ndani namaanisha sabuni na vitu vingine unavyokua navyo kwa siri. Jipende usijisuse ni hali ya muda soon utarudi ulaya(uraiani)

8- Usipende kudadisi wenzako mambo yao au kesi zao acha wao wakuambie vinginevyo wewe pambana na yako,wakili wako endelea kua na mawasiliano nae kupitia ndugu zako kuandaa mikakati ya rufaa na mambo mengine.

N:b. Ni haya machache wadau najua mna mengi karibuni tuendelee kupeana uzoefu na mbinu kwa waliokaa na ambao hawajakaa kila mtu ni mfugwa mtarajiwa tumekaa tumetokaa huenda tukarudi WHO KNOWS!!
 
Linapokuja sawa lolote baya akili ya mwanadamu imekuwa ikilisusa bila kutegemea, ni rahisi sana kususia habari za kifo mtandaoni na kutafuta vichekesho au habari za kufurahisha, Sio bahati mbaya ila ni maumbile asili ya mwanadamu.

Lakini hoja uliyoleta mkuu ni nzuri kwa mwanadamu yeyote ambaye bado hajafikwa na umauti. Sikuwahi hata siku moja kuwaza kwamba mimi mwenyewe ipo siku ntakanyaga rumande achana na gerezani, lakini nilipelekwa rumande. Hii ilinifanya niamini kitendo cha mimi kuwa mwanaume na harakati zangu za utafutaji basi lolote linawezekana.

Binafsi nikushukru, kwa kutoa hizi "basics" ntajitahidi kuwa raia mwema, lakini wakati wa upotofu basi zitumike aidha kwangu au ndugu nitakayemshauri pia.
 
Ndio maana umejiita Notorious mkuu? Nice topic
hili waliniita wanangu wa kitaa
Linapokuja sawa lolote baya akili ya mwanadamu imekuwa ikilisusa bila kutegemea, ni rahisi sana kususia habari za kifo mtandaoni na kutafuta vichekesho au habari za kufurahisha, Sio bahati mbaya ila ni maumbile asili ya mwanadamu.

Lakini hoja uliyoleta mkuu ni nzuri kwa mwanadamu yeyote ambaye bado hajafikwa na umauti. Sikuwahi hata siku moja kuwaza kwamba mimi mwenyewe ipo siku ntakanyaga rumande achana na gerezani, lakini nilipelekwa rumande. Hii ilinifanya niamini kitendo cha mimi kuwa mwanaume na harakati zangu za utafutaji basi lolote linawezekana.

Binafsi nikushukru, kwa kutoa hizi "basics" ntajitahidi kuwa raia mwema, lakini wakati wa upotofu basi zitumike aidha kwangu au ndugu nitakayemshauri pia.
 
Gerezani ni sehemu ngumu sana na isiyoelezeka kwa mambo yaliyopo kule ili kupunguza makali ya gerezani unaweza fanya haya mambo.

1-Mfungwa hachagui gereza ni kweli ila unaeza kuchagua gereza wengi wanapohukumiwa huingia gerezani hapa unaeza kutambua gereza ulilopo ni la kilimo au vipi kama ni la kilimo fanya juu chini wewe na ndugu zako uhamishwe hapa ni wewe kusuka mipango na mabwana wakubwa toa fungu ndugu yangu utafia shambani. Bora ukae gereza la mjini huku kazi ni ndogo ndogo magereza ya kilimo ni mateso kazi ni ngumu vifaa butu askari wakali nyapara hawana huruma mbele bunduki nyuma fimbo.

2-Hela ya kula. Gerezani mlo ni mmoja saa nane achana na uji mlo wa gerezani ni kukufanya usife njaa ila sio mlo wa kula mwanadamu wakuu sasa hapa unaweza kuacha hela kwa mapai kwa mwez ukawa unapata msosi kutoka kwa wake za wadau wa pale ongea na ndugu zako angalau waache laki kwa mwezi kama inawezekana usijepata vidonda vya tumbo.

3-Nidhamu. Gerezani nidhamu unafundishwa kwa lazima ila watu sugu wapo pia epuka makundi gerezani utapata shida sana kuna wafugwa wao ni watata labda kuzaliwa au makabila kuna mfugwa alikua ni Mmasai kabila huyu alikua si mwelewa anaeza akaanza kkushambulia muda wowote kutokana na msongo wa mawazo na namba aliyokula kutoka ni 2035 watu kama hawa usijenge urafiki nao akili hua zinafyatuka.

4-Uongozi. Hapa namaanisha upate kitengo kizuri jikoni hua ni ngumu ila unaweza kupata uongozi wa kuongoza wenzako mnapokua kazini simaanishi uwe nyapara hapana unyapara unapewa kwa kuangalia muda uliokaa gerezani na nidhamu yako, hapa nazungumzia kusimamia genge mnapokua kazini kumbuka gerezani kazi ni nyingi na watu ni wengi muhimu ni wewe upatee nafasi ya kuwasimamia vinginevyo mikono itaota sugu na ngozi itapigwa jua kama la mbarali.

5- Marafiki. Anzisha urafiki na askari gereza ambaye labda ni kabila lako lafudhi hazipotei utaweza kumgundua huyu atakusaidia utakapokua mgonjwa au kwenye mambo mengine madogomadogo, askari mara nyingi hua wakali sana ila hamna mwanadamu anayekosa chembe chembe ya huruma atakusaidia kwa kujua huyu ni wa nyumbani. Pia kuna viongozi wa dini ambao ni wafugwa pia hawa watakusaidia kiroho na kukushauri ni watu muhimu pia.

6-Punguza mawazo. Hamna jambo gumu kama kuishi mbali na familia baba,mama,dada,kaka,mke na watoto utakua unawaza sana kuhusu maisha yao na pengo lako jipe moyo sana na jione bado wewe ni mtu kwenye jamiii. Unapokua na kifungo cha chini ya miaka30 ina maana bado una nafasi ya siku moja kutoka gerezani na kuendelea na maisha yako kma zamani usiangalie mwaka utakao toka utakata tamaa wewe amini tyu nitatoka siku si

7-Jifanyie usafi, linda afya yako. Ngozi yako epuka kushare share baadhi ya vitu unapokua kule ndani namaanisha sabuni na vitu vingine unavyokua navyo kwa siri. Jipende usijisuse ni hali ya muda soon utarudi ulaya(uraiani)

8- Usipende kudadisi wenzako
mambo yao au kesi zao acha wao wakuambie vinginevyo wewe pambana na yako,wakili wako endelea kua na mawasiliano nae kupitia ndugu zako kuandaa mikakati ya rufaa na mambo mengine.

N:b. Ni haya machache wadau najua mna mengi karibuni tuendelee kupeana uzoefu na mbinu kwa waliokaa na ambao hawajakaa kila mtu ni mfugwa mtarajiwa tumekaa tumetokaa huenda tukarudi WHO KNOWS!!
Watu wapo uraiani na bado wanajihisi hawana amani ya maisha, aise watu wanaoishi Gerezani wanawatamani sana mliopo mtaani(uraiani).
 
Nilitumwa kikazi gereza fulani, aiseeee kumbe kule pasikie tu, jamani nyie lile limlango lione tu ila ukiingia kutoka ni ngumu.

Basi nilivyofika nikajitambulisha nimetumwa na mamlaka fulani kumuona mfungwa fulani nikaonyesha docs anazotakiwa kusaini.

Sikupata usumbufu wowote askari walinipokea vizuri.nilikalishwa sehemu baada ya muda wakamleta nikaongea nae ila mbele ya askari.

Niliongea nae akaomba hizo documents nimpelekee mtu fulani baada ya yeyekusaini na wakagonga mhuri wa magereza kuwa kapokea.

Nafasi aloipata ni kupitia hiyo document nilopeleka ataweza pata hata wakili waongee tho nafasi ya kumsaidia ilikuwa ni ndogo.

Machache niliyoyaona ndani ni kusafi sana maua kila kitu mazingira kwa nje ni safi.

Wafungwa ambao walikuwa hawajavaa sale niliona wakiwa katika vazi zao na wasafi tu.

Nilichogundua kule kuna nidhamu ya hali ya juu.kila kitu ni utaratibu.

Wakati nikiwa pale mlangoni kwa ndani maafande walinzi walinambia mtu anapoingizwa pale kwa mara ya kwanza uamini kuwa atatoka soon ila sio kweli, kuingia ni rahisi ila kutoka sio unavyodhani.

Kwa ulinzi ule inabidi kuwa mpole ukiwaza kutoroka lazima uumie. Kwanza unaanzaje kutoroka kwa fensi ile? Fensi ndefu vile kama barabara?
Nilijifunza tuishi kwa kuwa makini ukiona mtu anataka kukuletea msala jiweke pembeni.mambo ya ugonvi, kuzurumu watu na mambo mengine mabaya tuepukane nayo.
 
Back
Top Bottom