Zima Moto taabani kwa ukosefu wa vifaa

BOB LUSE

JF-Expert Member
Jan 25, 2014
3,656
3,079
Jijini Dar zimamoto wana magari sita ambayo manne kati yao yanahitilafu.Moja linafanyakazi na lingine linahitilafu katika hayo mawili ya uokoaji!

Wizara ya mambo ya ndani wana magari mengi mpaka ya washawasha kwaajiri ya kuzima upinzani dhidi ya dola
kwanini hawanunui magari dhidi ya majanga ya moto?!

Hizi hela tunazokatwa za fire nani anakula? kweli hapa kazi ni kama kauli mbiu zingine za maisha bora/ ukuta hazisaidii mwananchi wa kawaida.
 
Ndiyo vipaumbele vyao kununua magari ya washawasha na magari ya kutuliza ghasia badala ya zimamoto na ambulance
 
kama hapa jijini mambo yako hivi.....huko wilayani,mikoani?! lazima kuwe na standard ya idadi ya vifaa stahili kwa jiji/mji/halmashauri......Hapa kazi tu.utajenga viwanda bila kuvilinda kweli? au kulinda raia na mali zao? defender/land cruiser za polisi zinatosha.....tujipange kwenye majanga please.
 
Kijan kama umekosa kazi za kufanya useme usaidiwe afu nyinyi ndo wale watoto wa kiume mnakaa hadi lao kwa mama zenu kazi kupiga umbea.....Juzi ijumaa nipo pale DIT nmeona gari za zimamoto zimeongozana mbili zikipiga kelel kuelekea posta na wakati huo ilikuwa mida ya saa moja,tumekaa pale mida ya saa mbili kasoro ikapita nyingine ikielekea huko huko maeneo ya posta jumla zinakuwa tatu...sasa wew huo umbea wa zimamoto tatu umetoa wapi...mtakuja olewa watoto wa kiume
 
Back
Top Bottom